Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 16 2019-11-06

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:-

Soko la Mji wa Mpwapwa, ni dogo, limechakaa na halifanani kabisa na hadhi ya Mji wa Mpwapwa ambao idadi ya watu ni zaidi ya laki moja?

Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia ujenzi wa soko jipya na la kisasa katika mji huo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa George Malima Lubeleje, Mbunge wa Mpwapwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa inafahamu changamoto ya udogo wa soko la Mji Mpwapwa na imekwishaandaa mikakati ya kujenga soko hilo la kisasa linaloendana na hadhi ya idadi ya watu katika eneo hilo. Halmashauri imetenga eneo katika Kiwanja Na. 61 Kitalu B Mazae chenye ukubwa wa mita za mraba 15,000 kilichopo katika Kata ya Mazae.

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri inaendelea kuandaa Andiko la Mradi pamoja na kufanya usanifu ili iweze kuwasilisha andiko hilo Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na hatimaye Wizara ya Fedha na Mipango kupitia utaratibu wa Miradi Mikakati, vilevile Halmashauri inaendelea na mazungumzo na uongozi wa Mradi wa Local Investmest Climate ili kupata fedha za ujenzi wa soko. Ahsante.