Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Primary Question

MHE. HUSSEIN M. BASHE aliuliza:- Wakati wa kampeni za uchaguzi Mheshimiwa Rais aliahidi ujenzi wa daraja la Nhobola na daraja la Butandula pamoja na barabara inayounganisha Kijiji hicho na Kijiji cha Mbogwe:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa ahadi ya ujenzi wa madaraja hayo pamoja na barabara zake?

Supplementary Question 1

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika nashukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa msingi wa ahadi ya Mheshimiwa Rais ilikuwa ni kutazama uwezo wa Halmashauri, kwamba haina uwezo wa kujenga madaraja haya pamoja na barabara zake, thamani ya madaraja haya mawili ni zaidi ya milioni 800.
Je, Waziri yupo tayari kuthibitishia Bunge lako na wananchi wa Jimbo la Nzega kwamba miradi hii itapalekwa TANROAD kama ambavyo Rais aliahidi?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikubaliane na yeye kwamba kwa kulinganisha na bajeti zetu za Halmashauri, fedha hii tu peke yake inaweza ikawa ndiyo bajeti ya Halmashauri hiyo kwa mwaka mzima kwa barabara zote. Kwa hivyo ni kweli kama anavyosema Mbunge na ndiyo maana pengine Mheshimiwa Rais alisema madaraja haya yapelekwe TANROADS.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu Serikali ni moja, na ahadi iliyotolewa fedha zinatoka zote Hazina, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa dhana ya D by D hata kama Halmashauri haina uwezo ama wa kitaalamu au wa kifedha, kazi ya Wizara yangu ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ni coordination ambapo Wizara nyingine pia zozote zile zinaweza zikachangia ama rasilimali fedha au watu au ujuzi katika kuhakikisha kwamba Halmashauri zinafikia malengo yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, hili Mheshimiwa Mbunge lisimpe shida, ndani ya Serikali tutaangalia kama linafaa kufanywa hivyo basi tunaweza tukashirikiana na Wizara ya Ujenzi kuona namna ya kutekeleza ahadi hii ya Mheshimiwa Rais.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. HUSSEIN M. BASHE aliuliza:- Wakati wa kampeni za uchaguzi Mheshimiwa Rais aliahidi ujenzi wa daraja la Nhobola na daraja la Butandula pamoja na barabara inayounganisha Kijiji hicho na Kijiji cha Mbogwe:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa ahadi ya ujenzi wa madaraja hayo pamoja na barabara zake?

Supplementary Question 2

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Waziri unafahamu kwamba gawio la Halmashauri za Mfuko wa Barabara ni ndogo sana zinazoenda kwenye Halmashauri zetu, tatizo la barabara siyo la Nzega tu lipo kwa nchi nzima baada ya mvua kunyesha sana mwaka huu barabara nyingi zimeharibika na madaraja. Napenda kufahamu Mheshimiwa Waziri kama upo tayari kuzungumza na Wizara ya Ujenzi ili gawio la Halmashauri ya fedha za Mfuko wa Barabara ziongezeke badala ya hivi sasa Halmashauri zimeshindwa kutengeneza barabara hizo zikiwemo za Babati Mjini?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba gawio ambalo Halmashauri zinapata kama fedha kwa ajili ya matengenezo ya barabara zetu hazina uwezo wa kuhimili mambo ya dharura. Kwa maana hiyo, kweli ipo haja ya kutafuta nguvu ya ziada katika kuhakikisha kwamba kwa dharura za mvua hasa zilivyokuwa nyingi kwa mwaka huu, basi tunapata fedha ili tuweze kukarabati hizo barabara lakini pia kutokuathiri miradi yake ya kawaida iliyokuwa imepanga na Halmashauri katika maombi yao ya fedha za kibajeti. Kwa kufanya hivyo ndiyo maana Waheshimiwa Wabunge Wizara ya Ujenzi mara nyingi imekuwa ikitengewa fedha kwa ajili ya dharura hiyo ambayo kusema kweli inaweza isitoshe, lakini pale kunapokuwa kuna dharura kubwa tunachukua hatua na wanatoa fedha na tunaweza kutengeneza barabara hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kama dharura hiyo itakuwa ni kubwa kama ninavyoisema basi Serikali haitasita kufanya hivyo.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. HUSSEIN M. BASHE aliuliza:- Wakati wa kampeni za uchaguzi Mheshimiwa Rais aliahidi ujenzi wa daraja la Nhobola na daraja la Butandula pamoja na barabara inayounganisha Kijiji hicho na Kijiji cha Mbogwe:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa ahadi ya ujenzi wa madaraja hayo pamoja na barabara zake?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi leo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile fedha za Mfuko wa Barabara ni asilimia 30 kwa TAMISEMI na asilimia 70 kwa Serikali Kuu, hatuoni kutokana na mahitaji kama haya ya makorongo aliyoyasema Mheshimiwa Bashe, sasa wakati umefika wa kugawa fedha hizo asilimia 50 kwa 50 na Wilaya ya Hanang‟ ina makorongo makubwa kutokana na uharibifu wa mazingira lakini Halmashauri kama alivyosema Mheshimiwa Waziri haina uwezo kabisa wa kujenga makorongo hayo?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba, Mfuko wa Barabara unagawanywa kwa asilimia maana mfuko ni mmoja, lakini Wizara ya Ujenzi inayoshughulikia barabara kwa maana TANROADS wanachukua asilimia 70 na Halmashauri zinachukua asilimia 30.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anajaribu kusema hapa kwamba, kwa sasa ni kama vile tunahitaji kuongezewa nguvu kwenye Mfuko wa Barabara katika upande wa barabara zinazosimamiwa na Mamlaka za Serikali za Mitaa takribani ni sawa kwa sawa na zile barabara za Kitaifa zinazounga Mikoa kwa Mikoa kwa sababu uharibifu mkubwa umetokea zaidi huko.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili ni la kisera na kwa hivyo siyo rahisi kulitolea jibu hapa, lakini sichelei kukubaliana na yeye kwamba kweli kwa sasa iko haja ya kuangalia kama tunaweza kubadilisha hizi namba hata angalau tukafika asilimia 40, sasa hili ni jambo la kisera siwezi kuliamua peke yangu hapa kusema ndiyo au hapana, Serikali tumesikia tuendelee kulitafakari tuone kama kuna haja ya kufanya hivyo.