Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Je, ni lini barabara ya Segerea – Sheli kwenda Kipawa kupitia Seminari itaanza kutengenezwa?

Supplementary Question 1

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa ni zaidi ya miaka 15 wananchi wa Segerea kupitia hiyo barabara ya Majumba Sita, Sitakishari wamekuwa wanapitia hiyo adha ya kukosa daraja, lakini ni kiungo kikubwa cha Gereza la Segerea, Seminari na sekondari mbalimbali: Je, Serikali haioni ni wakati sahihi wa kutengeneza hilo daraja ili kuondokana na hiyo adha?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Changamoto ya madaraja katika kata mbalimbali za Jimbo la Segerea ni kubwa, nikianzia na Kata ya Tabata, Segerea, Kimanga na nyingine: Je, nini kauli ya Serikali kuondoa hii adha ukizingatia kwamba hili eneo letu halina barabara nyingi za lami na halina mitaro ili kuondoa adha inayowakabili wananchi wetu? Nakushukuru.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, kumbukumbu zangu naamini ziko sahihi kwamba ni mara ya tatu Mheshimiwa Anatropia anaulizia barabara hii. Naomba nichukue fursa hii kumpongeza kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia kuhakikisha kwamba barabara hii inajengwa.

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu katika swali langu la msingi, changamoto ambayo tunakutana nayo kuhusiana na daraja hilo ni namna ambavyo mto unapanuka. Pia naomba yeye pamoja na Wabunge wote wanaotoka Dar es Salaam niwape maneno ya faraja kwamba ndani ya mwezi huu tumeweza kusaini kandarasi ya jumla ya shilingi bilioni 260 ambayo pia inashughulikia na adha ambayo inatokana na mafuriko mvua zinaponyesha na maeneo mengi ya Dar es Salaam yatakuwa yanafaidika katika hilo. Naamini hata hili suala la mto kupanuka baada ya kwamba kingo zimejengwa, adha itapungua.

Mheshimiwa Spika, namwomba Mheshimiwa Mbunge aendelee kuiamini Serikali maana yeye mwenyewe anashuhudia jitihada zinafanyika.

Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili, ameongelea madaraja mengi. Naamini katika package ya shilingi bilioni 260 nayo itakuwa imekuwa covered. Kama haitoshi, tumeweza kuweka taa 5,000 ndani ya Mji wa Dar es Salaam kwa ajili ya kuhakikisha wananchi wanaendelea kufaidi matunda ya chama chao.