Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Juma Khatib

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chonga

Primary Question

MHE. MOHAMMED JUMA KHATIB aliuliza:- Je, ni katika mazingira gani Askari Polisi anapaswa au hulazimika kumtesa Mtuhumiwa wa makosa mbalimbali wakati akiwa mikononi mwake au kwenye Kituo cha Polisi?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMMED JUMA KHATIB: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu hayo nina maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai pamoja na Kanuni za Utendaji wa Jeshi Polisi bado jambo hili linaendelea na ni sugu sana.

Je, Serikali haioni kwamba iko haja ya kubadili mfumo wa utendaji kazi wa Polisi likaingizwa suala la haki za binadamu ili kuwa-conscientious Polisi katika utendaji wao wa kazi wakazizingatia hizo haki za binadamu?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili, kwa kuwa Katiba yetu inakataza uteswaji na pia kwa kuwa kuna Mkataba wa Kimataifa wa Convention Against Torture, je, Serikali haioni kwamba iko haja ya kuridhia Mkataba huu ili hawa watu wanaoteswa wakapata fursa ya kwenda kushtaki katika Mahakama za Kimataifa? Ahsante sana.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mohamed Khatib, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na pendekezo lake la kuubadili mfumo, tunadhani tatizo siyo mfumo, mfumo wa Jeshi letu la Polisi uko vizuri kwani Askari Polisi kabla hajaajiriwa tuna utaratibu mzuri wa kutoa mafunzo. Moja katika mambo ambayo tunayazingatia kuwaelimisha kuhusiana na sheria na kanuni pamoja na kutenda kazi zao kwa uadilifu kwa kufuata sheria na kanuni hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini inapotokea changamoto ambazo zinahusu ukiukwaji wa sheria, ni matatizo ya baadhi ya Askari mmoja mmoja. Kama nilivyojibu katika swali lake la msingi kwamba tunapogundua kwamba kuna Askari ambaye anafanya vitendo hivyo vya kunyanyasa raia huwa tunachukua hatua mbalimbali ikiwemo kuwashtaki na kuwafukuza kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi kwa maelezo hayo naona nimejibu maswali yake yote mawili kwa pamoja.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. MOHAMMED JUMA KHATIB aliuliza:- Je, ni katika mazingira gani Askari Polisi anapaswa au hulazimika kumtesa Mtuhumiwa wa makosa mbalimbali wakati akiwa mikononi mwake au kwenye Kituo cha Polisi?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kumekuwa na malalamiko kutoka kwa watuhumiwa wanaoteswa wakiwa mikononi mwa Polisi kwa lengo la kulazimishwa kusema ukweli, hasa ule ambao Polisi wanautaka wakati mtuhumiwa ana haki ya kutoa hoja yake au kuzungumza ukweli akiwa na Wakili au Mahakamani.

Je, Serikali haioni ni muda muafaka wa kufuatilia mateso haya ambayo watuhumiwa wanapewa na Askari ili kuondoa malalamiko haya?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Ushahidi ya mwaka 1967, kifungu cha 31, inaeleza kuhusu namna ambavyo Polisi wanaweza kutumia nguvu kiasi katika kumhoji mtuhumiwa ili waweze kupata ushahidi. Pia sheria hiyohiyo inaeleza kwamba ushahidi ambao utapatikana si lazima Mahakama uuzingatie, Mahakama itazingatia ukweli wa jambo husika. Tafsiri yake ni nini? Tafsiri yake ni kwamba inapelekea kuwa-discourage Polisi kutumia nguvu katika kupata ushahidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimezungumza katika jibu la msingi la swali kwamba tunapogundua kwamba kuna raia ambaye amefanyiwa vitendo ambavyo si kwa kibinadamu na Polisi basi sisi huwa tunachukua hatua. Tunaomba tutoe wito na rai kwa wananchi wote pale itakapotokea wananchi kupata madhara kama hayo basi wachukue hatua stahiki za kutoa taarifa ili tuweze kuchukua hatua. Hatuwezi kuliruhusu au kukubali wananchi wetu wanyanyaswe na baadhi ya skari wetu ambao pengine hawafuati maadili ya kazi zao.