Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 29 Works, Transport and Communication Ofisi ya Rais TAMISEMI. 239 2016-05-26

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Primary Question

MHE. HUSSEIN M. BASHE aliuliza:-
Wakati wa kampeni za uchaguzi Mheshimiwa Rais aliahidi ujenzi wa daraja la Nhobola na daraja la Butandula pamoja na barabara inayounganisha Kijiji hicho na Kijiji cha Mbogwe:-
Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa ahadi ya ujenzi wa madaraja hayo pamoja na barabara zake?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimwia Hussein Mohamed Bashe, Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini kama ifuatavyo:
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua za awali za ujenzi wa daraja la Nhobola na Butandula zimeshafanyika kufuatia kukamilia kwa upembuzi yakinifu (feasibility study), usanifu wa awali (preliminary design) na usanifu wa kina yaani (detailed design) ili kujua gharama za ujenzi wa madaraja yote mawili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa usanifu huo daraja la Nhobola linatarajiwa kugharimu shilingi milioni 589.8 ambazo zitahusisha ujenzi wa barabara yenye kilomita 5.1 kuunganisha kati ya Mbogwe na Nhobola. Ujenzi wa daraja la Butandula utagharimu shilingi milioni 245.57 na utahusisha matengenezo ya sehemu zote korofi zenye urefu wa kilomita 16.2 katika vipande vya barabara ya Ijanija-Butandula, Butandula-Izegwa, Mwangoye na Butandula-Uchama. Kwa kuwa hatua hiyo imekamilika, Halmashauri itaweka katika mpango wa bajeti yake ili kupata fedha hizo na kuanza ujenzi wa madaraja hayo yote mawili.