Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Ipo ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya kilometa nane oinayopita katikati ya Mji wa Itigi. Je, ni lini sasa barabara hii itaanza kujengwa?

Supplementary Question 1

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu ya Serikali ambayo kidogo yana ukakasi, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara hii ya Mkiwa - Rungwa hadi Makongolosi imekuwa ikitengewa pesa kwa muda mrefu toka nimeingia katika Bunge hili na hata Mheshimiwa Rais aliwahi kusimama katika mkutano wa hadhara akiwaambia wananchi wa Itigi kwamba sasa inajengwa na mkandarasi alipatikana lakini hatujui kilichotokea.

Sasa je, Serikali hususani Wizara hii ambayo inayohusika na barabara hii ambayo inahusika na TANROADS, Wizara ya Ujenzi, wako tayari sasa kusema mbele ya Bunge lako tukufu ni lini wataanza kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami kilometa 56.9 ambazo zimetajwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, barabara hii inapita katikati ya Mji wa Itigi, mji wa kibiashara na wananchi wanajishughulisha katika kuhangaika kutafuta maisha yao vizuri, barabara hii sasa imegeuka mto inapitisha maji. Je, ni lini Serikali itafanya haraka kukarabati barabara hii kwa dharura?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, tumemsikia Mheshimiwa Mbunge na kama nilivyosema kwenye jibu la msingi ni kwamba tumeshafanya usanifu na tutawasiliana na wenzetu wa TANROADS tuangalie namna bora ya haraka zaidi kuweza kurekebisha hali hii katika Jimbo lake. Lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama sasa anavyozungumza Mji wa Itigi unapitisha maji; naomba nimuagize Meneja wa TANROADS Mkoa wa Singida na Wilaya hii afanye tathmini ili alete maombi tuone hatua ya haraka zaidi ya kuweza kurekebisha hali hii ili maji yasiweze kupita katika eneo hili na huduma ziweze kuendelea. Ahsante.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Ipo ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya kilometa nane oinayopita katikati ya Mji wa Itigi. Je, ni lini sasa barabara hii itaanza kujengwa?

Supplementary Question 2

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, nilitaka kujua; kwa kuwa gharama ya kutumia asphalt yaani kujenga lami kama zinavyoonekana ni ya ghali na kwa kuwa ahadi za Mheshimiwa Rais ikiwemo barabara za Himo Mjini, Kahe na ya kwenda Kilema kwenye maeneo ya mwinuko zinahitajika zijengwe ili zipitike wakati wote. Nataka kujua, Serikali imefikia wapi kupitia wataalam kuja na teknolojia nyingine ya kutumia calcium oxide na moram ambayo ni rahisi kuliko hii ya asphalt ili ziweze zikatumike kwenye barabara zote nchi nzima na barabara zote ziweze kupitika kwa sababu ziko kwenye hali mbaya sana?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kijibu swali la kaka yangu James Mbatia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli gharama ya kutumia asphalt ni kubwa lakini mara nyingi sana mahitaji ya barabara aina gani ya teknolojia ijengwe ni kutokana na jinsi gani ya ile barabara mahitaji yake yalivyo. Ndiyo maana ukiangalia katika ofisi yetu sasa hivi kuna barabara tunazijengwa kwa double surface dressing na hizi cost yake unaona kwamba ina- range katia ya shilingi milioni 300 mpaka milioni 500 lakini barabara ya asphalt inakwenda mpaka one billion per kilometer.

Sasa unakuja kuona ukiangalia hizi barabara ambazo sasa hivi tunazijenga katika miji mbalimbali tunatumia asphalt kwa sababu mizigo inayopita huko na kwa sababu tunalenga katika ajenda ya kiuchumi lazima tutengeneze barabara ambazo zitaweza kupitisha magari mazito kuhakikisha tunachochea uchumi wa eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, ushauri uliozungumza katika kitengo chetu cha ofisi yetu kuna watu wanafanya research maalum kwa aina mbalimbali ya barabara ya madaraja na ndiyo maana hata ukienda kule Kigoma tumeamua sasa hivi kuna teknolijia nyingine tumetoa Belgium ya ujenzi wa madaraja, kwa hiyo hiyo yote ni juhudi ya Serikali kuangalia nini tufanye katika maeneo gani, lengo kubwa ni kuhakikisha Wanancho wote waweze kufika.

Kwa hiyo, ushauri wako unachukiliwa lakini naamini kwamba Serikali inafanya juhudi kubwa kuhakikisha Wananchi wanapata huduma nzuri ya barabara. Ahsante.