Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Othman Omar Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Gando

Primary Question

MHE. OTHMAN OMAR HAJI aliuliza:- Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACPHR) inatumia jengo la TANAPA lililopo Arusha kwa mkataba wa upangaji baina ya TANAPA na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ulioanza tarehe 1 Desemba, 2008 kwa kodi ya dola za Marekani 38,998.89 kwa mwezi:- Je, kati ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu ni nani mwenye jukumu la haki za binadamu na nani mwenye jukumu la kulipa kodi ya jengo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. OTHMAN OMAR HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, hadi natuma swali hili Mei 8, 2017, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ilikuwa inadaiwa na TANAPA zaidi ya shilingi bilioni 3 za Tanzania. Je, deni hili limeshalipwa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Wizara kupitia Shirika lake la AICC inamiliki majengo ya kutosha pale Mjini Arusha ambapo ingetumia majengo yale ingewezesha mahakama hii kufanya shughuli zake kwa ufanisi mkubwa sana. Je, Mheshimiwa Waziri haoni upo umuhimu kuhamisha mahakama hii huko inakokodi na kuipeleka katika majengo haya ya AICC ili kuokoa matumizi yasiyokuwa ya lazima?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Othman Haji, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba TANAPA inadai fedha ya pango kwa ajili ya ofisi za Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu lakini taratibu zinaendelea ili ziweze kulipwa. Hata hivyo, naomba nimueleweshe Mheshimiwa Mbunge kwamba siyo mahakama ndiyo inadai Serikali bali ni Serikali na Serikali. Kwa hiyo, ni suala la kawaida, pesa hiyo italipwa muda ukifika na kama nilivyosema mchakato unaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na swali lake la pili kwamba kwa nini majengo ya AICC yasitumike kama ofisi za mahakama hiyo. Naomba nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari Serikali imetafuta hekari 20 Arusha kwa ajili ya kujenga ofisi za mahakama hiyo na taratibu za ujenzi zimefika mbali sana. Kwa hiyo, tunategemea baada ya muda mfupi ofisi hizo zitajengwa na hakutakuwa na haja ya kwenda kubanana kwenye Ofisi ya AICC. Hata kama mahakama hiyo ingeenda kwenye majengo ya AICC labda suala lile lile la kudaiwa na TANAPA lingeweza kujirudia. Kwa hiyo, tunachotaka kufanya ni kujenga ofisi ambazo zitatosha na changamoto hii haitatokea tena.

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. OTHMAN OMAR HAJI aliuliza:- Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACPHR) inatumia jengo la TANAPA lililopo Arusha kwa mkataba wa upangaji baina ya TANAPA na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ulioanza tarehe 1 Desemba, 2008 kwa kodi ya dola za Marekani 38,998.89 kwa mwezi:- Je, kati ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu ni nani mwenye jukumu la haki za binadamu na nani mwenye jukumu la kulipa kodi ya jengo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo hili la wanadiplomasia kutolipa kodi za pango halipo tu Arusha lakini pia lipo kwenye baadhi ya Balozi. Kwa mfano, Ubalozi wa Palestina nchini umepanga katika jengo linalomilikiwa na Halmashauri ya Temeke toka mwaka 2003 na mpaka leo hawajawahi kulipa kodi hata shilingi moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri imejaribu kufuata hatua mbalimbali za kudai ikiwa ni pamoja na kuripoti ofisi ya Wizara ya Mambo ya Nje lakini hakuna lolote lililofanyika. Tunahofia kuwaondoa kinguvu kwa sababu ya kulinda hiyo image ya ushirikiano wetu. Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari leo kuwapa notice Ubalozi wa Palestina kwamba ndani ya miezi mitatu kuanzia leo wahame katika jengo hilo huku Halmashauri ikiendelea na taratibu nyingine za kudai deni lao?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtolea, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kulitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba kuna utaratibu wa kidiplomasia wa kudaiana kati ya Serikali na Serikali na kwa vyovyote haiwezi ikawa kwa kupitia matamko ya Bungeni. Kwa hiyo, naomba tu nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba hili suala linafanyiwa kazi. Madeni yapo kila mahali, ni kawaida, awe na subira, nina hakika Serikali italifanyia kazi na changamoto hii itaondoka.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OTHMAN OMAR HAJI aliuliza:- Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACPHR) inatumia jengo la TANAPA lililopo Arusha kwa mkataba wa upangaji baina ya TANAPA na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ulioanza tarehe 1 Desemba, 2008 kwa kodi ya dola za Marekani 38,998.89 kwa mwezi:- Je, kati ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu ni nani mwenye jukumu la haki za binadamu na nani mwenye jukumu la kulipa kodi ya jengo hilo?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Wizara ya Mambo ya Nje imekuwa na madeni mengi hasa kwenye Balozi za nje ambazo Mabalozi wetu wanaishi na ni tabia ambayo inatuletea image mbaya kama taifa. Je, ni lini Serikali italipa hayo madeni ya pango za nyumba za Mabalozi wetu katika nchi mbalimbali za dunia hii tuliyopo sasa?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwakagenda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Bunge hili katika bajeti zake za miaka ya hivi karibuni limekuwa likitenga fedha mara kwa mara kwa ajili ya kulipa madeni hayo. Kwa hiyo, naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni kweli madeni yapo na kila wakati madeni ni sehemu ya maisha lakini Serikali itaendelea kulipa kadiri uwezo unavyopatikana. Hata hivyo, mkakati mkubwa wa Serikali sasa ni kuzuia madeni mengine kutokea kwa kulipa madeni kwa wakati. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba suala hili litafanyiwa kazi.

Name

John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. OTHMAN OMAR HAJI aliuliza:- Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACPHR) inatumia jengo la TANAPA lililopo Arusha kwa mkataba wa upangaji baina ya TANAPA na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ulioanza tarehe 1 Desemba, 2008 kwa kodi ya dola za Marekani 38,998.89 kwa mwezi:- Je, kati ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu ni nani mwenye jukumu la haki za binadamu na nani mwenye jukumu la kulipa kodi ya jengo hilo?

Supplementary Question 4

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Katika swali hili Serikali imeeleza inalipa Dola za Marekani 38,000 kwa mwezi ambazo ukipiga kwa mwaka ni takribani shilingi bilioni 1 na Serikali imeanza kulipa kuanzia 2008, kwa hiyo, ni takribani shilingi bilioni 9 kama all facts are being equal zimelipwa. Wizara hii ina experience kwenye ujenzi wa hosteli za chuo kikuu pale walisema block moja iligharimu shilingi milioni 500, ukigawanya kwa wastani wa hizo shilingi bilioni 9 kwa kipindi hiki kungeweza kujengwa maghorofa kati ya 18 mpaka 20.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hali kama hii, ni kwa nini Serikali imeachia hali ikae muda mrefu na ni lini hasa ujenzi huu utafanyika ili pesa zisiendelee kutumika kwa kiwango kikubwa namna hii kwenye kulipa kodi?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba gharama hizo ni kubwa, hata hivyo, ujenzi wa majengo ya Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu ni suala la kimkataba na wala haliamuliwi na Serikali peke yake, inabidi kukaa kukubaliana, michoro. Kwa hiyo, ni suala ambalo sio sisi wenyewe, ingekuwa ni kawaida kwamba ni la kwetu tungeshajenga lakini kama nilivyoliarifu Bunge lako Tukufu, tayari hatua za ujenzi zimefika mbali. Tumeshapata eka 20, michoro tayari, kwa hiyo muda wowote jengo hilo litajengwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba avute subira sanasana ucheleweshwaji umetokea kwa sababu majadiliano yanaendelea kuhusu namna gani jengo hilo lijengwe kwa sababu sio letu peke yetu lazima tuongee na Mahakama ya Afrika pamoja na Umoja wa Afrika.