Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Soko la Mji wa Mpwapwa, ni dogo, limechakaa na halifanani kabisa na hadhi ya Mji wa Mpwapwa ambao idadi ya watu ni zaidi ya laki moja? Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia ujenzi wa soko jipya na la kisasa katika mji huo?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa Serikali ilichukua vyanzo vingi vya mapato katika Halmashauri zetu, kwa hiyo Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa haina mapato ya kutosha ya kuweza kujenga soko; je, kwa nini Serikali isitoe fedha kwa ajili ya kujenga soko la Mpwapwa kama vile inavyotoa fedha kujenga majengo mengine kama vile Vituo vya Afya na majengo mengine?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa mimi niliwahi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa na kwa kuwa jukumu la Mikopo ya Serikali za Mitaa ni kukopesha Halmashauri ili ziweze kujenga masoko, kujenga Vituo vya Mabasi; je, huo mpango umeishia wapi? Ahsante.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa George Malima Lubeleje, kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni kweli kwamba kuna vyanzo vingine vilichukuliwa na Serikali Kuu kutoka Serikali za Mitaa kwa maana ya Halmashauri, lakini hizi fedha ambazo zilichukuliwa kuletwa Serikali Kuu, kwa maana Mfuko Mkuu wa Serikali ni fedha ambazo zinatumika kujenga miradi mikubwa ya Kitaifa ambayo inanufaisha maeneo yote ya nchi. Zingeachwa kama ilivyokuwa maana yake kuna Halmashauri zingine zingepata miradi zingine zingekosa miradi, kitendo cha kupelekwa Hazina maana yake fedha hizi zinasimamiwa na Serikali na inapeleka miradi mikubwa ambayo kila Mtanzania mahali popote alipo wananufaika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niliweke sawa jambo hilo, lakini jibu langu la swali la pili ni kwamba, ni kweli kwa sasa kuna miradi ambayo Halmashauri Kuu inapewa fedha kutoka pengine kwa Wafadhili wa nje, kadri muda ulivyokuwa unaenda miradi hii ilikuwa unapanga mipango ambayo huna uhakika nayo. Sasa Serikali imeleta Mpango Mkakati ambayo ina uhakika hata mikopo kutoka Mfuko wa Serikali za Mitaa ilikuwa ni fedha ambayo ina riba na wakati mwingine haina uhakika sana na kuna Halmashauri zingine zimekopa fedha zinadaiwa mpaka leo hawajawahi kurejesha.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa hiyo Serikalia imetengeneza Mkakati pamoja na Wizara ya Fedha, fedha zipo Halmashauri inaandika andiko na Mheshimiwa Mbunge ni Mjumbe katika Halmashauri yake vikao vya Kamati ya Fedha wanaainisha mradi ambao wanadhani wao utakuwa ni mkakati wao kupata fedha nyingi, wanaleta Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa unaenda Hazina unapitiwa na Wataalam, wakipata fedha hizo wataanzisha mradi mkubwa kama hilo soko Mbunge alivyosema hiyo, hiyo fedha ikipatikana watafanya miradi ambayo wana uhakika nayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, yako maeneo juzi nilikuwa Manispaa ya Moshi, wana Mradi wa zaidi ya shilingi bilioni ishirini na nane, Jiji la Dar es Salaam wana bilioni hamsini na nane, maeneo mengine bilioni kumi na sita, kumi na saba, kumi na nane, kwa hiyo fedha zipo Mheshimiwa Mbunge na Halmashauri husika waandae Andiko la Kimkakati, tufanye tathmini wapate fedha wajenge mradi ambao utapata fedha za uhakika ili waweze kufanya miradi ya maendeleo katika eneo lao. Ahsante.

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Soko la Mji wa Mpwapwa, ni dogo, limechakaa na halifanani kabisa na hadhi ya Mji wa Mpwapwa ambao idadi ya watu ni zaidi ya laki moja? Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia ujenzi wa soko jipya na la kisasa katika mji huo?

Supplementary Question 2

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Mji wa Karatu ni Mji wa Kitalii na ni mji ambao unakua kwa kasi sana, lakini bahati mbaya mji huo hadi wa sasa hauna soko la uhakika, Halmashauri kwa kutumia mapato yake ya ndani imeanza ujenzi wa soko la kisasa, je, Serikali lini itaunga mkono jitihada hizo za Halmashauri ya Karatu?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nijibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Qambalo Mbunge wa Karatu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi ni kwamba Halmashauri zote hizi Wakurugenzi wameelekezwa, wameitwa Dodoma Wakurugenzi wote nchi nzima, Waweka Hazina, Maafisa Mipango wakapewa utaratibu, Serikali inachofanya kama soko lenu mnadhani kwamba linakidhi viwango walete kama nilivyosema andiko ili fedha zitolewe waweze kufanya kazi, wanakopeshwa fedha, wanawekeza, wanasimamia wenyewe, wanaanza kurejesha kidogo kidogo. Hiyo ni fedha ambayo ina uhakika tofauti na kuahidiwa bilioni kumi halafu haiji au unapata bilioni moja. Fedha za Miradi ya Kimkakati zipo, walete andiko tupitie, wapate fedha wasimamie na Mheshimiwa Mbunge awepo ili wapate fedha ya uhakika na soko lisimame wapeleke huduma na kupata mapato mema ya kujenga Halmashauri yao.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Soko la Mji wa Mpwapwa, ni dogo, limechakaa na halifanani kabisa na hadhi ya Mji wa Mpwapwa ambao idadi ya watu ni zaidi ya laki moja? Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia ujenzi wa soko jipya na la kisasa katika mji huo?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Kama ulivyo Mji wa Mpwapwa kuna Mji wa biashara unaitwa Endasak Wilaya ya Hanang ni mahali ambapo wanahitaji soko kama hilo wanalolihitaji Mpwapwa, naomba kujua kwa Mheshimiwa Waziri ni nini kitakachofanyika kushirikiana na Halmashauri yetu pale tujenge soko kwa sababu imezungukwa na vitunguu saumu, vitunguu maji, makabichi na nini na hakuna soko, Ahsante. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu, Mbunge wa Hanang kama ifuatavyo:-

Naomba majibu haya pia yaende kwa Waheshimiwa Wabunge wote ambao wana maswali yanafanana na hayo; maelekezo ni kwamba Wakurugenzi na Wataalam wetu katika Halmashauri wameelekezwa, hii ni fursa tunaomba waitumie. kila Halmashauri inaangalia fursa ya kibiashara iliyopo, kuna wengine wameandika Miradi ya Kimkakati kujenga masoko, wengine wamependekeza kujenga stendi na miradi mbalimbali kama hiyo na wale ambao wamefanikiwa tunavyozungumza fedha wamepewa wanaendelea na ujenzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa wengine wote Halmashauri zote walete maandiko katika Ofisi ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa pamoja na Hazina tutapitia, fursa iliyopo waitumie, fedha hizi zipo pale, isipokuwa wale ambao walileta mkakati wakapewa fedha na fedha zile hawakuzitumia, maelekezo yametoka vinginevyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, waandike haraka andiko lao, washirikishe Wataalam wao, Waheshimiwa Wabunge washiriki, fedha zipo waanzishe miradi ya kimkakati tupate fedha za uhakika ili kukamilisha miradi ya maendeleo ya wananchi na kuondoa kero katika maeneo yetu. Ahsante.