Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:- Baadhi ya wanawake huingia gerezani wakiwa na ujauzito na hivyo kujifungulia gerezani. (a) Je, ni huduma gani wanazopata ili kuhakikisha wanajifungua salama? (b) Je, ni jitihada gani zinafanywa ili kuwapatia akina mama hao vyakula vinavyopendwa na wajawazito?

Supplementary Question 1

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, nimshukuru Mheshimiwa Waziri na kumpa pongezi kwa majibu yake ambayo yanaonyesha nia ya dhati ya Serikali kuwasaidia wafungwa wanawake. Maswali yangu mawili yanyongeza ni kama ifuatavyo:-

(a) Je, Serikali inawasaidiaje watoto ambao wapo gerezani na mama zao kielimu na kisaikolojia kwa kuzingatia haki za watoto husasan wanapotumikia kifungo hicho ambacho watoto wao hawahusiki nacho?

(b) Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa wanawake wafungwa ambao ni wajawazito wakatumikie kifungo hicho nje ili waweze kuwalea watoto wao katika familia huru badala ya kuwa gerezani?

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Malembeka kwa jina maarufu Nyoka wa Kijani, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba wapo akina mama wafungwa ambao wanajifungua watoto wakiwa magerezani. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Nyoka wa Kijani, Nyara ya CCM kwamba utaratibu wa Jeshi la Magereza kupitia kanuni za Jeshi la Magereza watoto ambao wamekwishazaliwa magerezani wanpofikia umri wa kuanza awali wamekuwa wakisoma kwenye shule za awali zilizopo kwenye magereza zetu. Pia kwa kupitia watumishi wa magereza ambao wana utaalamu wa masuala ustawi wa jamii wamekuwa wakiwapa elimu pamoja na kuwafariji watoto hawa ili wajione wao siyo wafungwa ndani ya magereza isipokuwa wamezaliwa katika wakati ambao mama zao wapo magerezani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kwamba kwa nini wafungwa ambao wanajifungua magerezani wasipate adhabu nyingine badala ya kuwafunga magerezani. Tunao utaratibu kupitia sheria yetu ambayo inaitwa Probation for Offenders pamoja na Community Services, wale ambao wana vifungo chini ya miaka mitatu tumekuwa tukiandaa utaratibu wa kuwaondoa magerezani ili wawe na vifungo mbadala. Hata hivyo, kuna utaratibu watoto wanaokuwa magerezani wanapofikia umri ambao wanaweza wakaishi uraiani bila kuwa na mama zao ndugu zao wamekuwa wakishirikishwa ili waweze kutoa malezi kwa watoto ambao mama zao wapo magerezani. Ahsante sana.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:- Baadhi ya wanawake huingia gerezani wakiwa na ujauzito na hivyo kujifungulia gerezani. (a) Je, ni huduma gani wanazopata ili kuhakikisha wanajifungua salama? (b) Je, ni jitihada gani zinafanywa ili kuwapatia akina mama hao vyakula vinavyopendwa na wajawazito?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimwia Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Katika Gereza la Morogoro Mjini kuna msongamano mkubwa sana wa mahabusu na wafungwa hasa kwa upande wa wanawake. Je, kuna mkakati gani wa kupunguza msongamano huu wa wafungwa na mahabusu hasa wanawake kwenye Gereza la Morogoro?

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mkuu wa Mkoa Mstaafu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kuna msongamano kwa wafungwa na mahabusu katika magereza mbalimbali katika nchi yetu. Gereza alilolisema Morogoro ni mojawapo ya magereza yenye msongamano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali kupitia sheria mbalimbali tumekuwa tukijaribu kuzitumia ili kuwaondoa wafungwa ambao wana vifungo vifupi. Pia tumekuwa tukitumia Sheria yetu ya Parole kupunguza msongamano. Vilevile Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amekuwa akitoa msamaha kwa wafungwa ili kupunguza msongamano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kuwataka Watanzania popote pale walipo wasijihusishe katika uhalifu utakaowasababishia wawe wafungwa ama mahabusu. Waelewe kwamba watakapofanya uhalifu wataenda kwenye magereza ambazo zina msongamo. Kwa hiyo, nichukue fursa hii kuwasihi wasijihusishe katika uhalifu. Ahsante sana.

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:- Baadhi ya wanawake huingia gerezani wakiwa na ujauzito na hivyo kujifungulia gerezani. (a) Je, ni huduma gani wanazopata ili kuhakikisha wanajifungua salama? (b) Je, ni jitihada gani zinafanywa ili kuwapatia akina mama hao vyakula vinavyopendwa na wajawazito?

Supplementary Question 3

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa ujauzito ni kawaida kwa mwanamke yeyote kwa mfungwa au mtu aliyepo uraiani. Kwa hawa wafungwa ambao tayari ni wajawazito, kuna wakunga standby ili wawasaidie? Kwa sababu uchungu unakuja time yoyote na wapo ndani ya gereza, je, mnawawekea wazalishaji/wakunga standby wa kuwasaidia uchungu unapowajia?

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, kwamba kwenye Jeshi la Magereza, tunazo Zahanati na Vituo vya Afya ambapo wapo Madaktari wanaotoa utaalam wao kuhakikisha kwamba yale mahitaji yote ya akina mama katika kuhudhuria kliniki na kufuatilia siku za kujifungua wanazifanya kama kawaida. Pia tunao wakunga ambao siku zao zikifika wanawazalisha kama kawaida na hata vifaa vya kujifungulia wanavipata kama kawaida; na hata vile vyakula ambavyo akina mama, vinachochewa na mahitaji ya ujauzito; iwe ni udongo au chakula chochote kile wanaletewa kama kawaida. Ahsante sana.

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:- Baadhi ya wanawake huingia gerezani wakiwa na ujauzito na hivyo kujifungulia gerezani. (a) Je, ni huduma gani wanazopata ili kuhakikisha wanajifungua salama? (b) Je, ni jitihada gani zinafanywa ili kuwapatia akina mama hao vyakula vinavyopendwa na wajawazito?

Supplementary Question 4

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Mwuliza swali alitaka kujua msaada unaopatikana kwa hawa mama zetu wanaokuwa wajawazito Magerezani na kujifungua. Zipo taarifa kwamba wako baadhi ya wanawake wanaoingia wakiwa sio wajawazito lakini wakapata ujauzito ndani ya Magereza. Inaeleweka kwamba walinzi wa wafungwa wa kike ni wanawake, mimba hizi wanazipataje Mheshimiwa Waziri?

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa hakuna mimba ambazo zinatokea Magerezani. Hilo la kwanza. La pili, mimba tunazozizungumzia ni mimba ambazo mfungwa ama mahabusu anaingia gerezani akiwa tayari kule uraiani anakotoka ameshapata ujauzito.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana kulitokea jaribio hapa kwa Wabunge wakiwa wanataka tuweke sheria au utaratibu wa kuruhusu wenza wa mfungwa anayekuwa Gerezani ili waweze kupata fursa ya kwenda kufunguka wakiwa Gerezani, ya kwenda kujinafasi wakiwa Gerezani, lakini tulisema kwamba kwa sheria zetu na mila zetu, hatuwezi tukaruhusu hali hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.