Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE (K.n.y. MHE. ZUBEDA H. SAKURU) aliuliza:- Hospitali na Vituo vya Afya vinatakiwa kukidhi viwango vya utoaji huduma kwa wagonjwa; lakini hospitali na Vituo vya Afya vingi havina viwango vya utoaji huduma. Je, Serikali ina mkakati gani mahsusi wa kuhakikisha Vituo vya Afya na hospitali vinakidhi viwango vya utoaji huduma?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, pamoja na ujenzi wa hospitali na Vituo vya Afya lakini bado kuna upungufu mkubwa sana wa watumishi wa afya hapa nchini. Je, Serikali haioni sasa huu ni muda muafaka wakati wanajenga Vituo vya Afya, lakini pia watoe ajira mpya kwa watumishi wa afya na pia walipe stahiki za wale watumishi wa afya wengine ili kuongeza morali na tija?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Jimbo la Mikumi lina jiografia mbaya sana na tuna Vituo vinne vya Afya vya Kidodi, Mikumi, Ulaya na Malolo ambacho wananchi wanajenga kwa nguvu zao wenyewe. Je, Serikali haioni sasa huu ni muda muafaka ili kuokoa Watanzania wa Mikumi tuweze kupatiwa magari ya wagonjwa kusaidia akina mama na watoto ambao wanapata matatizo katika maeneo hayo? Ahsante sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mheshimiwa Haule katika ziara kadhaa nilizofanya tulikuwa pamoja kule Jimboni kwake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni mpango wa Serikali, kama tunavyofahamu kwamba Mheshimiwa Rais na Serikali kwa ujumla imefanya mchakato wa ujenzi wa Vituo vya Afya 352hivi karibuni, Hospitali zetu za Wilaya 67 na mwaka huu tumeongeza 27 mpya, jambo hili linataka human resources kwa ajili ya kuweza kufanya kazi vizuri.

Kwa hiyo, ni mpango wa Serikali tutaangalia nini kifanyike. Licha kwamba mwanzo tuliajiri takribani watumishi wasiopungua 11,000; wale wa Serikali za Mitaa na Serikali Kuu lakini tutaangalia nini kifanyike kwa ajili ya kuongeza idadi ya watumishi katika vituo vyetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Mikumi suala zima la kuongeza miundombinu, nikushukuru, lakini Mbunge hapa kwanza unge-appreciate kazi kubwa iliyofanyika pale Mikumi, nadhani na wewe unakumbuka, ilikuwa ni ya kusuasua sana. Serikali tumeenda tumefanya kazi kubwa na hivi sasa imekuwa ni miongoni mwa Kituo bora sana cha Afya katika eneo lile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo tutaendelea kuangalia nini kifanyike kwa maeneo mbalimbali yenye changamoto kubwa, siyo Mikumi peke yake. Ni mpango wa Serikali kuangalia nchi nzima tunahakikisha wananchi wanaopata shida ya huduma ya afya sasa inakuwa ni historia. Ahsante sana.

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE (K.n.y. MHE. ZUBEDA H. SAKURU) aliuliza:- Hospitali na Vituo vya Afya vinatakiwa kukidhi viwango vya utoaji huduma kwa wagonjwa; lakini hospitali na Vituo vya Afya vingi havina viwango vya utoaji huduma. Je, Serikali ina mkakati gani mahsusi wa kuhakikisha Vituo vya Afya na hospitali vinakidhi viwango vya utoaji huduma?

Supplementary Question 2

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Lupembe katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ina vituo vinne lakini haijawahi kupata fedha kwa ajili ya uboreshaji wa vituo hivi na jiografia ya Jimbo lile ni mbaya sana. Tunashuruku kwamba mmetupatia Hospitali ya Wilaya lakini wananchi wanataka kujua ni lini Halmashauri ya Wilaya ya Njombe itapata fedha kwa ajili ya uboreshaji wa Vituo vya Afya vya Kichiwa, Sovi, Lupembe na Ikuna ambacho ujenzi wake karibia unakamilika? Naomba tupate majibu.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, binafsi naomba nimpongeza Mheshimiwa Hongoli kwa vile nafahamu wazi na yeye anafahamu mpaka jana takribani saa tatu na nusu usiku tulikuwa tunaongea naye kuhusu suala zima la sekta ya afya. Hii inaonyesha jinsi gani anajali wananchi wake na kufuatilia masuala ya afya. Ndiyo maana katika awamu ya kwanza tulimpatia Hospitali ya Wilaya na najua katika mpango wa bajeti ya mwaka huu tumemtengea Kituo kimoja cha Afya lakini bado hali siyo nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana nilikuhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba ni commitment yetu sisi Serikali na Mungu akijalia huenda kabla hata mwezi Julai haujafika, tutafanya kila liwezekanalo tukupatie Kituo kingine cha Afya bora zaidi ili wananchi wa Jimbo lile la Njombe DC waweze kupata huduma vizuri.

Name

Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE (K.n.y. MHE. ZUBEDA H. SAKURU) aliuliza:- Hospitali na Vituo vya Afya vinatakiwa kukidhi viwango vya utoaji huduma kwa wagonjwa; lakini hospitali na Vituo vya Afya vingi havina viwango vya utoaji huduma. Je, Serikali ina mkakati gani mahsusi wa kuhakikisha Vituo vya Afya na hospitali vinakidhi viwango vya utoaji huduma?

Supplementary Question 3

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo hili linafanana sana na Hospitali ya Frelimo Mjini Iringa. Hospitali yetu ya Frelimo inatoa huduma kubwa kwa maeneo mengi ukizingatia kwamba Iringa Mjini ndiyo kitovu na maeneo mbalimbali wanakuja kutibiwa pale. Katika mpango wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa mmekuwa mkitoa pesa za vifaa kwenye hospitali mbalimbali lakini cha kushangaza mwaka jana kwenye Hospitali yetu ya Frelimo hamkutoa mkiona kwamba ni Kituo cha Afya wakati ni hospitali. Nilitaka nipate majibu ni kwa nini hamkutoa vile vifaa kama hospitali zingine kwenye Hospitali yetu ya Frelimo ambayo kwa kweli inasaidia wagonjwa wengi sana katika Manispaa yetu ya Iringa Mjini?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Mheshimiwa Msigwa na Mheshimiwa Msigwa anafahamu nimefika pale Flerimo mara kadhaa na nakumbuka tulikuwa na Mbunge pacha wako Mheshimiwa mama Kabati. Hospitali ile inachukua watu wengi sana na mimi nimefika pale nimeona. Naomba niwapongeze Madaktari wa pale wanafanya kazi vizuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni commitment yetu sisi Serikali, naomba nikuhakikishie kwamba eneo lile tutaenda kuliboresha zaidi. Nilivyofika pale nimeona kuna kila sababu ya kufanya maboresha na rasilimali ni chache lakini lazima tutazigawanya. Kwa hiyo, ni mpango wa Serikali tutafanya kila liwezekanalo ili wananchi wa Iringa waweze kupata huduma vizuri katika Hospitali ya Frelimo.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE (K.n.y. MHE. ZUBEDA H. SAKURU) aliuliza:- Hospitali na Vituo vya Afya vinatakiwa kukidhi viwango vya utoaji huduma kwa wagonjwa; lakini hospitali na Vituo vya Afya vingi havina viwango vya utoaji huduma. Je, Serikali ina mkakati gani mahsusi wa kuhakikisha Vituo vya Afya na hospitali vinakidhi viwango vya utoaji huduma?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Kituo cha Afya cha Endasak na Basotu nilishaongea na Mheshimiwa Waziri atusaidie kuboresha ili vionekane kama ni vituo kwa sababu havina hata wodi na havijafikia hadhi ile lakini vinajulikana na wananchi kama ni Kituo cha Afya. Naomba nijue Mheshimiwa Waziri anasema nini kuhusu vituo hivi viwili vya Hanang?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumshukuru mama yangu Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu senior MP katika Bunge hili. Ni kweli niliongea na Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu na bahati nzuri nimefika kule Hanang, ni mpango wa Serikali naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu kama tulivyozungumza ni commitment ya sisi Serikali tunatafuta fedha tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo vituo vile viweze kupata huduma kama tunayokusudia, kwa hiyo, hilo ondoa hofu Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu.