Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 30 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 253 2016-05-27

Name

Ezekiel Magolyo Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA (K.n.y. MHE. EZEKIEL M. MAIGE) aliuliza:-
Kilio kikubwa cha wananchi waishio jirani na Mgodi wa Bulyankulu ni kunufaika na mgodi huo:-
(a) Je, ni kiasi gani cha pesa Mgodi wa Bulyankulu ulitumia katika miradi ya ujirani mwema?
(b) Je, kwa nini mgodi huo hautekelezi miradi yake kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Msalala ambako kuna wataalam na gharama za utekelezaji miradi ni ndogo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ezekiel Magolyo Maige, Mbunge wa Msalala, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka 2015 Mgodi wa Bulyankulu kwa kutumia “Maendeleo Fund” ulitumia takribani dola za Marekani milioni 1.98, sawa na takribani shilingi bilioni 4.4 kwa ajili ya miradi ya ujirani mwema iliyotolewa na Kampuni hiyo ya Bulyankulu.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, Kampuni za Migodi huwa na utaratibu wa kutekeleza shughuli zake kwa kuajiri wafanyakazi kulingana na mahitaji yao na kwa kuzingatia sheria za nchi. Pamoja na hayo, kampuni hizo huruhusiwa kuajiri wakandarasi wafanyakazi katika taaluma za ujuzi ambao haupo nchini. Hadi sasa kampuni imeajiri wafanyakazi hapa nchini wapatao 1,168, kati yao wafanyakazi 517 wanatoka katika maeneo yanayozunguka mgodi huo. Aidha, miradi husika hutekelezwa kwa kushindanisha wakandarasi na wataalamu kutoka sehemu mbalimbali nchini wakiwemo kutoka Halmashauri husika na hasa ya Msalala.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, tutachukua hali hii kama ombi rasmi la Mheshimiwa Mbunge wa Msalala ili kulitafakari na kulifanyia kazi na kukaa na wakandarasi pamoja na mgodi unaomiliki shughuli za Mgodi wa Bulyankulu.