Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:- Mgogoro wa mipaka kati ya Kijiji cha Kikulyungu na Hifadhi ya Selous ni wa muda mrefu:- Je, Serikali itamaliza lini mgogoro huo?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante wa majibu ya Serikali athari kubwa ya mgogoro huo ni kijiji cha Kikulyungu kuondolewa kwenye WMA ya Jumuiya ya Magingo na kwa majibu haya inaonekana mgogoro huu umefika mwisho.

(i) Sasa ni lini Serikali itakuja Kikulyungu kuwapa wananchi matokeo ya maamuzi haya na kuwapa kibali au kuwapa kibali au kuwapa hati ili waweze kurudishwa kwenye Jumuiya ya Magingo?

(ii) Na kwa sababu sisi tunaoishi kwenye maeneo ya hifadhi kumekuwa na uharibufu mkubwa sana wa mazao unaotokana na wananyama waharibifu kama tembo, nguruwe, na wananyama wengine waharibu. Na Serikali imekuwa ikitoa kitu kinachoitwa kifuta machozi sasa ni lini Serikali itakuja na marekebisho ya sheria ili badala ya kutoa kifuta machozi iwe wananchi wao wanapata fidia inayotokana na uharibifu wa mazoa ya mashambani?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zuberi Mohamedi Kuchauka Mbunge wa Jimbo la Liwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimuahidi kwa kuwa taarifa ya kamati ambayo ilienda kuhakiki mipaka imekamilika na ipo mezani kwangu, kwamba baada ya Bunge hili la Bajeti kuisha aidha nitaenda mwenyewe ama nitamtuma Mheshimiwa Naibu Waziri kwenda kuzungumza na wananchi wa kijiji cha Kikulyungu kwenda kuwapa matokeo ya taarifa ya kazi iliyofanywa na kamati iliyokuwa chini ya uzongozi wa Wizara ya Ardhi ambayo ili hakiki mpaka ule kwa hivyo ni lini baada ya Bunge la Bajeti kumalizika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili kuhusu Serikali kuachana na kulipa kifuata machozi ama pia na kifuta chasho kutokana na uharibifu wa unaofanywa na wanyama wakali na waharibifu badala yake tulipe fidia. Ngumu kwa Serikali kuji-commit kwamba itaanza kulipa fidia ya uhalibifu unaofanywa na wanyama wakali na wanyama waharibifu na sababu zipo wazi. Kwa mfano mnyama amesababisha umauti wa raia wa mwananchi huwezi kusema utalipa fidia ya mnyama kuua mwanadamu kwa sababu thamani ya mwanadamu haiweezi kulinganishwa na kitu chochote kile.

Kwa hivyo, hiyo ni bahati mbaya ambayo inakuwa imetokea tunachoweza kulipa pale ni kufuta machozi na sio fidia. Lakini thamani ya mazao vilevile ni ngumu kusema Serikali itaji- commit kulipa fidia balada ya kufuta jasho kwa sababu changamoto zilizopo ambazo zinahusiana na wanyama hawa kwenda kwenye maeneo ni nyingi wakati mwingine wananchi wanawafuata wanyama kwenye mapito yao ama kwenye mazalia yao ama maeneo ya mtawanyiko na wakati mwingine sisi viongozi tukiwemo Wabunge, madiwani tunahamasisha sana Serikali imege maeneo ya hifadhi ambayo kiuhasili ni lazima yatapitiwa na wanyama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, kusema Serikali itaji-commit kwa kweli kulipa fidia ni jambo gumu kwa sababu gharama itakuwa kubwa sana mwisho wa siku tutashindwa kutunza hizi maliasili ambazo sisi zote tunapaswa kuzilinda kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 27.

Kwa hivyo ninawaomba sana wa kwa Waheshimiwa Wabunge wote na wananchi wote watambue kwamba wanyamapori ni maliasili ya Taifa, ni utajiri, ni urithi wa Taifa letu na hatuwezi kwamwe kuacha kuilinda kwa ajili ya matumizi ya sasa na vizazi vijavyo.