Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 25 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 205 2019-05-10

Name

Mohamed Juma Khatib

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chonga

Primary Question

MHE. MOHAMMED JUMA KHATIB aliuliza:-

Je, ni katika mazingira gani Askari Polisi anapaswa au hulazimika kumtesa Mtuhumiwa wa makosa mbalimbali wakati akiwa mikononi mwake au kwenye Kituo cha Polisi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohammed Juma Khatibu, Mbunge wa Chonga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura ya 20, kifungu cha 11 kinaelekeza namna ya ukamataji. Aidha, kifungu hiki mahsusi cha ukamataji, hakimruhusu askari kumpiga au kumtesa mtuhumiwa wa makosa mbalimbali wakati akiwa mikononi mwa Polisi au kwenye Kituo cha Polisi.

Mheshimiwa Spika, Kanuni za Kudumu za Utendaji wa Jeshi Polisi la (PGO) zinakataza na kuelekeza utendaji mzuri wa Askari Polisi, ambapo askari yeyote atakapobainika kufanya vitendo vya kumpiga au kumtesa mtuhumiwa huchukuliwa hatua za kunidhamu ikiwepo kufukuzwa kazi na au kufikishwa Mahakamani.