Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GIMBI D. MASABA aliuliza:- Serikali iliahidi kujenga Mradi mkubwa waMaji kutoka Ziwa Victoria kuanzia Nyashimo, Ngasamo, Dutwa, Bariadi, Itilima, Meatu na Maswa:- Je, ni lini mradi huo utaanza na kukamilika?

Supplementary Question 1

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja namajibu ya Serikali, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, Mradi wa Ziwa Victoria, ulikuwa na mabomba mawili makubwa, bomba la kwanza ni bomba la maji safi na salama nabomba la pili ni bomba la maji ambayo hayana dawa kwa matumizi ya mifugo na mengineyo. Sasa naomba kufahamu kama mkataba huu umezingatia ufanisi wa mradi huu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, tumekuwana miradi mingi ambayo tunayo katika bajeti ambayo sasa hivi inakamilika hususan Mradi wa Nyangokulwa, Mradi wa Nyakabindi, Mradi wa Sanungu na Mradi wa Mahina. Miradi hii bado haijatekelezeka na kwenye kitabu cha Waziri nimeona kama miradi 10 ambayo wametupa. Sasa nataka kufahamu, ni kwa nini Serikali inatupa miradi ambayo haitekelezeki?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote kwanza nataka nimpe taarifa Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wote wa Simiyu akiwemo Mtemi Chenge pamoja na Mheshimiwa Mbunge Mpina, kwamba leo ni siku muhimu sana kwa Wanasimiyu kwamba ule mradi ambao umeahidiwa na Serikali kwa muda mrefu sana ninavyozungumza Katibu Mkuu yuko Dar es Salaam anasaini financial agreementkwa ajili ya utekelezaji wa mradi mkubwa huu wa maji Simiyu.

Kwa hiyo, kikubwa hii ni Serikali ya awamu ya tano inapoahidi inatekeleza. Hata hivyo, kikubwa cha msingi kuhusu suala zima la utekelezaji wa mkataba, nataka nimakikishie, design au mkataba jinsi ulivyotuelekeza na sisi ndivyo tutakavyotekeleza mradi ule kama tulivyoelekezwa na mkataba.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili, kuhusu miradi ambayo tumeahidi kwa ajili ya utekelezaji, sisi kama Wizara ya Maji zipo changamoto, moja, kulikuwa na miradi ambayo ilikuwa inahitaji kulipwa certificate, tumeshapokea bilioni 44 zingine na moja ya watu ambao tumewalipa ni wakiwemo Wanasimiyu, lakini kikubwa tumewatengea tena katika bajeti hii bilioni tano na milioni 950, yote katika kuhakikisha tunatatua matatizo ya maji.

Mheshimiwa Spika, nataka nimwagize Mhandisi wa Maji wa Mkoa wa Simiyu, ahakikishe fedha hizi zinatumika katika kuhakikisha wanakamilisha miradi ya maji na wananchi wa Simiyu waweze kupate maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.

SPIKA: Kabla hujaoondoka Naibu Waziri, kabla hujaondoka hapo, kidogo tu, rudi hapo. Kuna ufafanuzi wa Itilima, itaguswa na Kisesa kwa Mheshimiwa Mpina.

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, bila shaka.