Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Peter Ambrose Lijualikali

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. PETER A. LIJUALIKALI aliuliza:- Je, kwa nini Serikali isifute kodi kwenye vifaa vya kusambazia maji kutokana na matatizo ya maji tuliyonayo katika Taifa letu?

Supplementary Question 1

MHE. PETER A. P. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Spika, nafahamu Serikali imetoa msamaha wa kodi kwenye miradi yake lakini natamani nifahamu ni kwa nini sasa miradi ya watu binafsi wanaofanya kazi hii wenyewe hawapati misamaha? Maana yangu ni kwa nini kwenye vifaa vingine watu wanaofanya kazi hizi hawapati misamaha ya kodi ili kusaidia Serikali kupeleka huduma hii? Msamaha huu ungekuwa inclusive yaani usiwe tu kwa watu wanaofanya kazi Serikali peke yake. Kwa hiyo, napenda kufahamu ni kwa nini watu wengine pia hawapati misamaha huo?

Mheshimiwa Spika, pia naomba nifahamu kama Mheshimiwa Waziri atakubali kwenda nami sambamba kwenye Jimbo langu hasa kwenye Kata za Kipangalala na Kibaoni ambako kuna miradi mikubwa ya maji ya takribani shilingi milioni 600 lakini ni kama vile imesimama na fedha hizi ni kama zimelala. Kwa hiyo, naomba nifahamu commitment ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwa sababu anafahamu haya mambo nilishakaa naye ofisini kwake na kuzungumza kwa kirefu.

Kwa hiyo, naomba nijue kama yuko tayari twende Jimboni kwangu ili tukaone nini shida na tupate majibu kwenye mambo haya. Nashukuru sana.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake zuri lakini kubwa sisi kama Wizara ya Maji lengo letu na nia ya Mheshimiwa Rais ni kumtua mwana mama ndoo kichwani na kuhakikisha Watanzania waishio mijini na vijijini wanapata maji safi salama na yenye kuwatosheleza. Kwa mazingatio na ushauri wako niseme tu kwamba tumepokea ushauri na tutaufanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la commitment ya mimi kuongozana naye katika Jimbo lake, Mheshimiwa Lijualikali mimi sina kikwazo chochote, nipo tayari kuhakikisha tunakagua miradi ya maji. Ahsante sana.