Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:- Nchi yetu imebarikiwa kuwa na Hifadhi nyingi zenye wanyama wengi wa kuvutia lakini mapato yatokanayo na utalii ni kidogo: Je, Serikali ina mikakati gani ya kuongeza mapato ya utalii?

Supplementary Question 1

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba niipongeze Serikali kwa dhati kabisa kwa juhudi zake za dhati za kuboresha utalii katika nchi yetu. Kama Mbunge, nimesikitishwa na kauli za baadhi ya Wabunge wa Upinzani kubeza juhudi za Serikali za kuboresha utalii na kuchochea kwa kutumia wasanii wa ndani. Niwaambie tu wasanii, Serikali ya Awamu ya Tano inatambua mchango wao mkubwa katika kuijenga nchi yetu. Kwa hiyo iwapuuze hao, hii ni tabia yao na ndivyo walivyo.

Mheshimiwa Spika, swali langu namba moja, maeneo au halmashauri nyingi ambazo zimezungukwa na National Park hawanufaiki na shughuli za utalii kwa kuwa hoteli zile zimejengwa ndani ya zile mbuga. Sasa je, Seriakli haioni sasa umefika wakati wa kuweka utaratibu wa kujenga hoteli zile za kitalii nje ya zile hifadhi ili wananchi wa maeneo yale waweze kunufaika kama kodi na vitu vinginevyo.

Mheshimiwa Spika, swali namba mbili, tunafahamu nyamapori ni tamu sana. Mtalii anapoona akatamani na akala, itavutia watalii wengi sana kuja hasa wa ndani. Je, Serikali haioni sasa umefika wakati iweke utaratibu wa kuweka vigenge vya nyama choma ndani ya mbuga zile ili mtalii anapoona nyama ile anaitamani halafu anaila sio aone, atamani, aondoke. Ahsante.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, MALIAISILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwanza kipekee kabisa naomba nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Mlinga, watu wengi wanapomuona hapa Bungeni huwa wanafikiri ni mtu wa vituko lakini nikuhakikishie Mheshimiwa Mlinga ni mfuatiliaji mkubwa sana wa masuala ya uhifadhi lakini na masuala ya kiuchumi yanayohusu wananchi wake na halmashauri yake. kwa hiyo nampongeza sana Mheshimiwa Mlinga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba hivi karibuni tumefanya mabadiliko ya Kanuni na tunaandaa Kanuni ili kuruhusu matumizi ya nyama ya wanyamapori kwa watu wengi na katika kufanya hivyo tunapitia upya kanuni ili tuweze kuruhusu uwindaji wa ndani lakini pia kufunguliwa kwa mabucha ambayo yatakuwepo katika maeneo mbalimbali na kuyasajili. Kwa hiyo, taratibu hizo zitasaidia pia kuhakikisha kwamba nyama hii ya wanyamapori inapatikana katika maeneo yote yaliyoko katika hifadhi na maeneo ya mapori ya akiba ambapo wafanyabiashara watataka kupeleka nyama hiyo.

Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili Mheshimiwa Mlinga anataka kujua maoni ya Serikali ni kwanini hoteli zisijengwe nje ya hifadhi. Nakubaliana na Mheshimiwa Mlinga kwamba hivi sasa kwa mfano katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, nafasi ya kujenga hoteli ndani zimejaa na uzoefu tulionao ni kwamba kadri hoteli nyingi zinavyozidi kujengwa ndani ndivyo uharibifu wa mazingira unazidi kuondoa uhalisia wa hifadhi yenyewe ya Serengeti.

Mheshimiwa Spika, tumekubaliana kwa sasa kwamba wawekezaji wote wapya tutawapeleka nje ya Hifadhi ya Serengeti na hifadhi zingine za Taifa ili kuvutia pia wananchi wanaozunguka maeneo hayo kuweza kujishughulisha na biashara ndogondogo moja kwa moja na hoteli hizo. Kwa hiyo, tunauchukua huo kama ushauri ingawa hauwezi kutumika hivyo katika hifadhi zote kwa sababu zipo hifadhi ambazo bado zina nafasi ambazo zimetengwa kwa ajili ya uwekezaji. (Makofi)

Name

Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:- Nchi yetu imebarikiwa kuwa na Hifadhi nyingi zenye wanyama wengi wa kuvutia lakini mapato yatokanayo na utalii ni kidogo: Je, Serikali ina mikakati gani ya kuongeza mapato ya utalii?

Supplementary Question 2

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, nina swali moja dogo. Kwa mujibu wa United Nation World Tourism Organization mwaka 2018 dunia nzima imekuwa na watalii bilioni 1.4 ni kwanini Tanzania imeendelea kusuasua imeshindwa ku- capitalize kuwavutia watalii hawa kuja nchini ikizingatiwa kuwa watalii kutoka Israel na kutoka Ulaya hususan Ujerumani wamekuwa ni wale wale wanaokuja kutoka enzi za utawala uliopita?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwanza Mchungaji Msigwa ni Mjumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa hiyo ninaamini kwamba kama ana mchango wowote utakaosababisha watalii waje nchini anaweza kuutoa kwenye Kamati. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini la pili kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi tumetoka kwenye watalii 1,100,000 mpaka 1,500,000 watalii ni tofauti kabisa na mzigo wa mahindi kwamba unaweza ukaamka asubuhi ukawa na tani 10 kesho ukaleta tani 100. Wanahitaji maandalizi makubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ikitokea leo Tanzania ikapata watalii 3,000,000 kwanza nafikiri takwimu wanazo, Tanzania kwa ujumla wake na hoteli zake zote hatujazidi vitanda 30,000. Sasa ikatokea leo tukapata watalii 2,000,000 kwa mpigo, Tanzania nzima itajaa watalii na inawezekana hata sehemu ya kuwapeleka hakuna. Lakini tunahitaji miundombinu. Katika nchi nyingi ambazo unaona zinapata watalii wengi, hakuna seasonal za utalii. Watalii wanafanya utalii mwaka mzima. Sisi katika kipindi kifupi cha mwaka tuna high season ambacho ndicho tunachopokea watalii 1,500,000 tunachofanya sasa hivi ni kuimarisha miundombinu, tunafungua barabara zipitike mwaka mzima, tunaimarisha usafiri tuwe na shirika ambalo linaweza likasafirisha watalii ndani na tunaendelea kuyafikia masoko na kuhamasiaha uwekezaji ili tuweze ku-accommodate idadi kubwa ya watalii ambao wanakuja nchini.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Msigwa kwamba idadi ya watalii wanaokuja sasa anaweza akawa ni yule yule kutokana na experience aliyoipata Tanzania nafikiri unafahamu kauli yetu ya Tanzania unforgettable kwa hiyo mtu anaweza kutamani kurudi mara kumi lakini tunaendelea kuyafikia masoko mengine nje na hivi sasa tunaendelea kufika Urusi, China, India masoko ambayo hatukuweza kuyazoea awali. Kwa hiyo naamini kwa muda mfupi ujao tutafikia watalii ambao anawataka Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naamini kwa muda mfupi ujao tutafikia watalii wengi ambao anawataka Mheshimiwa Mbunge.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:- Nchi yetu imebarikiwa kuwa na Hifadhi nyingi zenye wanyama wengi wa kuvutia lakini mapato yatokanayo na utalii ni kidogo: Je, Serikali ina mikakati gani ya kuongeza mapato ya utalii?

Supplementary Question 3

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Tunatambua na tunajua kuwa maliasili ni kitu muhimu sana katika ustawi wa Taifa letu la Tanzania na huchangia pato la asilimia 17 kutokana na utalii huo. Mkoa wetu wa Lindi ni miongoni mwa sehemu ambazo zinapitiwa na Selous ambayo sasa hivi ni Mwalimu Nyerere National Park.

Mheshimiwa Spika, sasa katika Mkoa huu wa Lindi, kuna tatizo ambalo lipo katika Tarafa ya Melola, Kata ya Milola na Tarafa ya Mkinga, Kata ya Mchinga ambalo hili ni Jimbo la Mchinga. Wanyama kama tembo wanaingia katika maeneo hayo hata Mbunge wa Jimbo hilo Mheshimiwa Bobali ana ushahidi juu ya jambo hili. Pia wanyama hawa wanapoingia wanaleta uharibifu wa mazao na vilevile wanasababisha baadhi ya watu kupoteza maisha yao.

Mheshimiwa Spika, Serikali inatuambia nini au inawaambia nini wananchi hawa juu ya uharibufu huo ambao umetokea katika maeneo hayo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba majibu ya Serikali. (Makofi)

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwa kweli naomba nikiri kwamba kutokana na mafanikio makubwa ya uhifadhi ambayo yametokea katika kipindi hiki cha Awamu ya Tano, migogoro mingi ya wanyama na binadamu imeripotiwa katika almost nchi nzima. Nakubaliana na Mheshimiwa Mama Salma kwamba katika maeneo ya Melola imeripotiwa sana kwamba tembo wanavamia makazi ya watu na kula mazao; lakini siyo huko tu, ni maeneo mengi, almost nchi nzima.

Mheshimiwa Spika, tumeafanya nini kama Wizara? Moja, tumeelekeza taasisi zetu zote ikiwemo TAWA, TANAPA, TFS na Ngorongoro kuimarisha vitengo vinavyo-respond na matukio haya. Wote tumewaambia wawe na kikosi ambacho kipo tayari. Hata hivyo, imetokea mara nyingi kwamba wakati wanyama wanakuwepo kijiji kingine, wakati mwingine tumeshindwa kuwahi. Naomba nitumie fursa hii kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge kwamba tumetoa maelekezo na suala hili tunalifanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu fidia ya mazao, Wizara imerekebisha kanuni ili kuweza kutoa kifuta jasho na kifuta machozi kinachoridhisha. Kanuni hizo zimekamilika, tutahakikisha kwamba malipo haya yanawahi kwa waathirika ili kuweza angalau kuwafuta machozi na jasho kwa muda mu Nakushukuru sana. (Makofi)