Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA (K.n.y. MHE. EZEKIEL M. MAIGE) aliuliza:- Kilio kikubwa cha wananchi waishio jirani na Mgodi wa Bulyankulu ni kunufaika na mgodi huo:- (a) Je, ni kiasi gani cha pesa Mgodi wa Bulyankulu ulitumia katika miradi ya ujirani mwema? (b) Je, kwa nini mgodi huo hautekelezi miradi yake kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Msalala ambako kuna wataalam na gharama za utekelezaji miradi ni ndogo?

Supplementary Question 1

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Kwa kuwa yapo mazungumzo yanayoendelea kwa ajili ya ujirani mwema kati ya mgodi na vijiji vinavyozunguka ikiwemo Kijiji cha Bugarama na kwa kuwa kijiji hiki kina shida ya maji na wana mpango wa kupata maji kupitia mgodi huu. Je, Serikali iko tayari kuratibu mazungumzao haya?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikiri kwamba Mgodi wa Bulyankulu umekuwa ukitoa pia huduma za jamii katika maeneo ya Ilogi, Kakora, Runguya na maeneo mengine lakini hivi karibuni mgodi umekuwa ukifanya mazungumzo na vijiji vya jirani na tumekuwa tukiendelea kuratibu shughuli za migodi pamoja na wananchi. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali iko tayari, itaendelea kuratibu mazungumzo mpaka suluhisho la wananchi kunufaika na mgodi huo zipatikane kama kawaida.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA (K.n.y. MHE. EZEKIEL M. MAIGE) aliuliza:- Kilio kikubwa cha wananchi waishio jirani na Mgodi wa Bulyankulu ni kunufaika na mgodi huo:- (a) Je, ni kiasi gani cha pesa Mgodi wa Bulyankulu ulitumia katika miradi ya ujirani mwema? (b) Je, kwa nini mgodi huo hautekelezi miradi yake kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Msalala ambako kuna wataalam na gharama za utekelezaji miradi ni ndogo?

Supplementary Question 2

MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa niweze kuuliza swali moja la nyongeza. Mkoa wa Mbeya umebarikiwa sana kuwa na madini pamoja na vyanzo mbalimbali vya umeme. Nataka nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa mfano, kuna vyanzo vya umeme vya jotoardhi kule Busokelo lakini pamoja na Lake Ngozi, kuna makaa ya mawe, kuna maporomoko ya maji na vitu vingine katika sehemu nyingine mbalimbali. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, ni lini vyanzo hivi vitaanza kufanya kazi ili wananchi wa Mbeya na Tanzania kwa ujumla ipate umeme wa kutosha?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa, kati ya mikoa hapa nchini iliyojaliwa kwa kuwa na rasilimali za madini pamoja na maporomoko ya maji ni pamoja na Mkoa wa Mbeya na hasa Mbeya Vijijini. Nikubaliane naye, kwa sasa Wizara yetu inafanya utafiti na inakamilisha utafiti wa jotoardhi (geothermal) ambapo sasa tumegundua madini hayo yatakuwa na megawati 20 kwa kuanzia lakini baadaye tutakwenda hadi megawati 100, hiyo ni kwa jotoardhi. Bado tunafanya upembuzi yakinifu katika makaa ya mawe pamoja na maporomoko ya maji katika mito hiyo na hasa katika Mto Ngozi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hatua tunazochukua ni kukamilisha utafiti huo yakinifu na kadri itakavyowezekana tukipata fedha, shughuli ya kutekeleza miradi hiyo itaanza. Mradi wa geothermal unaanza kutekelezwa mwezi Julai, 2017.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA (K.n.y. MHE. EZEKIEL M. MAIGE) aliuliza:- Kilio kikubwa cha wananchi waishio jirani na Mgodi wa Bulyankulu ni kunufaika na mgodi huo:- (a) Je, ni kiasi gani cha pesa Mgodi wa Bulyankulu ulitumia katika miradi ya ujirani mwema? (b) Je, kwa nini mgodi huo hautekelezi miradi yake kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Msalala ambako kuna wataalam na gharama za utekelezaji miradi ni ndogo?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda Waziri atuambie, kwa migodi kama ya Kiwira ambayo tayari inazalisha, je, tunapata kiasi gani kama Halmashauri?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nifanye masahisho kidogo, Mgodi wa Kiwira haujaanza kazi rasmi, uko katika kukamilisha detailed design na hatua za kumpata mkandarasi kwa ajili ya kuanza ujenzi. Hata hivyo, mgodi huo utakapoanza, Halmashauri zote zinazohusika zitanufaika na mambo yafuatayo. La kwanza, Halmashauri zitakuwa na uwezo wa kukusanya service levy ambayo ni asilimia 0.3. Kadhalika zitaweza kupata mrabaha ambao utaingia Serikali kuu. Pia, mradi wa Kiwira unakadiriwa kuajiri wafanyakazi zaidi ya 1,000 utakapoanza kufanya kazi. Kwa hiyo, wananchi wa Mbeya na Watanzania wengine wataendelea kunufaika na kupata ajira.
Mheshimiwa Naibu Spika, kadhalika mradi huo utakuwa sasa na kipengele kinachowalazimisha wakandarasi na wamiliki wa migodi kuanza kuwashirikisha Watanzania kwa kununua bidhaa zao pamoja na huduma za jamii ili huduma za jamii zianzie maeneo yanayozunguka mgodi huo. Kwa hiyo, napenda niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge Mradi wa Kiwira utakuwa na manufaa makubwa sana kwa Taifa lakini pia kwa wananchi wanaozunguka mgodi huo.

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA (K.n.y. MHE. EZEKIEL M. MAIGE) aliuliza:- Kilio kikubwa cha wananchi waishio jirani na Mgodi wa Bulyankulu ni kunufaika na mgodi huo:- (a) Je, ni kiasi gani cha pesa Mgodi wa Bulyankulu ulitumia katika miradi ya ujirani mwema? (b) Je, kwa nini mgodi huo hautekelezi miradi yake kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Msalala ambako kuna wataalam na gharama za utekelezaji miradi ni ndogo?

Supplementary Question 4

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri swali dogo. Kwa sababu Mkalama kuna wachimbaji wadogo wadogo wa madini ya shaba, ni lini Wizara itawasaidia wachimbaji wadogowadogo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba eneo la Mkalama lina madini na siyo shaba tu, yapo madini ya shaba, madini ya ujenzi na madini mengine ya viwandani. Huduma ambazo zitatolewa na Serikali kwa wachimbaji wadogo ni kote nchini ikiwemo pia wachimbaji wadogowadogo wa Mkalama, ni kama ifuatavyo. Hatua ya kwanza kama tulivyosema kwenye bajeti yetu, Waheshimiwa Wabunge niwapongeze sana kwa sababu mmepitisha shilingi bilioni 6.68 kwa ajili ya ruzuku ya wachimbaji wadogo wadogo na ruzuku hiyo itatumika pia kwa wananchi wa Mkalama Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini manufaa mengine ambayo pia Serikali imejizatiti ni pamoja na kuyafanyia utafiti maeneo yote. Sasa hivi Wakala wa Jiolojia Tanzania anapita maeneo yote na kuyafanyia utafiti ili kubaini maeneo ambayo yanaweza kuchimbwa na wachimbaji wadogo kwa tija. Jambo lingine tunalofanya kama Serikali kusaidiwa wachimbaji wadogowadogo ni pamoja na kutoa elimu wezeshi na ushauri kwa ajili ya kuufanya uchimbaji mdogo uwe wa tija zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kubwa zaidi tumesogeza sasa huduma zote za ugani huko wachimbaji wadogo waliko. Tumefungua ofisi za madini karibu kila mkoa ili kuwawezesha wachimbaji wadogo kupata ushauri nasaha kwa masuala ya afya migodini pamoja na mazingira. Kwa hiyo, huduma za wafanyakazi, huduma za wachimbaji wadogo, zitaendelea kama kawaida na kama ambavyo nimeeleza.