Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA aliuliza:- Tabora Manispaa kuna Zoo ya Wanyamapori ambayo ilijengwa muda mrefu na mpaka sasa wanyama wanapungua na kuifanya kukosa maana:- Je, Serikali iko tayari kupeleka wanyama hao katika zoo hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali ambayo yanaridhisha na yanakidhi swali langu, naomba niulize maswali mawili, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa mpaka sasa Bodi ya TAWA haijakabidhiwa rasmi uendeshaji wa shughuli hiyo ili waweze kutekeleza mipango waliyotarajia. Ni lini sasa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa itawakabidhi TAWA ili waweze kufanya kazi zao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari tuongozane siku ya Jumamosi akaone hali halisi ambayo naizungumzia? Ahsante?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mwanne Mchemba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kumpongeza kwa sababu amekuwa akifuatilia kwa karibu sana kuimarishwa kwa bustani hii kama chanzo cha mapato cha Mkoa wa Tabora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali lake la kwanza, naomba kumhakikishia kwamba taratibu za kukabidhiwa kwa TAWA zimekamilika na ndiyo maana mshauri mwelekezi amepatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, niko tayari kuongozana na Mheshimiwa Mbunge kwenda Tabora kwenda kuangalia bustani hiyo.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA aliuliza:- Tabora Manispaa kuna Zoo ya Wanyamapori ambayo ilijengwa muda mrefu na mpaka sasa wanyama wanapungua na kuifanya kukosa maana:- Je, Serikali iko tayari kupeleka wanyama hao katika zoo hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mpaka wa hifadhi wa Guruneti na Mto Rubana katika Vijiji vya Hunyali, Mariwanda, Kihumbu, Sarakwa na Mgeta lakini limekuwa tatizo la buffer zone inayotoka kwenye mto kuelekea vijijini na kuzuia watu kwenda kunywesha ng’ombe na malisho kwenye maeneo haya. Mheshimiwa Waziri alishatoa maelekezo ya mdomo lakini ni lini Serikali itapeleka sasa vigezo vya kisheria vya kuondoa eneo hilo?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Getere, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni kweli kwamba kutokana na matatizo ya mwingiliano wa shughuli za kibinadamu na wananchi na hifadhi pamekuwepo na migogoro mingi ambayo sasa hivi kama ambavyo nimekuwa nikijibu maswali yangu mengi Serikali inayafanyia kazi. Nimkumbushe tu Mheshimiwa Mbunge kwamba suala lake tumekwishalizungumza, tunasubiri maelekezo ya Kamati ambayo iliundwa na Mheshimiwa Rais itakapotoa maelekezo tutatengeneza buffer zone ambayo itaruhusu wafugaji kwenda kwenye mto kunywesha mifugo.

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA aliuliza:- Tabora Manispaa kuna Zoo ya Wanyamapori ambayo ilijengwa muda mrefu na mpaka sasa wanyama wanapungua na kuifanya kukosa maana:- Je, Serikali iko tayari kupeleka wanyama hao katika zoo hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mheshimiwa Naibu Waziri anajua kwamba kijiji cha Ruhoma, Jimbo la Mchinga kimevamiwa na tembo na wanakula mashamba ya wakulima. Nataka kujua hawa watu mnafanyaje kuwa-compensate gharama zile za mashamba yao kuliwa na tembo?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nikiri kwamba, tatizo la wanyama kuvamia mashamba na makazi ya watu limeongezeka. Limeongezeka baada ya usimamizi wa maeneo haya yenye wanyamapori pia, kuimarika na watu waliokuwa wanafanya mauwaji ya wanyama kwenye hifadhi zetu kupungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili limesababisha pia, uharibifu mkubwa wa mazao kwenye maeneo mbalimbali. Lakini utaratibu upo kwamba, pale ambapo wanyama hawa wanapovamia eneo na kuharibu mashamba ya wananchi utaratibu umewekwa kwamba, afisa wetu wa wanyamapori apewe taarifa. Tunamuelekeza anakwenda pale anafanya tathmini na tathmnini ile inapofika katika Wizara yetu tunaelekeza kulipa mara moja.