Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 3 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 34 2020-01-30

Name

Alfredina Apolinary Kahigi

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI aliuliza:-

Wapo akina mama wanaojifungua wakiwa gerezani na kuendelea kutumikia adhabu zao huku wakiwa na watoto wachanga:-

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapumzisha kama miezi sita bila kufanya kazi ili wapate nguvu kwanza?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Alfredina Apolinary Kahigi, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba wapo wafungwa wanawake wanaoingia na ujauzito gerezani na kujifungua wakiwa bado wanatumikia adhabu zao. Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na Jeshi la Magereza inatambua umuhimu wa kumpatia huduma stahiki pamoja na kutofanya kazi ngumu kwa mama mjamzito na aliyejifungua akiwa gerezani, ili aweze kumnyonyesha na kumhudumia mwanae inavyostahili mfano, kupelekwa kliniki, kupewa maziwa kwa ajili ya mwanae, chakula cha ziada na kutengwa na wenzie kwa kipindi kisichopungua miezi mitatu ili aweze kujihudumia vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huduma za wafungwa hawa zimeainishwa vizuri katika Kanuni za Kudumu za Uendeshaji wa Jeshi la Magereza kifungu Na. 728 - 729 Toleo Na. 4 la mwaka 2003.