Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 20 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 159 2019-05-03

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:-

Je, ni lini barabara ya Segerea – Sheli kwenda Kipawa kupitia Seminari itaanza kutengenezwa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Lwehikila Theonest, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Segerea – Sheli – Kipawa kupitia seminari yenye urefu wa kilometa 2.93 inasimamiwa na TARURA Manispaa ya Ilala, imesajiliwa kwa jina la Majumba Sita, Sitakishari. Katika mwaka wa fedha 2018/2019, barabara hiyo imechongwa kwa grader ili kuiwezesha kupitika. Hata hivyo, barabara hii inakatisha katika mto Msimbazi ambapo hakuna daraja. Daraja linalohitajika kujengwa ni kubwa na usanifu wake ulishafanyika.

Mheshimiwa Spika, changamoto iliyopo inatokana na mto kutanuka, hivyo inahitajika kufanyiwa study ya kina na mapitio ya usanifu wa awali ili kupata mahitaji halisi ya ujenzi wa daraja kutokana na changamoto hiyo. Mara baada ya kukamilika kwa mapitio ya usanifu na tathmini ya gharama Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kujenga daraja na kuifanyia matengenezo makubwa barabara hii. Katika mwaka wa fedha 2019/2020 Serikali kupitia TARURA imeitengea barabara hii jumla ya shilingi milioni 43 kwa ajili ya matengenezo ya maeneo korofi.