Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 26 Water and Irrigation Wizara ya Maji 214 2019-05-13

Name

Lathifah Hassan Chande

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y MHE. LATHIFAH H. CHANDE) aliuliza:-

Serikali iliahidi Mji wa Liwale Kufanyiwa usanifu wa mradi wa maji:-

(a) Je, ni lini mradi huo uliofanyiwa usanifu utakamilika na kuanza kutoa huduma ya maji kwa wananchi wa Liwale?

(b) Je, ni kata zipi zilizopo katika Wilaya ya Liwale ambazo zitanufaika na mradi huo wa maji?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa ruksa yako kwanza naomba nitoe pole kwa wananchi wa Pangani na Chama cha Mapinduzi na wanaCCM wote kwa kuondokewa na Mzee wetu ndugu Hamis Mnegerwa ambaye ni Mwenyekiti wa chama chetu Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Pangani. Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi. Amin.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lathifah Chande, Mbunge wa Viti Maalum lenye sehemu (a), (b) na (c) kwa pamoja kama ifuatavyo;

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto ya upatikanaji wa maji katika Mji wa Liwale ili kutatua changamoto hiyo, Serikali inatekeleza mipango ya muda mrefu na muda mfupi. Kwa upande wa muda mfupi katika mwaka wa fedha 2018/2019 Serikali imekamilisha mradi wa uboreshaji wa huduma ya maji katika Mji wa Liwale.

Mheshimiwa Spika, kazi zilizotekelezwa katika mradi huo ni ukarabati wa kituo cha kusukuma maji, ununuzi na ufungaji wa pampu, ununuzi na ulazaji wa mabomba, usambazaji maji umbali wa kilometa 16 pamoja na ununuzi wa dira za maji 200 kwa gharama ya shilingi milioni 264. Kukamilika kwa mradi huo kumeongeza hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kutoka masaa matano kwa siku hadi masaa 12 kwa siku.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa muda mrefu, Serikali imepanga kufanya upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na uandaaji wa vitabu vya zabuni ambazo kazi hiyo imepangwa kufanyika mwaka wa fedha 2019/2020. Kukamilika kwa kazi hiyo kutatoa gharama halisi ya utekelezaji wa mradi mkubwa katika Mji wa Liwale pamoja na kuainisha kata zitakazonufaika na mradi huo.