Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 22 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 177 2019-05-07

Name

Zubeda Hassan Sakuru

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE (K.n.y. MHE. ZUBEDA H. SAKURU) aliuliza:-

Hospitali na Vituo vya Afya vinatakiwa kukidhi viwango vya utoaji huduma kwa wagonjwa; lakini hospitali na Vituo vya Afya vingi havina viwango vya utoaji huduma.

Je, Serikali ina mkakati gani mahsusi wa kuhakikisha Vituo vya Afya na hospitali vinakidhi viwango vya utoaji huduma?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zubeda Hassan Sakuru, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuimarisha utoaji wa huduma za afya kwenye Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwenye maeneo mbalimbali ya vituo vya kutolea huduma za afya ili kukidhi viwango vya kutolea huduma za afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuboresha viwango vya utoaji huduma za afya nchini, katika mwaka wa fedha 2017/ 2018 na 2018/2019, Serikali imetoa kiasi cha shilingi bilioni 285.17 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali za Halmashauri 67, ujenzi na ukarabati wa Hospitali za Wilaya tisa (9), Vituo vya Afya 304 na Zahanati 39. Vilevile, Serikali imejenga na kukarabati nyumba za watumishi wa afya nchini 301. Aidha, kwa mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali imetenga shilingi bilioni 23.9 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali za Halmashauri mpya 27 na ujenzi na ukarabati wa Vituo vya Afya 52.


Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2017/2018 na 2018/2019, Serikali imeajiri jumla ya watumishi 8,444 wa kada mbalimbali za afya kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya afya, kuajiri wataalamu, kununua dawa, vitendanishi na vifaa tiba ili kuhakikisha vituo vya kutolea huduma vinakidhi viwango vinavyohitajika.