Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA aliuliza:- Barabara ya Meimosi Nanenane katika Manispaa ya Morogoro imegharimu fedha nyingi sana za Serikali lakini barabara hiyo haikujengwa katika viwango vinavyofaa. Je, kwa nini Wakandarasi waliohusika na ujenzi wa barabara hiyo wasichukuliwe hatua?

Supplementary Question 1

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana yapo mambo ya ajabu sana, barabara hii ya Meimosi ni barabara ambayo imelalamikiwa kutumia fedha nyingi sana za walipa kodi na hili limekuwa question kwa LAAC walipokwenda kuitembelea barabara hii CAG mwenyewe ali-question barabara hii, Mainjinia wa TANROADS wali-question barabara hii na cha kushangaza mpaka sasa kama kweli Waziri anasema barabara haina shida

Ni kwa nini mpaka Serikali haijazindua barabara hii?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili Mheshimiwa Rais alikuja Morogoro mwaka 2018, na akamuagiza Waziri wa TAMISEMI kuunda tume ya kuchunguza barabara hii baada ya kubaini kuna ubadhirifu.

Je, ni kwa nini toka miaka hiyo miwili mpaka sasa hakuna taarifa yoyote ya barabara hii?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge ameuliza swali na ukweli kwamba majibu haya kule kuna Mkuu wa Mkoa tena makini ameleka juzi karibuni kazi imefanyika kwa sasas hayo ndiyo majibu ya Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili anazungumza maelekezo ambayo Mheshimiwa Rais alitoa, Mheshimiwa Rais akitoa maelekezo kwamba ufanyike uchunguzi sehemu fulani aliyetoa maelekezo uchunguzi ufanyike ndiyo unapewa taarifa. Kwa hiyo, sitarajii kwamba taarifa ya Mheshimiwa Rais tutaileta Bungeni hapa labda kama Bunge litaagiza vinginevyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii imejengwa kwa makubaliano na mikataba iliyokuwepo ndiyo imepitiwa. Kama kuna jambo ambalo analizungumza yeye na tofauti na maelezo yetu haya tutalifanyia kazi, lakini kimsingi kwa sasa majibu ya Serikali ni hayo tumetuma wqatu wetu wameenda site Mheshimiwa Waziri amefanya kazi yake na haya ndiyo majibu ya Serikali kwa sasa katika eneo hili, la barabara ya Meimosi Morogoro Mjini, ahsante.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA aliuliza:- Barabara ya Meimosi Nanenane katika Manispaa ya Morogoro imegharimu fedha nyingi sana za Serikali lakini barabara hiyo haikujengwa katika viwango vinavyofaa. Je, kwa nini Wakandarasi waliohusika na ujenzi wa barabara hiyo wasichukuliwe hatua?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana licha ya barabara ya Meimosi kuwa haina matatizo yoyote, lakini Manispaa ya Morogoro barabara za pembezoni ni mbovu kiasi hazipitiki kwa muda wa mvua. Kwa hiyo, kuna mkakati gani wa kutengeneza hizi barabara ? Ahsante.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, swali hili jana limeuliza naomba nirudie majibu ya Serikali kama ambavyo amesema Mheshimiwa Naibu Waziri yule wa Ujenzi, tumeshafanya tathimini kuangalia maeneo mbalimbali ambayo kwa kweli yameathirika na mvua na baadhi ya maeneo hayapitiki, tumeagiza watu wetu Meneja wa TARURA SO, tumeagiza Meneja wa Mikoa yote na Meneja Wilaya walete tathimini yao taarifa tumeshaipata tunaifanyia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuwahakikishie hivyo Waheshimiwa Wabunge na Waheshimiwa watanzania kwamba ndani ya muda mfupi sana maeneo yote ambayo hayapitiki kwa dharura, lakini tutaendelea kuwa tunaboresha ili kuimarisha barabara zetu katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niwaelekeze TANROAD Meneja wa TANROAD Mkoa wa Morogoro apitie maeneo ambapo Mheshimiwa Mbunge amezungumza na yako mambo ambayo unaweza kufanya ndani ya uwezo wao kwa bajeti ndogo iliyopo katika halmashauri na mikoa yetu, lakini yale maeneo makubwa ambayo ni changamoto kwao tumewaambia tuwapokee TAMISEMI ngazi ya taifa tuweze kuyafanyia kazi lengo ni kwamba barabara hizi zipitike wakati wote na huduma kwa jamii yetu iendelee kutolewa kama kawaida. Ahsante.

Name

Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA aliuliza:- Barabara ya Meimosi Nanenane katika Manispaa ya Morogoro imegharimu fedha nyingi sana za Serikali lakini barabara hiyo haikujengwa katika viwango vinavyofaa. Je, kwa nini Wakandarasi waliohusika na ujenzi wa barabara hiyo wasichukuliwe hatua?

Supplementary Question 3

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona, kufuatia mvua kubwa ambazo zinaendelea kunyesha nchini kumekuwa na uharibifu mkubwa sana wa miundombinu jambo ambalo limesababisha vifo kwa baadhi ya wananchi na kudhorota kwa shughuli za kiuchumi na za kijamii.

Je, Serikali ina mkakati gani maalum wa kuhakikisha kwamba baraka hii ya mvua inakuwa fursa na chachu ya maendeleo na siyo majanga kama ilivyo sasa hivi kwenye nchi yetu? Ahsante.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tunao utaratibu kawaida kama sehemu ya mkakati wa kushughulikia hali mvua zinavyokuwa nyingi, ndiyo maana katika bajeti ya mwaka huu unayoendelea kupitia Bunge lako Serikali ilitenga bilioni 8 zaidi ya bilioni 8 kwa ajili ya kumudu dharura zinavyojitokeza, kwa hiyo mkakati tuko nao.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu mvua zimekuwa nyingi ndiyo maana tumeendelea kufanya utambuzi wa mahitaji hasa mvua zinavyoendelea, na hapa ninavyozungumza mpaka kufikia Januari tuna mahitaji ya shilingi bilioni 13.6 kwa ajili ya maeneo ya Mikoa 14 ambayo tumeitambua imekuwa na shida. Kwa hiyo, tunaendelea kupitia utaratibu wa kibajeti Serikali itafanya utaratibu wa kuona namna nzuri ya kutatua maeneo haya.

Mheshimiwa Naibu Spika, yako maeneo mengine yatahitaji mvua ikipungua ndiyo tuende tufanye marekebisho makumbwa, sasa hivi TARURA kushirikiana na TANROAD tunafanya utaratibu wa ku-harmonize yaani kufanya kazi kwa pamoja ili kutengeneza barabara mbadala kwenye maeneo ambayo yana shida ili wananchi waendelee kupata huduma ya barabara mvua zikipungua tutarudi kufanya marejesho makubwa kwenye maeneo ambayo yamepata athari kubwa. Kwa hiyo, utaratibu upo wa kibajeti tutaendelea kuufuata kwa kuzingatia taratibu na sheria ili tuone tunafanya vizuri katika maeneo na kuwanusuru wananchi na hali hii ya mvua kubwa zilizoendelea kunyesha. Ahsante sana.