Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 21 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 174 2019-05-06

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:-

Mgogoro wa mipaka kati ya Kijiji cha Kikulyungu na Hifadhi ya Selous ni wa muda mrefu:-

Je, Serikali itamaliza lini mgogoro huo?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Mohamedi Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuwa mgogoro wa mpaka kati cha kikulyungu na poro la Akiba Selous umekuwepo kwa muda mrefu. Chanzo cha mgogoro huo ni wananchi wa kijiji hicho kufutiwa kibali cha kuvua samaki katika bwawa la kihurumila ambalo limo ndani ya Pori la Akiba Selous baada ya wananchi wa kijiji hicho uanza kuvua kwa njia zisizo endelevu au haribifu ikiwemo kutumia sumu. Baada ya kufutiwa kibali wananchi wa Kikulyungu walianza kulalamika na kudai kuwa mpaka wa Selous na kijiji hicho upo mto Matandu jambo ambalo ni kinyume na Tangazo la Seriklai Na.475 la Mwaka 1974.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya uhakika wa mipaka imekamika na taarifa imewasilishwa Wizarani kwangu. Aidha, zoezi la kuhakika mipaka hiyo lilienda sambamba na uwekaji wa alama za kudumu baada ya maridhiano ya pande zote kwa kuzingatiwa tangazo la Serikali kuanzishwa kijiji cha Likulyungu, Tanganzo la Serikali kuanzishwa pori la Akiba la Selous GN. Na. 275 la 1974 na Tanganzo la Serikali la kuanzishwa pori tengefu Kihurumila Na.269 ambalo pia ni la mwaka 1974 lililopo kati ya kijiji cha Likulyungu na pori la Akiba Selous.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa uhakiki huo umefanywa na wataalam kutoka Wizara yenye dhamana ya ardhi na kushirikisha pande zote zilizohusika katika mgogoro huo, ni imani kuwa mgogoro huo umemalizika.