Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 18 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 152 2019-04-30

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA aliuliza:-

Tabora Manispaa kuna Zoo ya Wanyamapori ambayo ilijengwa muda mrefu na mpaka sasa wanyama wanapungua na kuifanya kukosa maana:-

Je, Serikali iko tayari kupeleka wanyama hao katika zoo hiyo?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwanne Ismail Mchemba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, bustani ya wanyamapori ya Tabora ina ukubwa wa ekari 35.67 ambapo ekari 28.15 ni eneo la wanyamapori na ekari 7.52 ni eneo la makazi. Bustani hii ilianzishwa na Idara ya Wanyamapori mwaka 1967 ikiwa na aina mbalimbali za wanyamapori wakiwemo chui, simba, duma, fisi, pundamilia nyumbu, swala na ngiri. Kwa sasa, bustani hiyo ina jumla ya wanyamapori 256 wa aina tofauti 16.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 1972 bustani hii ilikabidhiwa kwa Mkoa wa Tabora ili kuisimamia kwa ukaribu. Mwaka 2001, Ofisi ya Mkoa wa Tabora ilikabidhi shughuli za usimamizi wa bustani hii kwa Manispaa ya Tabora. Manispaa ya Tabora iliisimamia hadi mwaka 2012 ilipoirejesha kwa Idara ya Wanyamapori kutokana na kuongezeka kwa gharama za uendeshaji. Katika Idara ya Wanyamapori, bustani hii ilisimamiwa na Mfuko wa Wanyamapori Tanzania (Tanzania Wildlife Protection Fund). Mwaka 2018 bustani hii ilihamishiwa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori-TAWA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuongeza tija katika bustani ya wanyamapori, TAWA inaandaa mkakati wa kusimamia bustani ya wanyamapori zilizopo chini yake ikiwemo hii ya Tabora. Mkataba kati ya TAWA na mtaalam mwelekezi wa kuandaa mkakati huo umeshasainiwa ambapo mtaalamu huyo ataanza kazi hivi karibuni. Mkakati utakapokamilika utaainisha aina na idadi ya wanyama watakaowekwa katika bustani, aina ya huduma zitakazotolewa kwa wageni na kiwango cha tozo.