Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 30 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 244 2019-05-17

Name

Ahmed Ally Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Solwa

Primary Question

MHE. AHMED A. SALUM aliuliza:-

Katika Jimbo la Solwa tayari kuna maboma 158 ikiwemo shule za msingi, sekondari na afya na tayari tumeomba fedha ili kukamilisha maboma hayo:-

Je, ni kiasi gani cha fedha Jimbo hilo limepata ili kukamilisha maboma hayo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ahmed Ally Salum, Mbunge wa Solwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka wa fedha 2018/ 2019, Serikali imetoa kiasi cha shilingi bilioni 29.9 kwa ajili ya kukamilisha maboma 2,392 ya shule za sekondari ambazo Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga imepatiwa kiasi cha shilingi milioni 87.5 kwa ajili ya kukamilisha maboma saba ya shule za sekondari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea na ukarabati/ujenzi wa vituo vya afya na zahanati 352 kwa gharama ya shilingi bilioni 184.6 ambapo kipaumbele ni ukamilishaji wa maboma yaliyoanza kujengwa kwa nguvu za wananchi. Ukarabati wa vituo 352 unahusisha ukamilishaji wa maboma 199 ya vituo vya afya na zahanati.

Katika Halmashauri ya Wilaya Shinyanga, Serikali imefanya ukarabati wa Kituo cha Afya Samuye na Tinde kwa gharama ya shilingi milioni 900. Vilevile, katika mwaka wa fedha 2019/2020 kupitia mapato yake ya ndani Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga imetenga kiasi cha shilingi milioni 140 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati.