Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 18 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 151 2019-04-30

Name

Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. MACHANO OTHMAN SAID (K.n.y. MHE. BAGWANJI MAGANLAL MEISURIA) aliuliza:-

Mara nyingi wakati wa chaguzi mbalimbali Zanzibar kunatokea hali ya fujo na ukosefu wa amani na kusababisha wananchi kukosa amani na wakati mwingine kutoshiriki katika chaguzi husika:-

Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Zanzibar juu ya suala hilo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maganlal Meisuria, Mbunge wa Chwaka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuwa nyakati za uchaguzi hukumbwa na vitendo vya uvunjifu wa amani hususani wakati wa kampeni na wakati wa kupiga kura. Hata hivyo, Serikali kupitia Jeshi la Polisi huchukua hatua mbalimbali kudhibiti vitendo hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, napenda kuwafahamisha wananchi kuwa ni jukumu la Serikali kuhakikisha amani na utulivu vinatamalaki nchini wakati wote bila kujali nyakati au majira mbalimbali katika mwaka. Jeshi la Polisi linaendelea kutoa mafunzo mbalimbali kwa Askari ya ukakamavu, upelelezi na kuongeza vitendea kazi ili kuwajengea uwezo na weledi wa kuzuia na kukabiliana na vitendo vya uvunjifu wa amani vinavyojitokeza hususani wakati wa uchaguzi.