Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y MHE. LATHIFAH H. CHANDE) aliuliza:- Serikali iliahidi Mji wa Liwale Kufanyiwa usanifu wa mradi wa maji:- (a) Je, ni lini mradi huo uliofanyiwa usanifu utakamilika na kuanza kutoa huduma ya maji kwa wananchi wa Liwale? (b) Je, ni kata zipi zilizopo katika Wilaya ya Liwale ambazo zitanufaika na mradi huo wa maji?

Supplementary Question 1

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, utakumbuka wakati Mheshimiwa Rais, Dkt. John Joseph Pombe Magufuli analihutubia Bunge hili wakati wa ufunguzi wake alisema asingependa tena kusikia tena hili neno la upembuzi yakinifu likiendelea kutumika kwa sababu linaonesha ni ambalo limekuwa liki-roll on mambo yaani ni utaratibu tu wa kutaka kuchelewesha. Sasa tunafahamu Serikali ina mipango yake na hapa unasema specifically kwamba itafanyika kwenye Mwaka wa Fedha 2019/2020. Sasa je, Serikali iko tayari kutueleza ni lini specifically mradi huu utaanza kufanyika ili kuondoa kero ya watu wa Liwale? Swali langu la kwanza.

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, ni kwamba matatizo yaliyoko Liwale yanafanana kabisa na matatizo yaliyoko Jimbo la Ndanda hasa kwenye Kata ya Nanganga. Kata ya Nanganga kuna mradi ambao ulikusudiwa upeleke maji kwenye vijiji vya Chinyanyila, Nanganga A na B, Mkwera moja na Mbili pamoja na Mumburu 1 na 2 pamoja na vijiji vya Chipite. Mpaka sasa hivi tunaonge ahapa mradi ule ulitekelezwa chini ya kiwango na inasemekana kwamba mkandarasi amekimbia hajaukamilisha na hajaukabidhi kufanya commissioning kama ambavyo ilikusudiwa.

Sasa nimuulize Mheshimiwa Waziri, je, yuko tayari kupeleka wataalam wake kutoka Makao Makuu ya Wizara ya Maji wakauchunguze mradi huu na kutoa majibu stahiki kwa wananchi wale?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, napenda kumjibu Mheshimiwa Mbunge, moja; Wizara yetu ya Maji jukumu lake ni kuhakikisha Watanzania wanapata maji safi na salama lakini katika kuhakikisha tunatatua tatizo la maji katika Mji huu wa Liwale, kuna miradi ambayo inaendelea. Moja, mradi wa Kipure pamoja na Mangilikiti na Nanyungu yote ni katika kuhakikisha tunatatua tatizo la maji na hata katika bajeti hii yetu ya 2019/2020 tumetenga zaidi ya 699,000,000 katika kuhakikisha tunatatua tatizo la maji. Kubwa, Mhandisi wa Mkoa, wahandisi wa wilaya wahakikishe fedha hizi zinatumika kuweza kutatua tatizo la maji.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu mradi ambao ameuelezea nataka nimhakikishuie, sisi kama Wizara ya Maji hatutakuwa kikwazo kutuma wataalam kwenda kuukagua mradi huo na mimi kama Naibu Waziri niko tayari kuongozana na wewe katika kuhakikisha tunaenda kuchukua hatua nzitio. Ahsante.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y MHE. LATHIFAH H. CHANDE) aliuliza:- Serikali iliahidi Mji wa Liwale Kufanyiwa usanifu wa mradi wa maji:- (a) Je, ni lini mradi huo uliofanyiwa usanifu utakamilika na kuanza kutoa huduma ya maji kwa wananchi wa Liwale? (b) Je, ni kata zipi zilizopo katika Wilaya ya Liwale ambazo zitanufaika na mradi huo wa maji?

Supplementary Question 2

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru, naomba kuuliza swali la nyongeza, Korogwe Mji tuna kijiji kinaitwa Mahenge, kiko nje kabisa ya Mji wa Korogwe na katika mpango wa miji 28, sina hakika kama kinaweza kikafikiwa na ule mradi wa maji.

Je, mtakuwa tayari kukipatia maji kijiji hicho kwa kuwapa kisima cha maji kirefu?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge anafanya kazi kubwa sana katika Jimbo lake wala haina haja ya kulalamika sana kwa sababu ukimuona mtu mzima ujue kuna jambo. Labda tuwaagize watu wa DDCI waende kuchimba kisima haraka pale ili wananchi wake waweze kupata maji safi na salama.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y MHE. LATHIFAH H. CHANDE) aliuliza:- Serikali iliahidi Mji wa Liwale Kufanyiwa usanifu wa mradi wa maji:- (a) Je, ni lini mradi huo uliofanyiwa usanifu utakamilika na kuanza kutoa huduma ya maji kwa wananchi wa Liwale? (b) Je, ni kata zipi zilizopo katika Wilaya ya Liwale ambazo zitanufaika na mradi huo wa maji?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika mradi wa kutafuta chanzo cha pili cha mbadala cha maji ya Wilaya ya Liwale palitolewa shilingi milioni 300 na DDCIA walishaanza kufanya kazi hiyo lakini wamechimba visima viwili ambavyo vina uwezo wa kutoa maji lita 5,000 lakini visima vile vimetelekezwa mpaka leo.

Je, Serikali iko tayari kutoa fedha kwa ajili ya kwenda kufanya uendelezaji wa visima vile ambavyo viko katika Kijiji cha Makata na kijiji na Mikunya?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza labda kwa nia njema kaisa katika kuhakikisha visima hivi vinakuwa endelevu labda baada ya saa saba nikutane na Mheshimiwa Mbunge na tuweze kufanya mawasiliano na wenzetu ili tangalie ni namna gani tunaweza tukasaidiana naye. Ahsante sana.