Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA aliuliza:- Matukio ya watu kupoteza maisha kutokana na ajali za moto yamezidi kuongezeka nchini:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukiwezesha Kikosi cha Zimamoto ili kufanya kazi ipasavyo kwenye Miji na nje ya Miji?

Supplementary Question 1

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi. Matukio ya ajali ya za moto, malori ya matenki ya mafuta yanaendelea kughalimu maisha ya Watanzania kwa kushabisha vifo na vilema vya kudumu. Tukio la Agosti 10, 2019 katika eneo la Msamvu eneo la Morogoro watu zaidi ya 100 walipoteza maisha, lakini umbali wa Ofisi za Zimamoto pale Morogoro haifiki kilometa moja kuelekea pale msamvu lilipotokea tukio.

Je, Serikali haioni kwamba kuna haja ya kuwalipa fidia wapendwa waliopoteza maisha yao pale, kwa sababu fire ilifika pale kuzima moto wakati watu wameshateketea na kuwa majivu na kuni? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Waziri Mkuu wakati wa mazishi yale pale Msamvu aliagiza kuunda Tume ya Kuchunguza Ajali ya Msamvu.

Je, ni kwa nini mpaka sasa Ofisi ya Waziri Mkuu haijatoa tamko lolote juu ya tume iliyouzwa kuchunguza ajali ya tukio la Msamvu? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza kabla sijajibu swali lake, naomba nisisitize majibu ya msingi ambayo niliyazungumza kuhusiana na mkakati wa Serikali ya kuimalisha Jeshi letu la Zimamoto na Uokoaji katika kulipatia vifaa mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, mbali na jitihada ambazo nimezungumza za kutenga bajeti ambapo kwa mwaka huu peke yake tumeshapokea karibu shilingi bilioni tatu kwa ajili ya ununuzi wa magari ya moto na vifaa vya uokoaji, lakini pia kuna mipango mbalimbali ikiwemo mkopo ambao nimezungumza, wa takribani Euro milioni 408 ambayo tunatarajia pamoja na mambo mengine kujenga vituo katika kila wilaya, kununua vifaa mbalimbali vya uokoaji ikiwemo magari, helkopta, boti na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, ni imani yangu kwamba tukapokuwa tumekamilisha mikakati hii na ikawa ipo vizuri, basi changamoto zote zinahusiana na majanga ya moto ikiwemo kama hili ambalo limetokea Morogoro, yatakuwa sasa tunayakabili kwa ufanisi zaidi.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na hoja yake specific kuhusu ripoti ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, Kamati ya Mheshimiwa Waziri Mkuu imepewa kazi. Kwa kuwa hii ilikuwa ni Kamati ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, nadhani siyo mamlaka yangu kuitolea kauli.

Mheshimiwa Spika, nina hakika kwamba Mheshimiwa Waziri Mkuu kupitia Ofisi yake, kuna utaratibu ambao umewekwa wa kuweza kuitolea taarifa pale ambapo mwenyewe ataona inafaa. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge avute subira ambapo Serikali inaendelea kulifanyia kazi suala hili. Ni imani yangu kwamba Kamati ile imeendelea kufanya kazi yake vizuri.

Mheshimiwa Spika, lengo na dhamira ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ni kuhakikisha kwamba taarifa ya ripoti ile inatupatia mapendekezo ambayo yanasababisha hatua zichukuliwe, lakini pamoja na kuepukana na matatizo kama haya yasitokeze siku zijazo.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA aliuliza:- Matukio ya watu kupoteza maisha kutokana na ajali za moto yamezidi kuongezeka nchini:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukiwezesha Kikosi cha Zimamoto ili kufanya kazi ipasavyo kwenye Miji na nje ya Miji?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona niweze kuulizwa swali dogo la nyongeza. Wilaya ya Ngara hatuna gari la Zimamoto na yameshatokea majanga mara nyingi na ya kusababisha vifo; na ni barabara inayopitisha magari makubwa yanayobeba mafuta yakielekea nchi za jirani Rwanda, Burundi na Kongo:-

Je, ni lini Serikali itatuletea gari la Zimamoto Wilaya na Ngara? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza niendelee kumpongeza Mheshimiwa Oliver kwa jinsi ambavyo amekuwa akipambana kuhakisiha kwamba changamoto mbalimbali zinazohusu vyombo vya usalama katika Mkoa wa Kagera zinapatiwa ufumbuzi.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na hoja yake ya kupeleka gari la zimamoto katika Wilaya ya Ngara, nimhakikishie kwamba pale ambapo mikakati ambayo nimeizungumza kwenye jibu la msingi itakapokuwa imekaa tayari, basi moja katika maeneo ambayo tunayazingatia ni Wilaya ya Ngara.

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA aliuliza:- Matukio ya watu kupoteza maisha kutokana na ajali za moto yamezidi kuongezeka nchini:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukiwezesha Kikosi cha Zimamoto ili kufanya kazi ipasavyo kwenye Miji na nje ya Miji?

Supplementary Question 3

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ajali za moto zimekuwa ni kubwa sana katika taifa; katika taasisi za Serikali na hata katika mabweni ya shule. Sasa nauliza, najua ni lazima kuwepo na fire extinguishers katika maeneo yote.

Mheshimiwa Spika, ni kwa nini sasa sheria isije Bungeni ikarekebishwa, au kanuni ikarekebishwa kusudi iwe ni lazima kuwa na smoke detectors katika mabweni ya shule na katika taasisi za Serikali ili ule moshi uweze kung’amuliwa mapema na kuzia madhara makubwa yanayosababishwa na moto?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ruth Molel, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa hoja ya Mheshimiwa Mbunge ni ushauri basi tunaipokea na tuitafakari na kuona ni jinsi gani tunaweza tukaifanyiakazi.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA aliuliza:- Matukio ya watu kupoteza maisha kutokana na ajali za moto yamezidi kuongezeka nchini:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukiwezesha Kikosi cha Zimamoto ili kufanya kazi ipasavyo kwenye Miji na nje ya Miji?

Supplementary Question 4

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Spika, nashukuru.

Kwa kuwa majanga yanayosababishwa na binadamu ni zaidi ya asilimia 96 ya majanga yote. Serikali haioni umuhimu wa kuhakikisha kunakuwa na somo rasmi kwenye mfumo rasmi wa elimu wa namna ya kujilinda, kujinga na kujiokoa na majanga hapa nchini?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mabtia, Mbunge wa Vunjo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nao vilevile ni ushauri; nadhani mamlaka husika zimeusikia, lakini kama Serikali tumeuchukua na tutafakari kuona kama kuna haja ya kufanya hivyo kwa wakati huu.