Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 18 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 147 2019-04-30

Name

Ajali Rashid Akibar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. AJALI R. AKBAR aliuliza:-

Takwimu zilizopo zinaonesha kuwa gesi kutoka Mtwara na Songosongo inatumika kwa asilimia sita tu:-

(a) Je, kwa nini Kiwanda cha Saruji cha Dangote na Mtwara Cement Mkoani Mtwara havijapatiwa umeme wa gesi asilia hadi leo?

(b) Je, kwa nini Wananchi wa Mtwara wasiunganishiwe gesi asilia kwenye nyumba zao?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Ajali Akbar, Mbunge wa Newala Vijiji, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa kiwanda cha Saruji cha Dangote kimeunganishwa na miundombinu ya gesi asilia ambapo awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mradi wa kuwezesha matumizi ya gesi asilia kuzalisha umeme kwa ajili ya kiwanda cha Dongote ilikamilika na kuanza kufanya kazi mwezi Agosti, 2018.

Aidha, hadi kufikia Mwezi Aprili, 2019 kiwanda cha Dangote kimeanza kutumia wastani wa futi za ujazo milioni tano kwa siku kwa kuzalisha umeme. Awamu ya pili ya mradi ilikamilika mwezi, Desemba, 2018 na sasa kiwanda cha Dangote kinatumia gesi ya wastani wa futi za ujazo milioni 15 hadi milioni 20 kwa siku kwa ajili ya uzalishaji wa Saruji. Jumla ya gharama za mradi ni shilingi bilioni 8,200.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa TPDC inaendelea na utekelezaji wa mradi kwa kuagiza na kujenga miundombinu ya usambazaji wa gesi asilia majumbani, viwandani na katika Taasisi mbalimbali kwa Mikoa ya Mtwara, Pwani na Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mradi wa kusambaza gesi asilia Mkoani Mtwara imeshaanza ambapo kwa sasa kazi ya ununuzi wa vifaa, mabomba, mita za kupimia gesi pamoja na vifaa vya kupunguza mgandamizo wa gesi inaendelea. Inategemewa zaidi ya Kaya 120 za awali zitaunganishwa mabomba ya gesi Mkoani Mtwara kwa matumizi ya nyumbani ifikapo Mwezi Juni, 2019.