Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbogwe?

Supplementary Question 1

MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Spika, ahsante pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize maswali madogo ya nyongeza. Swali la kwanza ni kwamba Wilaya ya Mbogwe ni Wilaya mpya na katika Mkoa wa Geita, ni Wilaya pekee ambayo kwa kweli ina watumishi wachache sana wa Idara ya Afya: Je, Serikali ina mpango gani wa kutuongezea watumishi hao?

Swali la pili ni kwamba Serikali imejitahidi kutupatia vituo viwili vya afya na huduma mojawapo ni ya mortuary; lakini kuna shida ya mortuary cabinets, yale mafriji ya kuhifadhia maiti hayajaletwa na watu MSD. Sasa Serikali ina mpango gani kupitia MSD kutuletea hiyo huduma mara moja? Ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, katika swali lake la kwanza Mheshimiwa Masele anaongelea upungufu wa watumishi wa Kada ya Afya katika Wilaya yake ambayo ni miongoni mwa Wilaya mpya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika na wewe umekuwa shuhuda kwamba wakati mwingi zinapoanzishwa Halmashauri mpya kumekuwa na nakutopata watumishi wa kutosha. Kwa hiyo, naomba kwanza niagize Ofisi ya RAS wahakikishe kwanza ndani ya Mkoa watazame ikama ilivyo ili katika maeneo ambayo yana upungufu mkubwa kama eneo la Mheshimiwa Mbunge waweze ku-balance.

Mheshimiwa Spika, nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba wakati nafasi nyingine zikitoka kwa ajili ya kuajiri, tutahakikisha kwamba tunazingatia maeneo yenye upungufu ikiwa ni pamoja na eneo lake kuwapeleka watumishi wale.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ni juu ya kupatikana kwa friji kwa ajili ya kutunza maiti. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni azima ya Serikali kuhakikisha maeneo yote ambayo mortuary zimejengwa, friji zinapelekwa. Naomba tuwasilaine na Mheshimiwa Mbunge baada ya kipindi cha maswali na majibu ili tujue MSD lini watapeleka hayo masanduku.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbogwe?

Supplementary Question 2

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niliulize swali dogo la nyongeza. Hospitali ya Nyamiaga ni Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Ngara ambayo ilipatiwa hadhi kutoka kituo cha afya mwaka 2013, lakini mpaka sasa hivi hakuna maboresho ya miundombinu katika hospitali hiyo. Kwa hiyo kuna upungufu wa jengo la utawala, jengo la upasuaji, jengo la X-Ray, mortuary na labor Ward:-

Ni lini Serikali itaweza kutenga fedha kwa ajili kuboresha hospitali hiyo ukizingatia kwamba hatuna hospitali ya Wilaya?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa
Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Gashaza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni ukweli usiopingika kwamba maeneo mengi ambayo vilikuwa aidha vituo vya afya au ilikuwa zahanati ikapandihswa hadhi; kwanza tumekuwa na changamoto ya eneo, hata pale ambapo tumepandisha hadhi kituo cha afya kuwa hospitali ya Wilaya inakuwa haina hadhi ya kulingana na hospitali ya Wilaya.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba Serikali katika utaratibu mziwa wa kuboresha na kujenga Hospitali za Wilaya zile za mwanzo zinaanza kuonekana kwamba zimeanza kuwa outdated. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa kadri ambavyo tumeanza na hosptali 67, zikaongezeka 27 kwa kadri bajeti itakavyoruhusu hakika na wao hatutawasahau ili wale na Hosptali ya Wilaya yenye hadhi ya kulingana na Hospitali za Wilaya za Halmashauri nyingine.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbogwe?

Supplementary Question 3

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa ujenzi wa Kituo cha Afya Mbori ambacho hata wewe unakifahamu, Waziri wa TAMISEMI anakifahamu, sasa ni zaidi ya miaka kumi kinajengwa kwa nguvu za wananchi na Halmashauri ambayo haina fedha; na kwa kuwa nimeomba shilingi milioni 500 TAMISEMI wasaidie kukamilisha jengo lile:-

Je, TAMISEMI au Serikali inasemaje kuhusu kukamilisha Kituo cha Afya Mbori?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, kama kuna Waheshimiwa Wabunge ambao wamekuwa wakiongelea kituo cha afya kwa kurudia mara nyingi ni pamoja na Mheshimiwa Lubeleje; na hivi karibuni alipata fursa ya kuonana na Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana na akamhakikishia.

Mheshimiwa Spika, hivi karibuni tumepata fedha kiasi, tumepeleka kwenye hospitali na vituo vya afya ikiwa ni pamoja na Kongwa shilingi milioni 400. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Lubeleje, ahadi ya Mheshimiwa Waziri hakika atatekeleza kama alivyomwahidi. Naomba avute subira fedha yoyote ikipatikana hatumsahau Mheshimiwa Lubeleje.