Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Chemba?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwanza nishukuru kwa majibu ya historia ya Mheshimiwa Waziri. Halmashauri ya Wilaya ya Chemba tayari tumeshatoa jengo kwa ajili ya Hakimu wa Wilaya na Hakimu wa Wilaya ya Chemba ameshateuliwa kama Waziri hana habari. Sasa swali langu ni kwamba, kama majengo haya Waziri anasema inategemea na upatikanaji wa fedha ndio mahakama itajengwa, Hakimu ameteuliwa kuja kufanya nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, Mheshimiwa Waziri kwa taarifa tu ni kwamba, Wizara ya Mheshimiwa Waziri tayari imeshanunua kiwanja Chemba na wamekwenda kukikagua. Sasa anaponiambia hapa kwamba inategemea na upatikanaji wa fedha, naomba anihakikishie hizo fedha kwenye bajeti ya mwaka huu zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Mahakama ya Wilaya ya Chemba?

Name

Dr. Augustine Philip Mahiga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba pesa hizo zimetengwa na ninaposema upatikanaji wa pesa ni kama fedha hizo tukiziomba zilizotengwa tutaweza kuzipata kutoka Hazina ili tuzielekeze katika kufanya shughuli za kazi na huduma katika Wilaya ya Chemba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kumhakikishia hilo. Ahsante.