Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. JULIUS K. LAIZER aliuliza:- Mji wa Mto wa Mbu ni mji wa kitalii na unaingiza mapato mengi ya kitalii; lakini unakabiliwa na tatizo la miundombinu ya barabara; (a) Je nini mkakati wa Serikali kuupatia Mji wa Mto wa Mbu angalau km 5 za lami? (b) Je Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa barabara ya Mto wa Mbu mpaka Loliondo kwa kiwango cha lami ili kusaidia mradi wa kimkakati wa magadi Engaruka? (c) Je ni lini Serikali itatimiza ahadi ya Mhe. Rais ya kuweka lami barabara ya Ngarasha mpaka Monduli Juu kwa Sokoine?

Supplementary Question 1

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili madogo ya nyongeza; na unipe ruhusa niwape pole wananchi wa Monduli, hasa wa Mto wa Mbu ambao wamekubwa na mafuriko kwa muda wa wiki moja sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, Serikali imesema imetenga shilingi bilioni saba kwa ajili ya ujenzi wa kilometa tisa; lakini bilioni saba hizo inawezekana zisipatikane kwa wakati. Nataka kujua commitment ya Serikali ya kuhakikisha kwamba walao barabara hii inawekwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2020/2021?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Barabara hii ya Monduli Juu ambayo Waziri anasema ipo katika hali ya upembuzi yakinifu, upembuzi yakinifu umekamilika na document zote zipo tayari. Je, ni lini hasa Serikali itaanza ujenzi wa barabara hiyo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Julius Kalanga yenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji Mdogo wa Mto wa Mbu unaufahamu vizuri. Na Mheshimiwa Mbunge amekuwa akipigania kwa sababu adha ambayo imekuwa ikipatikana kila wakati mvua zinaponyesha mafuriko yanakuwepo eneo lile. Kwanza kipekee naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa sababu amekuwa akilipigania eneo hili kwa muda mrefu. Naomba nimhakikishie, katika bajeti ya mwaka 2020/2021 tutaanza na mifereji na ujenzi wa kilometa moja utaanza ili tupunguze adha kwa wananchi wa Mto wa Mbu.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile ameongelea barabara ya kwenda kwa Marehemu Sokoine. Kama anavyokiri hata yeye mwenyewe, kwamba usanifu ulishakamilika. Naomba nimhakikishie, kufanyika kwa usanifu tafsiri yake ni kwamba, kama ambavyo nimejibu katika jibu langu la msingi kwamba fedha ikipatikana nako ujenzi utaanza. Aendelee kuiamini Serikali kama ambavyo tukiahidi daima tumekuwa tukitekeleza.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. JULIUS K. LAIZER aliuliza:- Mji wa Mto wa Mbu ni mji wa kitalii na unaingiza mapato mengi ya kitalii; lakini unakabiliwa na tatizo la miundombinu ya barabara; (a) Je nini mkakati wa Serikali kuupatia Mji wa Mto wa Mbu angalau km 5 za lami? (b) Je Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa barabara ya Mto wa Mbu mpaka Loliondo kwa kiwango cha lami ili kusaidia mradi wa kimkakati wa magadi Engaruka? (c) Je ni lini Serikali itatimiza ahadi ya Mhe. Rais ya kuweka lami barabara ya Ngarasha mpaka Monduli Juu kwa Sokoine?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza; lakini uniruhusu niseme jambo moja dogo ambalo siku zote nimekuwa nikitafakari wahenga wakisema kua uyaone, lakini hatimaye nimeyaona jana goli kuwa kona kwa watani zangu wa Yanga; kwa kweli, nimestaajabu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba swali langu dogo la nyongeza lipate majibu yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, Serikali imedhamiria kuhakikisha barabara zote ambazo ziko kwenye ahadi zinajengwa na kukamilika kwa kiwango cha lami ikiwemo Barabara ya kutoka Buhongwa – Lwanima – Kishiri mpaka Igoma. Sasa, ni lini Serikali itakuwa tayari kuhakikisha barabara hii inakamilika kwa kiwango cha lami kama ambavyo iliahidi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mabula, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ambayo Mheshimiwa Mbunge anaitaja ni barabara ambayo iko chini ya TARURA. Na kipekee Mheshimiwa Mbunge amekuwa akiipigania barabara hii kwa muda mrefu. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge; usanifu wa barabara hii umeshakamilika; na kitakachofuata katika bajeti ya mwaka 2020/2021 tutaanza kuijenga hatua kwa hatua, ili barabara yote iweze kukamilika.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIUS K. LAIZER aliuliza:- Mji wa Mto wa Mbu ni mji wa kitalii na unaingiza mapato mengi ya kitalii; lakini unakabiliwa na tatizo la miundombinu ya barabara; (a) Je nini mkakati wa Serikali kuupatia Mji wa Mto wa Mbu angalau km 5 za lami? (b) Je Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa barabara ya Mto wa Mbu mpaka Loliondo kwa kiwango cha lami ili kusaidia mradi wa kimkakati wa magadi Engaruka? (c) Je ni lini Serikali itatimiza ahadi ya Mhe. Rais ya kuweka lami barabara ya Ngarasha mpaka Monduli Juu kwa Sokoine?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji Mdogo huu wa Mto wa Mbu ni sawasawa na Mji Mdogo wa Karatu; kwa maana ni miji ambayo watalii wanapita kuingia katika Hifadhi ya Manyara na Hifadhi ya Ngorongoro.

Je, Serikali sasa haioni kuna umuhimu wa kuwa na mpango mkakati wa kuendeleza miji hii kwa sababu ni kitovu cha kuingia katika Hifadhi zetu za Taifa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Paresso kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo Mbunge ameongelea Mji Mdogo wa Mto wa Mbu na Mji wa Karatu; ni kweli ni miji ambayo ni ya pekee kwa sababu ni lango katika watalii wanapoenda kutembelea mbuga zetu. Kama ambavyo Serikali imekuwa na mpango kupitia TSSP tumekuwa tukiendeleza miji kwa kujenga barabara za kiwango ambacho ni kiwango kizuri. Naomba Mheshimiwa Mbunge aendelee kuridhika na Serikali yetu hatua kwa hatua tunamaliza hiyo miji ambayo tulianzanayo nina hakika, katika mji ambao ameutaja kwa sababu ni jicho la kipekee kwa watalii nao hakika hatutauacha.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. JULIUS K. LAIZER aliuliza:- Mji wa Mto wa Mbu ni mji wa kitalii na unaingiza mapato mengi ya kitalii; lakini unakabiliwa na tatizo la miundombinu ya barabara; (a) Je nini mkakati wa Serikali kuupatia Mji wa Mto wa Mbu angalau km 5 za lami? (b) Je Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa barabara ya Mto wa Mbu mpaka Loliondo kwa kiwango cha lami ili kusaidia mradi wa kimkakati wa magadi Engaruka? (c) Je ni lini Serikali itatimiza ahadi ya Mhe. Rais ya kuweka lami barabara ya Ngarasha mpaka Monduli Juu kwa Sokoine?

Supplementary Question 4

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kumuuliza Naibu Waziri, kwa nini Nyanghwale haitengewi pesa za maendeleo ya barabara ilhali kuna barabara ambazo zimeharibika vibaya yakiwemo madaraja kutoka Nyanghwale pale makao makuu kwenda Lushimba. Ni kwa nini Serikali haitutengei fedha za maendeleo ya barabara?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Amar, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali hii ya CCM ambayo na yeye Mheshimiwa Mbunge anatokana na CCM anajua kabisa kumekuwa hakuna upendeleo katika kupeleka maendeleo katika nchi yote kwa ujumla. Kwa kuwa yeye ni sehemu ya Madiwani ni vizuri basi wakahakikisha kwanza wanaanza kutenga wao na sisi Serikali Kuu tukapata taarifa. Kimsingi hakuna hata eneo moja ambalo hatutengi fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara.