Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ahmed Ally Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Solwa

Primary Question

MHE. AHMED A. SALUM aliuliza:- Katika Jimbo la Solwa tayari kuna maboma 158 ikiwemo shule za msingi, sekondari na afya na tayari tumeomba fedha ili kukamilisha maboma hayo:- Je, ni kiasi gani cha fedha Jimbo hilo limepata ili kukamilisha maboma hayo?

Supplementary Question 1

MHE. AHMED A. SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante, pamoja na majibu yasiyoridhisha ya Mheshimiwa Naibu Waziri na ni mepesi mepesi sana, naomba sasa niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema hivi, katika Jimbo la Solwa tuna maboma 158, kati ya hayo maboma 40 ni zahanati kwa maana zahanati 32 na nyumba za watumishi ni 10 na maboma 50 ni shule za msingi, 58 tupo kwenye sekondari kwa maana ya maabara. Fedha zinazohitajika ni zaidi ya bilioni 4.7 lakini sijaona commitment ya Serikali ya kuniambia kwamba katika mwaka huu wa fedha au mwaka unaofuata tutatenga kiasi fulani kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma haya. Kwa majibu haya, ninaona kabisa kwamba hata miaka kumi hatuwezi kukamilisha maboma haya ambayo ni nguvu za wananchi tulikwenda kuyakamilisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini sasa Serikali inatoa commitment majibu sahihi kwa wananchi wa Jimbo la Solwa kwenda kukamilisha maboma haya hata kwa awamu tatu polepole ili tukamilishe maboma haya?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, kwanza haya siyo majibu mepesi, kwa sababu Serikali imepeleka fedha shilingi bilioni 29.9 nchi nzima, siyo jambo dogo ni jambo kubwa na la kupongeza. Na Majimbo yote yamepata na Mheshimiwa Mbunge tumetaja kiasi cha fedha ambazo amepata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kumalizia maboma haya ya zahanati, msingi na sekondari ni jambo mtambuka, tunahusisha wadau mbalimbali wa elimu, Serikali yenyewe, Mheshimiwa Mbunge, halmashauri yake na wadau wengine, kwa hiyo hili jambo ni la pamoja. Niseme tu kwamba commitment kwa mfano Halmashauri ya Shinyanga wametenga fedha mapato ya ndani milioni 140 kumalizia maboma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapozungumza niseme tu kwamba wiki iliyopita Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi ya Awamu ya Tano imepeleka fedha shilingi bilioni 68.48 kumalizia maboma ya shule za msingi na halmashauri yake imepata. Kwa hiyo, hii ni commitment kubwa, tunaomba hizi fedha zitumike vizuri, cha muhimu wakurugenzi wa halmashauri wanapoleta maboma kule TAMISEMI wawasiliane na Wabunge wao ili wawe kwenye lugha moja, fedha zikienda Wabunge wajulishwe ili waweze kusimamia utekelezaji, fedha iweze kutumika vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. AHMED A. SALUM aliuliza:- Katika Jimbo la Solwa tayari kuna maboma 158 ikiwemo shule za msingi, sekondari na afya na tayari tumeomba fedha ili kukamilisha maboma hayo:- Je, ni kiasi gani cha fedha Jimbo hilo limepata ili kukamilisha maboma hayo?

Supplementary Question 2

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba nimuulize swali Mheshimiwa Waziri katika Mkoa wa Mwanza, katika mgao wa fedha za maboma kwa ajili ya sekondari, Wilaya ya Kwimba haikupangiwa hata senti tano kwa maana hata boma moja, ilisahaulika na tayari tulikuwa tumeshaleta Shule za Sekondari za Wala, Kikubiji, Malya, Wungumarwa, Ndami, Mwabomba, Shilembo, Iseni na Mwangalanga. Mheshimiwa Waziri, tunaomba tupate majibu kwa nini Wilaya ya Kwimba katika mgao huo wa bilioni
29.9 ilirukwa yenye Majimbo mawili na tayari tulikuwa tumeshaweka majina.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mheshimiwa Mbunge ameshawasilisha hoja yake hiyo Wizarani na nilimuahidi kwa niaba ya Wizara kwamba watakapoanza kugawa fedha za EPFR sekondari maeneo yote siyo kwake tu, maeneo yote ambayo yalivukwa kwa bahati mbaya maana huo haukuwa mpango mahsusi wa makusudi, ilikuwa ni bahati mbaya tu, tutazingatia Kwimba pamoja na maeneo mengine yote ambayo yalirukwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, niombe, wakati tunaomba taarifa hizi, ndiyo maana nikasema hapa Wakurugenzi na maafisa elimu wetu wa sekondari na msingi, wanapoombwa walete taarifa ya maboma TAMISEMI tunawaelekeza washauriane na kupeana taarifa na Wabunge ili wazungumze kwenye lugha moja. Imegundulika kuna maboma mengine yameletwa na Waheshimiwa Wabunge lakini kule wanasema kwamba hiyo siyo shida kubwa sana. Kwa hiyo, tumesema tunaposema tunahitaji maboma, wakurugenzi na maafisa elimu wakitoa taarifa wapitishe au kushauriana na Waheshimiwa Wabunge ili tuzungumze pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vivyo hivyo, fedha zikipelekwa kama zilivyopelekwa sasa, tumepeleka bilioni 29.9 kuna baadhi ya Wabunge hawakupewa taarifa, tumepeleka bilioni 68.48 wiki iliyopita, inawezekana Wabunge hawajui;
kwa hiyo, Wabunge wajulishwe ili wajue lakini kama kuna mahali pesa imeletwa kwenye halmashauri una hali mbaya sana kwenye shule ya msingi au sekondari, mkurugenzi anajua anaandika barua kwa Katibu Mkuu TAMISEMI anaomba kubadilisha matumizi ili kutibu shida kubwa, hii nyingine itaendelea kusubiri, asante.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AHMED A. SALUM aliuliza:- Katika Jimbo la Solwa tayari kuna maboma 158 ikiwemo shule za msingi, sekondari na afya na tayari tumeomba fedha ili kukamilisha maboma hayo:- Je, ni kiasi gani cha fedha Jimbo hilo limepata ili kukamilisha maboma hayo?

Supplementary Question 3

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ni wazi kwamba kwa nchi nzima tuna matatizo makubwa sana ya upungufu wa madarasa. Sasa nilitaka kujua Serikali ina mpango mkakati gani wa kuhakikisha kwamba walau kwa kila mwaka wanajenga madarasa kadhaa wakati wanajua kabisa kwamba projection ya idadi ya watoto wanaijua. Sasa nilitaka kujua wana mkakati gani mahsusi wa kuhakikisha kwamba hili tatizo walau kila mwaka watakuwa wanajenga madarasa kadhaa kwa kila mkoa na wilaya.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba tumeona hiyo changamoto wakati ambapo watoto wanaenda kuingia kidato cha kwanza, darasa la awali na darasa la kwanza ilionekana kuna upungufu mkubwa wa madarasa. Tumeshawaelekeza wakurugenzi wanafahamu, mwaka huu projection darasa la saba wanamaliza wangapi, kwa hiyo vacancy itakuwa ni kiasi gani, form four wanamaliza wangapi, vivo hivyo kidato cha sita, wafanye hiyo kazi na kila halmashauri, Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa wameelekezwa lakini sisi kwenye bajeti tumetenga zaidi ya bilioni 90 kwa ajili ya kazi hiyo, ahsante.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. AHMED A. SALUM aliuliza:- Katika Jimbo la Solwa tayari kuna maboma 158 ikiwemo shule za msingi, sekondari na afya na tayari tumeomba fedha ili kukamilisha maboma hayo:- Je, ni kiasi gani cha fedha Jimbo hilo limepata ili kukamilisha maboma hayo?

Supplementary Question 4

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kupata nafasi hii. Pamoja na jitihada kubwa za Serikali zilizofanywa za kupeleka fedha kwa ajili ya kumalizia maboma, bado Wilaya ya Tanganyika kuna uhitaji mkubwa wa kumalizia majengo ambayo yalianzishwa kwa nguvu za wananchi hasa ya shule za sekondari Ablulamatam, Kapalamsenga, Tongwe na Mnyagala kwenye kituo cha afya. Je, ni lini Serikali itawaunga mkono wananchi ambao wamejitolea kwa kiwango kikubwa.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba tunatambua kuna uhitaji mkubwa na kuna majengo ambayo yamejengwa kwa nguvu za wananchi na wadau mbalimbali na Serikali yenyewe. Na ndiyo maana tuliekeza kwenye fedha ile ya maboma, kazi mojawapo ni kuchangia na kumalizia nguvu za wananchi. Na hata hizi ambazo zimepekwa sawa bilioni 68.48 ambayo ni wiki iliyopita tu, hizi fedha zina maelekezo, humu kuna fedha ambazo zinaenda kwenye ujenzi lakini pia kuna fedha za ku- balance ikama, kuna hoja ilikuwepo hapa kwamba kuna walimu wa kike shule moja hakuna walimu wa kiume, au walimu wa kiume hakuna walimu wa kike; wakurugenzi watumie fedha hii walimu walipwe ili waweze ku-balance kama kule halmashauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kubwa ambalo tumeomba, shule ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja, fedha zimeenda kwenye halmashauri yake, ni wao sasa kuangalia je, hiyo fedha itumike namna gani. Lakini kadri tutakapopata uwezo tutakuwa tunazingatia maeneo ambayo yana changamoto kubwa ili kuweza kuondoa hiyo kero lakini hasa kuchangia na kushiriki katika nguvu za wananchi ili wasiendelee kulalamika.