Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Usambazaji wa umeme kupitia REA ulikusudiwa kufikishwa kwenye vijiji na senta 54 kwenye Awamu ya II na ingewezesha upatikanaji wa umeme asilimia 25-30, kwani upatikanaji wa umeme kabla ya mpango huo ulikuwa ni asilimia 5 na kwa kuzingatia mahitaji makubwa ya umeme kwa maendeleo ya wananchi wa Rorya umeme wa asilimia 25 bado ni wa chini na hata hivyo bado mradi unasuasua:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kasi ya usambazaji umeme katika Wilaya ya Rorya? (b) Je, ni lini Mpango wa REA II utakamilika na kuanza REA III? (c) Je, REA III ina vijiji na senta ngapi ndani ya Wilaya ya Rorya?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, pamoja na kazi nzuri aliyofanya katika Jimbo la Rorya, naomba tu nimuulize maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile ahadi ya Serikali kupitia REA III itakamilisha mradi kabambe wa kuweka umeme katika Jimbo la Rorya kuanzia tarehe 1 Julai, 2016. Je, Waziri anawahakikishiaje wananchi wa Rorya kwamba katika REA III, vijiji vyote vilivyobakia kupata umeme vitapata umeme huo?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa vile Mpango wa REA III uko mpaka Jimbo la Busega na kuna Kituo cha Afya cha Lukungu pale Lamadi hakina umeme na kimeshapatiwa tayari vifaa kutoka Shirika la AMREF. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri anaweza kunihakikishia kwamba kupitia REA III Kituo hiki cha Afya cha Lukungu na chenyewe kitapata umeme huo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Chegeni aliyeuliza kwa niaba ya Mheshimiwa Mbunge wa Rorya kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa REA II tunatarajia itakamilisha kazi zake mwisho wa Juni, 2016. Nichukue nafasi hii, siyo kwa Jimbo la Rorya tu lakini na kwa Wabunge wengine, nimhakikishie Mbunge wa Rorya kwamba vijiji vyote ambavyo vilikuwa katika REA Awamu ya II ambavyo havitakamilishwa, pamoja na kwamba tunataka vikamilishwe, vitaingizwa katika REA Awamu ya III. Ni mpago wa Serikali kwamba vijiji vyote hapa nchini ambavyo havijapata umeme katika REA Awamu ya II vitapatiwa umeme katika REA Awamu ya III inayoanza Julai, 2016. Nirekebishe kidogo swali la Mheshimiwa, amesema tarehe 1 Julai siyo kukamilisha, tarehe 1 Julai sasa ndiyo tunaanza REA Awamu ya III itakayoendelea kwa miaka mitatu, minne hadi mitano, ile Awamu ya II ndiyo itakamilika Juni, 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusiana na Jimbo la Busega kupatiwa umeme wa uhakika REA Awamu ya III, ni kweli viko vijiji vya Mheshimiwa Mbunge wa Busega, Mheshimiwa Dkt. Chegeni ambavyo vilikuwa viunganishwe umeme kwenye REA Awamu ya II lakini havijapata umeme ikiwa ni pamoja na Hospitali ya Lukungu katika Mji wa Lamadi. Tunatambua eneo la Lamadi ni eneo la kibiashara kwenye Jimbo la Mheshimiwa wa Busega, eneo hilo litapatiwa umeme pamoja na vituo vingine na Kituo cha Afya cha Lukungu kitapatiwa umeme kwenye REA Awamu ya III.

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Usambazaji wa umeme kupitia REA ulikusudiwa kufikishwa kwenye vijiji na senta 54 kwenye Awamu ya II na ingewezesha upatikanaji wa umeme asilimia 25-30, kwani upatikanaji wa umeme kabla ya mpango huo ulikuwa ni asilimia 5 na kwa kuzingatia mahitaji makubwa ya umeme kwa maendeleo ya wananchi wa Rorya umeme wa asilimia 25 bado ni wa chini na hata hivyo bado mradi unasuasua:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kasi ya usambazaji umeme katika Wilaya ya Rorya? (b) Je, ni lini Mpango wa REA II utakamilika na kuanza REA III? (c) Je, REA III ina vijiji na senta ngapi ndani ya Wilaya ya Rorya?

Supplementary Question 2

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba nimuulize Naibu Waziri swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa huu umeme wa REA wananchi wengi hawajapata elimu ya kusaidiana na Serikali katika kutoa maeneo ya kuweka huu umeme wa REA. Je, Serikali mna mpango gani kuhakikisha mnakwenda kijijini kutoa hii elimu ili wananchi watoe maeneo haya ya kupitisha umeme wa REA?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa REA wanavyofanya kazi, elimu inayotolewa inatolewa kwa kiwango kidogo. Nichukue nafasi hii kutamka rasmi kwamba kuanzia tarehe 1 Julai, wafanyakazi wote wa REA pamoja na TANESCO watakuwa sasa wanawafuata wateja badala ya wao kufuatwa, hilo la kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili tunawaelekeza sasa kutoa elimu sahihi kwa ajili ya taratibu za uunganishaji umeme pamoja na ada zinazotakiwa kulipwa. Kwa sasa wananchi wataelimishwa kwamba hawatakiwi kuweka mchango wowote kwenye maombi ya umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, la tatu, wananchi wataeleweshwa kuhusu gharama za service levy kwamba zimeondolewa, kwamba huduma ya kuhudumiwa umeme sasa imeondolewa. Kwa hiyo, jitihada za Serikali za kuhakikisha kwamba wananchi wanapata elimu zitaendelea. Zilikuwa zikifanyika lakini sasa tutaongeza nguvu zaidi kwa kuwafanya watumishi wa TANESCO na REA kufanya kazi kibiashara kwa kuwafuata wateja na kuwapa elimu badala ya wao kufuatwa.

Name

Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Usambazaji wa umeme kupitia REA ulikusudiwa kufikishwa kwenye vijiji na senta 54 kwenye Awamu ya II na ingewezesha upatikanaji wa umeme asilimia 25-30, kwani upatikanaji wa umeme kabla ya mpango huo ulikuwa ni asilimia 5 na kwa kuzingatia mahitaji makubwa ya umeme kwa maendeleo ya wananchi wa Rorya umeme wa asilimia 25 bado ni wa chini na hata hivyo bado mradi unasuasua:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kasi ya usambazaji umeme katika Wilaya ya Rorya? (b) Je, ni lini Mpango wa REA II utakamilika na kuanza REA III? (c) Je, REA III ina vijiji na senta ngapi ndani ya Wilaya ya Rorya?

Supplementary Question 3

MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa wakandarasi wa REA wanalalamika hawajalipwa pesa mpaka juzi na hili linaweza kuathiri uanzaji wa Awamu ya III kwa sababu shughuli ya Awamu ya II haijakamilika, Serikali inatoa kauli gani?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, labda nipate ufafanuzi vizuri, tunataka tuwatambue wakandarasi wote wanaolalamika kwamba hawajalipwa pesa ili tujue wanalalamikia nini, hilo la kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini inawezekana kukawa na malalamiko kwamba baadhi ya wakandarasi hawajalipwa pesa lakini kwa takwimu tulizonazo wakandarasi kwa mara ya mwisho, miezi miwili iliyopita tumewalipa pesa kwa ajili ya kuanza kazi. Inawezekana kuna baadhi ya wakandarasi nao wanaweka pia subcontractors, inawezekana wanaolalamika ni wale subcontractors. Napenda nimhakikishie kwamba suala hili tutalifanyia kazi. Nimelichukua, nitakaa na Mheshimiwa Mbunge tuone ni mkandarasi gani analalamika tuanze kulifanyia kazi mara moja.

Name

Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Usambazaji wa umeme kupitia REA ulikusudiwa kufikishwa kwenye vijiji na senta 54 kwenye Awamu ya II na ingewezesha upatikanaji wa umeme asilimia 25-30, kwani upatikanaji wa umeme kabla ya mpango huo ulikuwa ni asilimia 5 na kwa kuzingatia mahitaji makubwa ya umeme kwa maendeleo ya wananchi wa Rorya umeme wa asilimia 25 bado ni wa chini na hata hivyo bado mradi unasuasua:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kasi ya usambazaji umeme katika Wilaya ya Rorya? (b) Je, ni lini Mpango wa REA II utakamilika na kuanza REA III? (c) Je, REA III ina vijiji na senta ngapi ndani ya Wilaya ya Rorya?

Supplementary Question 4

MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Nishati ya umeme ni nishati muhimu sana hasa kwa maendeleo ya elimu. Hivi sasa sekondari zetu nyingi za kata, hasa kwa mikoa ya pembezoni kama Manyara na kwingineko hakuna umeme kabisa. Je, ni kwa nini usambazaji huu wa umeme vijijini unaofanywa na REA usilenge kwanza sekondari hizi za kata ambazo zina hali mbaya na ambazo zinahitaji kuboreshwa kielimu na kuboreshewa mazingira ya kusoma?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tumebaini kwamba taasisi nyingi za jamii kwenye kuunganishiwa umeme zimekuwa zikisahaulika. Hata hivyo, niseme kipaumbele cha REA Awamu ya II, kipaumbele cha REA Awamu ya III itakayaoanza vinalenga sanasana kwa kuanzia kuzipatia umeme taasisi za jamii zikiwemo shule, zahanati na taasisi nyingine, hilo ni la kwanza. Niombe sana Wabunge tushirikiane sasa na wataalam wetu wa REA na TANESCO huko vijijini kuwaelekeza wanapoanza kazi waanze na taasisi za jamii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niombe tu kuwaambia Waheshimiwa Wabunge, vipaumbele kwa kawaida kabla ya matumizi ya nyumbani tunaanza na taasisi za jamii. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tutatembea na wewe kama ambavyo huwa unatembea siku zote, tutembee kwa karibu ikiwezekana siku nzima Mheshimiwa Mbunge, tuongelee hospitali yako ambayo haijapata umeme tuipelekee umeme kwa haraka iwezekanavyo. Naomba uvumilie tukitoka hapa, Mheshimiwa Naibu Spika naomba unipe fursa ya kukaa na Mheshimiwa Mbunge, tukitafakari namna ya kupeleka umeme kwenye maeneo aliyozungumzia.