Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 12 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 101 2019-04-17

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:-

Baadhi ya wanawake huingia gerezani wakiwa na ujauzito na hivyo kujifungulia gerezani.

(a) Je, ni huduma gani wanazopata ili kuhakikisha wanajifungua salama?

(b) Je, ni jitihada gani zinafanywa ili kuwapatia akina mama hao vyakula vinavyopendwa na wajawazito?

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Magereza limekuwa likihifadhi wafungwa wa aina zote wakiwemo wafungwa wa kike wajawazito. Katika kuhakikisha kwamba wafungwa wajawazito wanajifungua salama, Jeshi la Magereza limekuwa likitoa huduma za afya, chanjo na kuhakikisha wanahudhuria kliniki za mama wajawazito katika vituo vya afya vya magereza na pale inapobidi kuwapeleka hospitali za Serikali.

(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Magereza limekuwa likiwapatia wafungwa wajawazito vyakula wanavyovihitaji kiafya kwa kuzingatia maelekezo na ushauri wa Daktari wa gereza ili kuhakikisha afya ya mama na mtoto inalindwa. Aidha, Serikali inazidi kuboresha bajeti ya huduma hizo ili kuhakisha kwamba wafungwa wajawazito wanapata huduma hizo inavyostahili.