Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 3 2020-01-28

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:-

Ipo ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya kilometa nane oinayopita katikati ya Mji wa Itigi.

Je, ni lini sasa barabara hii itaanza kujengwa?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza utekelezaji wa ahadi iliyotolewa na Mhehsimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kukamilisha usanifu wa barabara inayopita katikati ya Mji wa Itigi yenye urefu wa takribani kilometa nane. Usanifu huo umefanywa kama sehemu ya usanifu wa barabara ya Mkiwa - Itigi - Rungwa - Makongolosi yenye urefu wa kilometa 413 uliosimamiwa na Wakala wa Barabara Tanzania yaani TANROADS. Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara inayopita katikati ya Mji wa Itigi kwa kiwango cha lami itakayojengwa chini ya mradi wa ujenzi Mkiwa -Itigi - Rungwa - Makongolosi ili kufungua fursa za kiuchumi na kijamii katika maeneo hayo. Ahsante.