Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI (K.n.y. MHE. BONNAH M. KALUWA) aliuliza:- Barabara ya Segerea Sheli kupitia Seminari, Stakishari Polisi kwenda kutokea Majumba Sita ni suluhisho la Msongamano wa magari yanayopita barabara ya Segerea - Tabata kutokea barabara ya Mandela, lakini kwa sasa barabara hiyo haipitiki kwa kuwa daraja la Seminari liliondoshwa na maji ya mvua mwaka 2013. Je, Serikali haioni kuna umuhimu wa kujenga daraja la Seminari ili kuondoa tatizo hilo na kurahisisha huduma kwa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa matatizo ya daraja la Segerea ni ya muda mrefu sana na kila wakati liko katika upembuzi yakinifu; na kwa kuwa Serikali sasa inataka kufanya tena usanifu kupitia TARURA; mimi nauliza swali: Je, kwa nini TARURA sasa wasianze kujenga hilo daraja la Segerea badala ya kuanza tena upembuzi yakinifu ili kuwasaidia wananchi wa Segerea ambao wanapata shida sana kutokana na ukosefu wa daraja lile?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kwa kuwa matatizo wanayopata wananchi wa Segerea yanafanana kabisa na yale wanayowapata watu wa Jangwani pale maeneo ya Magomeni: Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha daraja la Jangwani ili kuondoa matatizo ya kufunga barabara ile wakati wa mvua nyingi kila wakati?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi maswali yote mawili yanafanana. Adha ambayo tunaipata kutokana na lile daraja ambalo mto unahama, lakini na swali lake la pili kuhusiana na daraja la Jangwani ambalo linajaa maji kila muda, naomba Mheshimiwa Mbunge arejee katika siku moja ambayo nilijibu hapa, kwamba jumla ya shilingi bilioni 260 zimetengwa kwa ajili ya kuanza usanifu na kuhakikisha kwamba tunapata suluhu ya kudumu kuhusiana na Mto Msimbazi. Pia akubaliane name, kama ambavyo tunaweza tukafanya makosa tukajenga hilo daraja, baada ya muda likawa linaendelea kujaa, ndiyo maana tumemwomba Mheshimiwa Mbunge avute subira kama ambavyo nimetoa majibu katika jibu langu la msingi, kwamba ni vizuri tukafanya usanifu wa kina kujua hasa tatizo ili ujenzi ukikamilika tuwe tumepata suluhu ya kudumu.

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI (K.n.y. MHE. BONNAH M. KALUWA) aliuliza:- Barabara ya Segerea Sheli kupitia Seminari, Stakishari Polisi kwenda kutokea Majumba Sita ni suluhisho la Msongamano wa magari yanayopita barabara ya Segerea - Tabata kutokea barabara ya Mandela, lakini kwa sasa barabara hiyo haipitiki kwa kuwa daraja la Seminari liliondoshwa na maji ya mvua mwaka 2013. Je, Serikali haioni kuna umuhimu wa kujenga daraja la Seminari ili kuondoa tatizo hilo na kurahisisha huduma kwa wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali. Kwa kuwa swali la msingi linahusu muunganiko wa daraja na barabara; na kwa kuwa sote tumeshuhudia kwa macho au kupitia vyombo vya habari jinsi Mji wa Dar es Salaam ulivyoharibika kwa mafuriko; na kwa kuwa ujenzi wa madaraja na barabara umechangia kuhakikisha kwamba usafiri umekuwa siyo mzuri kwa watoto wetu, kwa watu wazima na kwa wagonjwa kutokana na mafuriko yaliyokuwepo: Je, Serikali itachukua hatua gani za dharura kuhakikisha mafuriko hayo hayataendelea tena na hayatatokea; na kuhakikisha Mji wa Dar es Salaam unarudi kama ulivyokuwa hapo awali?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza sisi sote ni mashuhuda kwamba mvua ambazo zinanyesha Dar es Salaam sasa hivi ni nyingi sana ambazo hatukuzitarajia. Kwa hiyo, kwanza ni sisi wote kushiriki kuhakikisha kwamba tunapambana na tabianchi ambayo inaleta mwongezeko wa mvua ambazo hatuwezi kuzitarajia. Sasa tunafanyaje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kipekee nichukue fursa hii kupongeza UDART jinsi ambavyo wamekuwa wakipambana na hali hii pale ambapo maji yanakuwa yamezidi, tunalazimika kusimamisha usafiri ili kusije kukawa na madhara makubwa, lakini immediately zinafanyika juhudi za kuhakikisha maji yale yanaondolewa na usafiri unarejea kama kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge, ni ukweli usiopongika, kwa mvua ambazo zinanyesha sasa hivi; na bahati nzuri watabiri wa hali ya hewa walitufahamisha kwamba mvua zinatarajiwa kunyesha nyingi sana, kwa hiyo, hakuna namna ambavyo tunaweza tukasema tutafanya kuzuia mvua kwa sababu ni calamity ambayo inaweza ikatokea muda wowote. Kwa hiyo, tuwe na subira, hali ya Dar es Salaam itarudia katika hali yake baada ya mvua hizi kukoma kama ambavyo wametuambia.

Name

Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI (K.n.y. MHE. BONNAH M. KALUWA) aliuliza:- Barabara ya Segerea Sheli kupitia Seminari, Stakishari Polisi kwenda kutokea Majumba Sita ni suluhisho la Msongamano wa magari yanayopita barabara ya Segerea - Tabata kutokea barabara ya Mandela, lakini kwa sasa barabara hiyo haipitiki kwa kuwa daraja la Seminari liliondoshwa na maji ya mvua mwaka 2013. Je, Serikali haioni kuna umuhimu wa kujenga daraja la Seminari ili kuondoa tatizo hilo na kurahisisha huduma kwa wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunpa nafasi ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza. Kule Moshi Vijijini kwa asili kabisa hali ni mbaya sana wakati wa mvua kwa sababu ya aina ya udongo ambao uko kule, lakini hali ni mbaya zaidi katika Kata ya Arusha chini kule TPC katika kijiji cha Chemchem ambacho kimetengwa na Mto Kikavu ambao wakati wa mvua kunakuwa hakuna mawasiliano kabisa na sehemu nyingine zozote za Jimbo.

Mhshimiwa Mwenyekiti, toka mwaka 2012, daraja hilo la Chemchem la hapo kwenye kivuko cha Mto Kikavu limekuwa likitengewa fedha, lakini ujenzi mpaka kesho haujaanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimwulize Mheshimiwa Waziri, ni lini mtakuja kuwaunganisha watu wa Chemchem na wenzao wa huku Tanzania?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kijiji ambacho Mheshimiwa Mbunge anakitaja kwangu mimi ndiyo nakisikia. Katika swali la msingi sikutarajia swali la kutoka huko ambako Mheshimiwa Komu anasema. Ni vizuri sasa nimwambie Mheshimiwa Mbunge, baada ya kipindi hiki cha maswali na majibu ni vizuri tukawasiliana tujue uhalisia ukoje ili tuweze kutatua tatizo ambalo lipo.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI (K.n.y. MHE. BONNAH M. KALUWA) aliuliza:- Barabara ya Segerea Sheli kupitia Seminari, Stakishari Polisi kwenda kutokea Majumba Sita ni suluhisho la Msongamano wa magari yanayopita barabara ya Segerea - Tabata kutokea barabara ya Mandela, lakini kwa sasa barabara hiyo haipitiki kwa kuwa daraja la Seminari liliondoshwa na maji ya mvua mwaka 2013. Je, Serikali haioni kuna umuhimu wa kujenga daraja la Seminari ili kuondoa tatizo hilo na kurahisisha huduma kwa wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwe Mwenyekiti, nakushukuru sana. Naomba niongeze swali dogo la nyongeza, kwamba kule kwangu kuna barabara ya kutoka Waama mpaka Masusu na hatimaye mpaka kule Lalaji na barabara nyingine ya Maskaroda na kwenda Lambo na kwenda Dareda ambapo zinaunganisha wananchi na hospitali na nilishatoa ombi: Je, Serikali inasemaje ili kunisaidia na watu wale ambao wana kilomita 20 kwenda kwenye hospitali wapate namna ya kufika? Nashukuru sana.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nilipata fursa ya kwenda Jimboni kwa Mheshimiwa Dkt. Nagu kutatua mgogoro wa kijiji na tukafanikiwa kuutatua mgogoro ule. Ingekuwa vizuri sana Mheshimiwa Nagu kama ungeniambia tukapata na fursa ya kwenda kutembelea huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu lengo la Serikali ni kuhakikisha kwamba huduma ya usafiri na hasa kwenda hospitali kama ambavyo yeye amesema kwenye swali lake, ni vizuri tukawasiliana na Meneja wa TARURA tujue nini hasa ambacho kinatakiwa kifanyike ili wananchi wetu waendelee kupata huduma na hasa ya kwenda hospitali.