Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ajali Rashid Akibar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. AJALI R. AKBAR aliuliza:- Takwimu zilizopo zinaonesha kuwa gesi kutoka Mtwara na Songosongo inatumika kwa asilimia sita tu:- (a) Je, kwa nini Kiwanda cha Saruji cha Dangote na Mtwara Cement Mkoani Mtwara havijapatiwa umeme wa gesi asilia hadi leo? (b) Je, kwa nini Wananchi wa Mtwara wasiunganishiwe gesi asilia kwenye nyumba zao?

Supplementary Question 1

MHE. AJALI R. AKBAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kuna taarifa ambazo ni rasmi, kwamba pamoja na kwamba Dangote amepatiwa gesi hii na baadhi ya viwanda vilivyopo Mkuranga, sasa vile viwanda vimeshindwa kutumia ile gesi katika kiwango ambacho ni tarajiwa. Ina maana wanatumia gesi pungufu na vingine vimetoa notice ya kufungwa.

Je, ni lini sasa Serikali itapunguza bei ya gesi hii ili viwanda hivi visifungwe?

Mheshimiwa Mwenyekiti, (b) nina taarifa rasmi vilevile kwamba kuna wawekezaji ambao walikuwa wametoka mashariki ya mbali; China na Uturuki, wapatao wanne ambao waliokuwa wamekusudia kuja kuwekeza hapa nchini. Ikumbukwe kwamba faida ya gesi siyo kwamba ni kwa kuuza tu, lakini vile viwanda vingeweza kulipa kodi, kutoa ajira na faida nyingine ambazo Taifa lingeweza kupata tija.

Mheshimiwa Mwenyekiti, inaonekana kwamba bei ya gesi yetu ni Dola 5.5 per metric tones wakati katika Soko la Dunia ni Dola 3.7 per metric tones. Sasa je, Serikali ina mkakati gani na kwa nini sasa isifanye sub…

MWENYEKITI: Swali, swali swali!

MHE. AJALI R. AKBAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali ni kwamba, naomba kwamba Serikali ipunguze bei ili wawekezaji hawa wasikimbie ili tupate faida nyingine zitokanazo na viwanda hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati napenda kujibu maswali mwili ya nyongeza ya Mheshimiwa Akbar, Mjumbe wa Kamati yetu ya Nishati na Madini. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri anayoifanya katika ushiriki wake kwa Kamati yetu inayosimamia Sekta yetu ya Nishati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali mawili aliyojielekeza; la kwanza Mheshimiwa Mbunge ameeleza namna ambavyo viwanda vilivyounganishiwa gesi ikiwemo Dangote na viwanda vya Mkuranga kwa mfano Goodwill, kwamba vinaona bei ya gesi ni kubwa; nataka nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba hilo suala limewasilishwa Wizarani; na kwa kuwa wapangaji wa gesi hii ni wa bei ya gesi asilia (EWURA) pamoja na Taasisi ya PURA ambayo ina- regulate Sekta ya Nishati upande wa gesi kuhusu masuala ya upstream, ni kwamba ndani ya Serikali jambo hili limepokelewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kupitia EWURA kwa kuwa ni kazi yao kupanga hizi bei za gesi itafanyia kazi kuangalia mchakato mzima. Pia ni lazima nikiri kwamba gharama ya uzalishaji wa gesi hapa nchini hii gesi ambayo inatumika ni zaidi ya shilingi USD 5.36. Kwa hiyo, utaona, lakini nia ya Serikali ni kuwezesha viwanda kutumia gesi na kuzalisha malighafi. Kwa hiyo, hili jambo limepokelewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili Mheshimiwa Mbunge ameulizia kwamba kuna wawekezaji kutoka nchi mbalimbali ambao wameonesha nia ya kuwekeza, sisi kama Serikali ya Awamu ya Tano kwa kweli imeandaa mazingira ya kukaribisha uwekezaji katika maeneo mbalimbali hasa viwanda vya mbolea katika Mkoa wa Mtwara na eneo la Kilwa. Hata sasa iliundwa Kamati ya Wataalam kufanya mapitio ya gesi hasa katika suala zima la kuwezesha viwanda hivi na wawekezaji katika kuwekeza kwenye suala la mbolea. Kwa hiyo, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge suala hili limefanyika, sasa hivi kinachofuata ni kikao baina ya wawekezaji na tangu mwezi wa Nne pia kilifanyika kwa ajili ya kupanga bei na kukubaliana. Hata wale wawekezaji kwa mfano Kampuni ya Helm na AG ya WD ya Egypt walishapewa mwelekeo na namna ya kufanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimthibitishie tu kwamba Serikali ipo tayari kuwakaribisha wawekezaji na waje tu na mazungumzo yanaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. AJALI R. AKBAR aliuliza:- Takwimu zilizopo zinaonesha kuwa gesi kutoka Mtwara na Songosongo inatumika kwa asilimia sita tu:- (a) Je, kwa nini Kiwanda cha Saruji cha Dangote na Mtwara Cement Mkoani Mtwara havijapatiwa umeme wa gesi asilia hadi leo? (b) Je, kwa nini Wananchi wa Mtwara wasiunganishiwe gesi asilia kwenye nyumba zao?

Supplementary Question 2

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Lindi na Mtwara ni Mikoa jirani sana. Katika majibu yake ya Msingi ya Mheshimiwa Naibu Waziri amesema gesi ya Mtwara itasambazwa majumbani katika Mkoa wa Mtwara, Pwani, pamoja na Dar es Salam, Lindi wameiruka. Sasa je, ni lini Lindi watasambaza gesi hii majumbani?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda tu kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kwamba ni kweli mpango wa kwanza unaanza na Mikoa mitatu ya Dar es Salaam pamoja na Mtwara na Lindi. Kwa sasa tumeanza kusambaza Dar es Salaam na tarehe 40 mwezi huu wataanza kujenga mabomba Mtwara na tarehe 30 mwezi Mei wataanza utaratibu wa kujenga mradi wa kusambaza gesi majumbani Lindi.