Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 13 2020-01-29

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA aliuliza:-

Barabara ya Meimosi Nanenane katika Manispaa ya Morogoro imegharimu fedha nyingi sana za Serikali lakini barabara hiyo haikujengwa katika viwango vinavyofaa.

Je, kwa nini Wakandarasi waliohusika na ujenzi wa barabara hiyo wasichukuliwe hatua?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Raisi TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Devotha Mathew Minja, Mbunge wa Viti Maluum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Meimosi-Nanenane yenye urefu wa kilometa 5.1 (Meimosi (2.6 km), Meimosi 2 (1km) na Meimosi 3 (1.5 km) ilijengwa kwa kiwango cha lami nzito (asphalt concrete) kwa gharama ya Shilingi bilioni 11.81. Ujenzi ulianza Julai, 2015 na kukamilika mwaka 2017 chini ya usimamizi wa Mhandisi Mshauri Ms DOCH Ltd ambaye alikabidhi mradi kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro mnamo tarehe 30 Aprili, 2017.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi zote zilizoainishwa kwenye mradi huu zilifanyika kwa viwango vya ubora vilivyoelekezwa na upimaji wa ubora kwa kila hatua ulifanyika. Tangu barabara hii ilipokabidhiwa, haijaonesha udhaifu wowote na inatumika kama ilivyokusudiwa hivyo, Serikali haina sababu yoyote ya kuchukua hatua kwa Mkandarasi aliyejenga barabara hiyo, ahsante.