Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Machano Othman Said

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. MACHANO OTHMAN SAID (K.n.y. MHE. BAGWANJI MAGANLAL MEISURIA) aliuliza:- Mara nyingi wakati wa chaguzi mbalimbali Zanzibar kunatokea hali ya fujo na ukosefu wa amani na kusababisha wananchi kukosa amani na wakati mwingine kutoshiriki katika chaguzi husika:- Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Zanzibar juu ya suala hilo?

Supplementary Question 1

MHE. MACHANO OTHMAN SAID: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa matatizo makubwa ya Askari Polisi wakati wa uchaguzi ni uchache wao, je, Wizara iko tayari kushirikiana na vikosi vya SMZ kuongeza idadi ya Askari wakati wa uchaguzi huo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa imedhihirika kwamba kufanya uchaguzi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ule wa Zanzibar kwa siku moja unaleta matatizo zaidi. Je, Serikali iko tayari kutenganisha chaguzi hizi na kufanywa siku mbili tofauti?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Machano Othman Said, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza anauliza kama tuko tayari na ndivyo ambavyo inatokea kwamba vyombo hivi vinafanya kazi kwa ushirikiano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na swali lake la mabadiliko ya uchaguzi, nadhani hili suala linazungumzika na ni hoja ya msingi. Kwa hiyo, tunaichukua tuone kipi kinaweza kufanyika kwa kutilia maanani maoni yake.

Name

Saada Salum Mkuya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Welezo

Primary Question

MHE. MACHANO OTHMAN SAID (K.n.y. MHE. BAGWANJI MAGANLAL MEISURIA) aliuliza:- Mara nyingi wakati wa chaguzi mbalimbali Zanzibar kunatokea hali ya fujo na ukosefu wa amani na kusababisha wananchi kukosa amani na wakati mwingine kutoshiriki katika chaguzi husika:- Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Zanzibar juu ya suala hilo?

Supplementary Question 2

MHE. SAADA MKUYA SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mheshimiwa Waziri ameelezea jinsi gani vikosi vyetu vitashiriki katika kuhakikisha kwamba amani inakuwepo wakati wa uchaguzi. Changamoto inayoonekana ni kwamba kunakuwa na uchache wa muda wa kutoa elimu ya uchaguzi (voters education). Je, ni kwa kiasi gani wamejitayarisha kushirikiana na Tume ya Uchaguzi kuona kwamba hiyo voters education inatolewa kipindi kirefu zaidi kabla ya uchaguzi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Saada Mkuya Salum, Mbunge Welezo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie kwamba wakati wowote tutakuwa tayari kushirikiana na Tume za Uchaguzi pale ambapo watapanga ratiba zao vizuri. Naamini kabisa Tume hizi zimekuwa zikijifunza kulingana na changamoto zilizopita. Kwa hiyo, kama kulikuwa na mapungufu ya muda watarekebisha utaratibu huo na sisi tutakuwa tayari kushirikiana nao pale ambapo watapanga ratiba hizo.

Name

Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Primary Question

MHE. MACHANO OTHMAN SAID (K.n.y. MHE. BAGWANJI MAGANLAL MEISURIA) aliuliza:- Mara nyingi wakati wa chaguzi mbalimbali Zanzibar kunatokea hali ya fujo na ukosefu wa amani na kusababisha wananchi kukosa amani na wakati mwingine kutoshiriki katika chaguzi husika:- Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Zanzibar juu ya suala hilo?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana kabisa na hoja ya Mheshimiwa Bagwanji kwamba wakati wa uchaguzi kunakuwa na fujo nyingi Zanzibar. Ni kweli vilevile kwamba wakati huo kunakuwa kama uwanja wa vita Zanzibar; vifaru, magari ya deraya na vitendo vya kiharamia vingi vinafanywa na vikosi vya SMZ. Je, ni lini Serikali ya Muungano itaacha kutaka interest za matokeo ya Zanzibar kwa kuingilia kwa njia mbalimbali na badala yake waaachie mfumo wa demokrasia ufanye kazi na mshindi apewe ushindi wake?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Ally Saleh, Mbunge Malindi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza si sahihi kwamba Serikali imekuwa ikiingilia chaguzi. Hata hivyo, kuhusiana na hoja yake ya ulinzi kuimarika nyakati za uchaguzi Zanzibar hii inatokana na vitendo vya kiharamia ambavyo vimekuwa vikifanywa mara nyingi na hasa na vyama na upinzani. Tumeshuhudia katika uchaguzi mbalimbali hususani Chama Kikuu cha Upinzani Zanzibar wamekuwa wanaongoza katika ukiukwaji wa taratibu za sheria za uchaguzi.

WABUNGE FULANI: Aaaaa.

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumza hivyo kwa uthibitisho nikiwa nasimamia Jeshi la Polisi, nakijua nachokizungumza kwamba nathibisha kwamba Chama Kikuu cha Upinzani Zanzibar kimekuwa kikikiuka taratibu za uchaguzi na kufanya vitendo ambavyo ni kinyume na sheria. Kwa hiyo, Jeshi la Polisi ama vyombo vya dola vitakuwa imara zaidi kudhibiti uvunjifu wa sheria ambao unafanywa na vyama hivyo katika chaguzi mbalimbali.