Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 20 Water and Irrigation Wizara ya Maji 162 2019-05-03

Name

Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GIMBI D. MASABA aliuliza:-

Serikali iliahidi kujenga Mradi mkubwa waMaji kutoka Ziwa Victoria kuanzia Nyashimo, Ngasamo, Dutwa, Bariadi, Itilima, Meatu na Maswa:-

Je, ni lini mradi huo utaanza na kukamilika?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika,kwa niaba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Gimbi Dotto Masaba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali itatekeleza mradi wa kutoa maji kutoka Ziwa Victoria kupeleka katika Miji ya Nyashimo (Busega), Bariadi na Langangabilili, Maswa na Mwanhuzi. Mtaalam Mshauri anaendelea na kazi ya usanifu na uandaaji wa makabrasha ya zabuni na mradi huu utatekelezwa katika awamu mbili.

Mheshimiwa Spika, awamu ya kwanza itahusisha Miji ya Nyashimo (Busega), Bariadi na Lagangabilili pamoja na vijiji vipatavyo 170 vilivyo ndani ya kilomita 12 kutoka bomba kuu kila upande. Awamu hii itagharimu Euro milioni 105 ambapo kati ya hizo Serikali ya Ujerumani kupitia benki yake KfW itatoa Euro milioni 25naGreen Climate Fund(GCF) Euro milioni 80. Ujenzi waawamu ya kwanza unatarajiwa kuanza mwezi Oktoba, 2019 na kukamilika mwaka 2022.

Mheshimiwa Spika, awamu ya pili ya mradi itahusisha Miji ya Mwanhuzi, Maswa na vijiji vipatavyo 83. Kwa sasa Serikali inaendelea na majadiliano na Green Climate Fund ili kupata fedha kiasi cha Euro milioni 208 zitakazotumika kugharimia utekelezaji wa awamu hii. Ujenzi wa awamu ya pili utaanza baada ya kukamilisha taratibu za upatikanaji wa fedha hizo. Kukamilika kwaawamu zote kutawanufaisha wananchi wapatao 834,204.