Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Alfredina Apolinary Kahigi

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI aliuliza:- Wapo akina mama wanaojifungua wakiwa gerezani na kuendelea kutumikia adhabu zao huku wakiwa na watoto wachanga:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapumzisha kama miezi sita bila kufanya kazi ili wapate nguvu kwanza?

Supplementary Question 1

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kunipa nafasi kwa mara nyingine tena. Namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri kama yanatekelezwa lakini nina maswali yangu mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ikibainika mwanamke aliyefungwa gerezani akachukua mimba, je, ni hatua gani za kisheria atakazochukuliwa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; iwapo mwanamke huyo aliyefungwa amehukumiwa kufungwa miaka 10 na zaidi, je, yule mtoto ambaye amejifungulia humo gerezani atakaa nae mpaka kifungo chake kiishe? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ameuliza ikibainika atachukua mimba lakini moja kwa moja nilivyomuelewa ni kwamba anakusudia atachukulia mimba nje ya gereza kwa sababu hakuna uwezekano wa kuchukua mimba akiwa gerezani. Na kama akiwa amechukua mimba akiwa nje ya gereza utaratibu ndio kama ambavyo nimeuzungumza katika jibu langu la msingi kwamba atajifungua, atakapokuwa amejifungua atapewa utaratibu maalum kwa mujibu wa sheria ambayo nimeinukuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala ni kwamba je, akishakujifungua ambalo ni swali lake la pili. Akishajifungua na amefungwa muda mrefu, nini hatma ya yule mtoto? Jibu ni kwamba mtoto yule atakapofikia umri wa kumaliza kunyonya, maafisa Ustawi wa Jamii wanakwenda katika magereza kwa ajili ya kuzungumza na yule mama ili mtoto yule aweze kupata fursa ya kupata malezi nje ya gereza aidha kwa jamaa zake ama kwa watu au taasisi zozote ambazo zimekuwa zikihudumia watoto ikiwa hana jamaa. Huo ndio utaratibu wa kawaida ambao tupo nao kwa sasa hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kipindi ambacho wapo magerezani watoto wale wanahudumiwa vizuri kwa kadri ambavyo sheria inazungumza ikiwemo hata kuweza kuwapatia huduma ya elimu za awali katika shule zilizopo karibu na magereza.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI aliuliza:- Wapo akina mama wanaojifungua wakiwa gerezani na kuendelea kutumikia adhabu zao huku wakiwa na watoto wachanga:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapumzisha kama miezi sita bila kufanya kazi ili wapate nguvu kwanza?

Supplementary Question 2

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa hali ya maumbile ya mwanadamu, hasa mwanamke yanapelekea kujifungua au kupata watoto: Je, Serikali inachukua hatua gani kudhibiti utungwaji mimba ndani ya Magereza ili kupunguza shida ambazo watoto hao watapata katika kulelewa katika mazingira ambayo siyo rafiki kama Magereza; kwa kuwa bado inasemekana kwamba kuna mchanganyiko wa wanawake na wanaume na wanapata access ya kukutana? Sasa Mheshimiwa Waziri atuambie atadhibiti vipi utungwaji mimba?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilieleza wakati najibu swali la msingi kuhusiana na uwezekano wa mwanamke kupata mimba ndani ya Magereza. Nimezungumza hivyo kwa sababu zifuatazo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba Magereza yametenganishwa, hakuna mchanganyiko kati ya Magereza upande wa wanawake na wanaume; hata Askari ambao wanahudumia wafungwa na mahabusu wa kike basi wanakuwa ni Askari wa kike. Kwa hiyo, mara nyingi tunapozungumzia upataji mimba wa Magereza inakuwa ni kwa wafungwa ama mahabusu ambao wameingia tayari Magerezani ikiwa mimba zimeshaanza kutungwa.