Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- Mapema mwaka 2016 Waziri wa Nishati alifanya uzinduzi wa Mradi wa Umeme wa REA na kuagiza Vijiji vya Sarakwa, Tingirima, Rakana, Nyang’aranga, Nyamakumbo, Saba–Osanza, Mmagunga, Nyabuzume, Bukama, Tiring’ati, Bigegu, Nyaburundu, Masaba, Nyansirori, Nyamuswa A, Saloka-Guta, Mahanga, Manchimweru, Nyangere, Makongoro A na B na Nyamuswa kupatiwa umeme:- (a) Je, ni lini kifanyike ili miradi ya vijiji 21 ikamilike kwa wakati kama Serikali ilivyoahidi? (b) Je, ni nani aliyepanga kijiji A kipate kilomita tatu, transfoma mbili au nguzo 20 na umeme upitie eneo bila kushirikisha vijiji na hata bila kujali wingi wa kaya?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Meshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza, lakini niipongeze Wizara ya Nishati, Waziri wake Mheshimiwa Dkt. Kalemani na Mheshimiwa Subira, Naibu Waziri na Watendaji wake wote kwa kasi ambayo wanaionesha sasa kwenye Jimbo la Bunda. Natambua kuna Vijiji vya Nyabuzume, Tiring’ati, Bigegu, Nyaburundu, Mihingo, Rakana, Manchimweru, Nyang’aranga, Sarakwa na Tingirima, wameweka nguzo za umeme. Swali langu la kwanza hapa, ni lini sasa umeme utawaka kwenye maeneo haya kwa sababu ninapouliza swali hili sasa hivi hapa kuna akinamama zaidi ya 100 wanataka kusikiliza wamechoka na mambo ya vibatari kwenye maeneo yao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kuna maeneo ya Nyamatutu, Saba-Osanza, Mmagunga, Nyamakumbo, Sanzate, Nyansirori, Saloka-Guta, Nyamuswa A. Mheshimiwa Waziri rafiki yangu Dkt. Kalemani, kutoa transfoma nane kwenye maeneo ya taasisi kama vituo vya afya, shule za msingi, sekondari survey ilishafanywa na Serikali imetumia hela pale tangu 2016, ni lini sasa zile Taasisi zitapata umeme, kuweka transfoma nane shida iko wapi?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri alivyojibu majibu mazuri kwenye swali la Mheshimiwa Mbunge Getere.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge Getere anavyofuatilia masuala ya umeme katika Jimbo la Bunda Vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa napenda nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Getere, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza amependa kujua ni lini sasa vijiji vya Bunda ambavyo vinapelekewa umeme vitapata umeme. Kwanza nianze kusema hapa tunapoongea wakandarasi wako site na hivi sasa vijiji takriban 11 wameshavifanyia kazi. Leo na jana wakandarasi wako site, Derm Electric, wanafanya kazi katika Vijiji vya Mwanchimweru, Nyanharanga, Mahanga, Lakani pamoja na Tingirima ambapo vyote watawasha umeme katika wiki inayokuja. Katika Jimbo la Mheshimiwa Getere vimebaki vijiji vitano tu vya Sarakwa, Nyabuzume, Tingirigi pamoja na vijiji anavyovitaja vitatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala lake la pili ambalo ni la msingi kabisa, maeneo ya vijiji takribani 11 yana umeme na vitongoji vyake vina umeme shida ni shule za sekondari na zahanati ambazo hazijapata umeme. Nimpe taarifa Mheshimiwa Mbunge wakandarasi wameshaweka design, tuna mpango wa kuongeza umeme katika vitongoji unaoanza mwezi ujao. Kwa hiyo, maeneo yote ya Shule za Msingi za Nyamatutu, Saba Osama, Nyamakumbu, Maguga, Salokikwa pamoja na Musa na Makongolai A&B vitapelekewa umeme pamoja na taasisi zake.

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- Mapema mwaka 2016 Waziri wa Nishati alifanya uzinduzi wa Mradi wa Umeme wa REA na kuagiza Vijiji vya Sarakwa, Tingirima, Rakana, Nyang’aranga, Nyamakumbo, Saba–Osanza, Mmagunga, Nyabuzume, Bukama, Tiring’ati, Bigegu, Nyaburundu, Masaba, Nyansirori, Nyamuswa A, Saloka-Guta, Mahanga, Manchimweru, Nyangere, Makongoro A na B na Nyamuswa kupatiwa umeme:- (a) Je, ni lini kifanyike ili miradi ya vijiji 21 ikamilike kwa wakati kama Serikali ilivyoahidi? (b) Je, ni nani aliyepanga kijiji A kipate kilomita tatu, transfoma mbili au nguzo 20 na umeme upitie eneo bila kushirikisha vijiji na hata bila kujali wingi wa kaya?

Supplementary Question 2

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza, nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri aliyoyatoa kwa Mheshimiwa Getere. Namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa sababu hata wapiga kura wa Mheshimiwa Getere wako hapa ndani leo wamesikia na wanausubiri huo umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia swali hilihilo niulize kwa Mkoa mzima wa Mara, kuna Wilaya ya Rorya ambako mimi nimezaliwa, Wilaya ya Msoma Vijijini pia nilikozaliwa lakini pia kuna shangazi zangu wa Wilaya ya Serengeti na Tarime. Swali langu sasa, ni lini Serikali itapeleka huduma za umeme wa REA katika huduma za shule, zahanati, vituo vya afya kwa maeneo mengine yote yaliyobaki ya Mkoa wa Mara?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nijibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Agness, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Mara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nampongeza Mheshimiwa Mbunge Agness anavyofuatilia masuala haya ya umeme katika taasisi za umma. Napenda kusema tu kwamba mkandarasi katika Mkoa wa Mara atapeleka umeme kwenye vijiji vyote 172 vya Mkoa wa Mara pamoja na vitongoji 318 na yuko site.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini cha msingi kabisa, katika Wilaya ya Rorya ameshapeleka umeme kwenye vijiji 17 na shule za sekondari 18. Katika Wilaya ya Msoma Vijijini, mkandarasi anaendelea na kazi. Niseme kwamba vijiji vyote vitapelekewa umeme kuanzia sasa na kuendelea na mwezi Juni, 2020 miradi yote itakamilika.

Name

Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- Mapema mwaka 2016 Waziri wa Nishati alifanya uzinduzi wa Mradi wa Umeme wa REA na kuagiza Vijiji vya Sarakwa, Tingirima, Rakana, Nyang’aranga, Nyamakumbo, Saba–Osanza, Mmagunga, Nyabuzume, Bukama, Tiring’ati, Bigegu, Nyaburundu, Masaba, Nyansirori, Nyamuswa A, Saloka-Guta, Mahanga, Manchimweru, Nyangere, Makongoro A na B na Nyamuswa kupatiwa umeme:- (a) Je, ni lini kifanyike ili miradi ya vijiji 21 ikamilike kwa wakati kama Serikali ilivyoahidi? (b) Je, ni nani aliyepanga kijiji A kipate kilomita tatu, transfoma mbili au nguzo 20 na umeme upitie eneo bila kushirikisha vijiji na hata bila kujali wingi wa kaya?

Supplementary Question 3

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kupata nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lililoko Bunda ni la Mkoa mzima. Tumeona ufunguzi wa REA Phase II na Phase III umefanyika lakini kilichofanywa na wakandarasi ni kwenda kumwaga nguzo tu. Naomba kujua ni lini vijiji vya Kabulabula, Bugoji, Mhoji, Komoge na Kabage vitapata umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nijibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Sokombi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Kijiji cha Kabulabula kimeshapelekewa umeme isipokuwa vitongoji viwili kati ya vitongoji vinne. Niseme tu mahali ambapo wamemwaga nguzo siyo kwamba wamemwaga bali wameshakamilisha survey. Kijiji cha Kabulabula vitongoji vitatu vilivyobaki vitaanza kupelekewa umeme kuanzia mwezi Julai, 2019.