Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 27 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 221 2019-05-14

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI (K.n.y. MHE. BONNAH M. KALUWA) aliuliza:-

Barabara ya Segerea Sheli kupitia Seminari, Stakishari Polisi kwenda kutokea Majumba Sita ni suluhisho la Msongamano wa magari yanayopita barabara ya Segerea - Tabata kutokea barabara ya Mandela, lakini kwa sasa barabara hiyo haipitiki kwa kuwa daraja la Seminari liliondoshwa na maji ya mvua mwaka 2013.

Je, Serikali haioni kuna umuhimu wa kujenga daraja la Seminari ili kuondoa tatizo hilo na kurahisisha huduma kwa wananchi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba nijibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa Segerea, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, daraja la Seminari Segerea liko katika barabara ya Majumba Sita Stakishari yenye urefu wa kilomita 2.93. Hapo awali usanifu wa kujenga daraja hili ulishafanyika. Hata hivyo, ipo changamoto inayotokana na mto kutanuka, hivyo inahitajika kufanyika stadi ya kina na mapitio ya usanifu wa awali ili kupata mahitaji halisi ya ujenzi wa daraja kutokana na changamoto hiyo. Mara baada ya kukamilika kwa mapitio ya usanifu na tathmini ya gharama, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kujenga daraja hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2019/2020 TARURA imepanga kufanya usanifu wa kina wa daraja hilo ili kujua gharama halisi kwa maana ya cost estimates zinazohitaji kulijenga. Namwomba Mheshimiwa Mbunge avute subira wakati Serikali inachukua hatua hizo muhimu kwa ajili ya kutatua tatizo la kukosekana kwa daraja hilo.