Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. HASNA S. MWILIMA aliuliza:- Jiografia ya Halmashauri ya Uvinza ni mbaya na kusababisha wanafunzi wanaomaliza Kidato cha Nne kutoka mwambao wa Ziwa Tanganyika kusafiri zaidi ya kilometa 200 kufuata Shule za Kidato cha Tano na Sita zilizopo katika ukanda wa Reli:- (a) Je, kwa nini Serikali isianzishe Shule za Kidato cha Tano na Sita kwenye Kata nane za Ukanda wa Ziwa Tanganyika ili kuwapunguzia usumbufu wanafunzi hao? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati na kuongeza miundombinu katika Shule za Kidato cha Tano na Sita Rugufu Wasichana na Wavulana ambazo miundombinu yake ni chakavu na haitoshelezi?

Supplementary Question 1

MHE. HASNA S. MWILIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Naibu Waziri na ninaishukuru pia Serikali kwa hiyo fedha ambayo imetuletea.

Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, ni kweli kwamba tunazo hizo High School mbili kwa maana ya Lugufu Boys na Lugufu Girls. Shule hizi kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri, zimeanzishwa kwenye majengo chakavu yaliyokuwa yakitumika na wakimbizi. Hali ya hizo shule ni mbaya sana na hata hiyo shilingi milioni 150 waliyoleta, yaani inakuwa haionekani imefanya nini kutokana na mazingira halisi tuliyonayo pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata umeme na maji kwenye hizi shule, hakuna. Sasa swali langu kwa Naibu Waziri: Je, ni lini sasa Serikali itaweza kutatua changamoto ya miundombinu iliyoko Lugufu Boys na Lugufu Girls sambamba na kuwapelekea umeme na maji?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili ni kweli kabisa kwamba Halmashauri inaangalia uwezekano wa kuanzisha Kidato cha Tano na cha Sita kwenye Sekondari zetu za Buhingu na Sekondari ya Sunuka. Kwenye majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ameonyesha kwamba Halmashauri inatumia pesa zake za ndani. Sisi wote ni mashahidi, hali ya kipato cha Halmashauri sasa hivi ni mbaya sana. Kwa hiyo, naiomba Wizara; swali langu ni: Je, Wizara haioni sasa ni vyema ituletee fedha kwa ajili ya kuendeleza miundombinu kwenye Shule ya Sekondari ya Sunuka na Shule ya Sekondari ya Buhingu ili tuweze kuwa na Kidato cha Tano na cha Sita?

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, hawa ni miongoni mwa Wabunge jembe wanawake wa Majimbo ambao wanafanya kazi kubwa sana kuwatetea Watanzania wenzao na hasa katika suala zima la elimu na unaona anazungumza habari ya wanawake ili na wao wafikie hatua kama yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza anataka kujua ni namna gari Serikali imejipanga kuboresha majengo ya shule hasa ambazo amezitaja ambazo ni chakavu. Ni utaratibu wa Serikali kuboresha majengo haya na bahati nzuri kwenye Bunge hili Tukufu ambalo linaendelea tumeishapitisha bajeti ya TAMISEMI na tuna fedha mle karibu shilingi bilioni 90 ambayo itakwenda kufanyakazi EP4R. Kwa hiyo, tutagawa fedha katika maeneo yale na ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge tutazingatia hili katika kupeleka fedha kwenye eneo hilo kwa shughuli ambayo ameitaja.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, amezungumza habari ya Kidato cha Tano na Kidato cha Sita. Siyo kwamba Serikali imejitoa kushiriki. Tunachosema ni kwamba Halmashauri lazima ianze. Kuna mambo ya msingi kwa mfano ardhi, iwe na umiliki hatuna fedha ya kulipa fidia, lakini wachangie kupitia mapato yao ya ndani, nasi kama Wizara tunaongezea pale na kuboresha pamoja na kupeleka wataalam na maabara nyingine. Kwa hiyo, tutachangia jambo hili ila walianzishe. Kipaumbele ni kwamba kila Tarafa angalau iwe na High School moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kusema kwamba ni muhimu tungeomba kuhimiza, pamoja na kuanzisha Shule za Kidato cha Tano na cha Sita, ukweli ni kwamba hizi shule ni za Kitaifa, zikianzishwa maana yake utapeleka watoto kutoka nchi nzima. Kwa hiyo, unaweza kubadilisha miundombinu mingine ili watoto wa eneo lile kama ni Uvinza, utaenda kuwasaidia Nguruka. Ni muhimu kuhimiza elimu ya msingi, sekondari, halafu wengine tunaenda huko mbele.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. HASNA S. MWILIMA aliuliza:- Jiografia ya Halmashauri ya Uvinza ni mbaya na kusababisha wanafunzi wanaomaliza Kidato cha Nne kutoka mwambao wa Ziwa Tanganyika kusafiri zaidi ya kilometa 200 kufuata Shule za Kidato cha Tano na Sita zilizopo katika ukanda wa Reli:- (a) Je, kwa nini Serikali isianzishe Shule za Kidato cha Tano na Sita kwenye Kata nane za Ukanda wa Ziwa Tanganyika ili kuwapunguzia usumbufu wanafunzi hao? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati na kuongeza miundombinu katika Shule za Kidato cha Tano na Sita Rugufu Wasichana na Wavulana ambazo miundombinu yake ni chakavu na haitoshelezi?

Supplementary Question 2

MHE. SELEMANI M. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika wamejitahidi sana kwa kushirikiana na wananchi, wamejenga shule za sekondari zipatavyo sita, lakini kwa bahati mbaya sana bado baadhi ya majengo hayajapata kuezekwa. Kwa hiyo, tulikuwa tunauliza, Serikali ina mchango gani wa kuwasaidia hao wananchi ambao wametumia nguvu kubwa ili waweze kukamilisha hayo majengo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mwezi wa Pili mwanzoni tumepeleka fedha zaidi ya shilingi bilioni 29.9 kumalizia majengo kwa maana ya maboma katika Shule za Sekondari. Ninaamini Halmashauri karibu zote, kuna baadhi ya maeneo tu hatukupeleka, lakini maeneo mengi tumepeleka.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, ni kwamba vile vile mwaka huu wa fedha tuna miradi mingi na fedha ambazo zipo kwenda kumalizia maboma. Sasa kama kuna changamoto katika eneo hili kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge, tutazingatia maombi yake ili tuweze kumalizia majengo haya na watoto wetu waweze kukaa sehemu salama na waweze kupata elimu kama ambavyo ndiyo makusudio na matarajio ya Serikali ya Awamu ya Tano. Ahsante.

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASNA S. MWILIMA aliuliza:- Jiografia ya Halmashauri ya Uvinza ni mbaya na kusababisha wanafunzi wanaomaliza Kidato cha Nne kutoka mwambao wa Ziwa Tanganyika kusafiri zaidi ya kilometa 200 kufuata Shule za Kidato cha Tano na Sita zilizopo katika ukanda wa Reli:- (a) Je, kwa nini Serikali isianzishe Shule za Kidato cha Tano na Sita kwenye Kata nane za Ukanda wa Ziwa Tanganyika ili kuwapunguzia usumbufu wanafunzi hao? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati na kuongeza miundombinu katika Shule za Kidato cha Tano na Sita Rugufu Wasichana na Wavulana ambazo miundombinu yake ni chakavu na haitoshelezi?

Supplementary Question 3

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Hali ya Jimbo la Same Mashariki na Shule za High School haiko tofauti sana na ile ya Kigoma Kusini. Serikali ilishatupa hela ya kujenga bweni la wasichana ili Kidato cha Tano kianze na bweni hilo la kuchukua wanafunzi 80 limeisha. Sasa hivi wananchi wameshatengeneza matofali na wanaanza ujenzi wa kupandisha madarasa mawili ili Form Five ianze. Je, Serikali inaweza kutusaidia katika vile vifaa kama mabati na kumalizia umeme? Ahsante.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kama ambavyo umesema, tunaposema Serikali inamalizia maboma, tumepiga mahesabu maana yake ni pamoja na kumalizia majengo yenyewe, kuezeka kuweka madirisha na kuweka madawati ndani ya vyumba vile. Tumekadiria karibu shilingi milioni 12,500,000/= kila boma moja kukamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu tumeshapeleka fedha mwezi wa Pili kama nilivyosema, ambapo sasa tunarajia watakuwa wanaendelea kumaliza, kwenye bajeti hii pia kuna mpango wa kupeleka fedha za kumalizia maboma ya Shule za Msingi na Sekondari. Kwa hiyo, nimtie moyo Mbunge kwamba tutapeleka fedha hizo. Hayo aliyozungumza ya umeme na miundombinu mingine itazingatiwa katika kurekebisha. Hiyo ni nchi nzima kwenye Majimbo yote. Ahsante.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. HASNA S. MWILIMA aliuliza:- Jiografia ya Halmashauri ya Uvinza ni mbaya na kusababisha wanafunzi wanaomaliza Kidato cha Nne kutoka mwambao wa Ziwa Tanganyika kusafiri zaidi ya kilometa 200 kufuata Shule za Kidato cha Tano na Sita zilizopo katika ukanda wa Reli:- (a) Je, kwa nini Serikali isianzishe Shule za Kidato cha Tano na Sita kwenye Kata nane za Ukanda wa Ziwa Tanganyika ili kuwapunguzia usumbufu wanafunzi hao? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati na kuongeza miundombinu katika Shule za Kidato cha Tano na Sita Rugufu Wasichana na Wavulana ambazo miundombinu yake ni chakavu na haitoshelezi?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Mara chache nimeuliza kwenye sehemu ya Walimu. Nnataka kuuliza, kwa nini kwenye Shule za Halmashauri na nje ya Halmashauri Walimu wanatengwa na wake zao wanapelekwa shule nyingine hata zaidi ya kilomita 100? Hamwoni hiyo itaathiri familia ile ya Walimu na kwamba ni hatari kwa watoto kupata mimba?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nia ya Serikali tungependa kila mtu akae na mwenza wake karibu, kwa maana kwamba mume akae na mke na mke akae na mume. Hayo ndiyo yalikuwa mapenzi na matarajio ya Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Waheshimiwa Wabunge wenyewe mmekuwa mkilalamika kwamba kuna maeneo mengine walimu hawapo kwa sababu wanahama sana; na sababu kubwa ni hiyo kwamba anamfuata mume wake au mke wake au sababu nyinginezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tulisema, jambo hili baada ya kupata malalamiko hata kutoka kwa wananchi na Wenyeviti wa Halmashauri, Madiwani, Wabunge na wananchi wengine, kwamba kuna upungufu na kwa hiyo, ikama hai-balance katika maeneo yetu. Serikali ikalichukua na kulifanyia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunatengeneza mfumo ambao kama Mwalimu anataka kuhama kutoka shule A kwenda shule B, pale anapotoka asilete shida, na hapo anapoenda asiende kujaza watu kuliko mahitaji yake. Mfumo huo unaikaribia mwisho. Ukikamilika, hii shida ya walimu kuhama na ku-balance haitakuwa shida, tutaimaliza hilo tatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, mfumo; hata Mbunge ukiomba, ukiwaambia mkoa mzima usambazaji ukoje, Halmashauri ikoje, hakutakuwa na shida. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira. Pia Walimu wanalalamika sana, kuna mambo mengi ya uhamisho. Tutayafanyia kazi yote na hii kero itaisha. Ahsante sana.