Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sonia Jumaa Magogo

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SONIA J. MAGOGO (K.n.y. MHE. MUSSA B. MBAROUK) aliuliza:- Wakazi wa Kata ya Kirare, Tongoni, Mzizima, Chongoleani, Mabokweni na Pongwe Wilayani Tanga Mjini ni wazalisaji wakubwa wa zao la muhogo lakini hawana soko la uhakika:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutafuta soko la uhakika wa zao la muhogo ndani na nje ya nchi? (b) Zipo mashine za kuchakata muhogo lakini bei zake ni kubwa na hivyo wakulima hawana uwezo wa kununua; je, Serikali haioni haja ya kuondoa kodi katika mashine hizo?

Supplementary Question 1

MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyogeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa wakulima wengi wa mihogo ni wadogowadogo na hawana mitaji na wamehamasishwa na wawekezaji kulima zao hili kwa wingi, je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wakulima hawa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, vilevile napenda kujua Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia elimu wakulima hawa ili waweze kuzalisha zao hili kwa wingi na kwa kiwango kinachohitajika?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Sonia Magogo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza kwamba wakulima wengi ni wadogo, hawana mitaji, kwa kweli hilo sio kwenye sekta ya kilimo cha muhogo peke yake bali wakulima wetu wengi hapa Tanzania hasa hawa wadogowadogo wanalima kilimo cha kawaida, kilimo cha kutegemea mvua.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la muhimu zaidi ni pale alipouliza katika sehemu ya pili ya swali lake kuhusu elimu, hilo ndilo jambo la muhimu zaidi kwa sababu elimu itahusu kilimo bora cha muhogo, utafiti na kutumia mbegu bora. Kwa hiyo, tunashirikiana kwa karibu sana sisi mapacha, Wizara ya Kilimo na Wizara ya Viwanda kuhakikisha kwamba mkulima anaongeza uzalishaji kutokana na ile elimu atakayopata kutoka kwa Maafisa Ugani walioko kwenye kata na vijiji. Hilo ndiyo jambo la msingi sana. Waziri wa Kilimo ameshaagiza Maafisa Kilimo wote nchini wale ambao hawajayajua vizuri mazao fulani kwenye maeneo yao wanatakiwa wapatiwe mafunzo wao wenyewe kwanza kabla hawajaenda kuwapatia wakulima. Ahsante sana.

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. SONIA J. MAGOGO (K.n.y. MHE. MUSSA B. MBAROUK) aliuliza:- Wakazi wa Kata ya Kirare, Tongoni, Mzizima, Chongoleani, Mabokweni na Pongwe Wilayani Tanga Mjini ni wazalisaji wakubwa wa zao la muhogo lakini hawana soko la uhakika:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutafuta soko la uhakika wa zao la muhogo ndani na nje ya nchi? (b) Zipo mashine za kuchakata muhogo lakini bei zake ni kubwa na hivyo wakulima hawana uwezo wa kununua; je, Serikali haioni haja ya kuondoa kodi katika mashine hizo?

Supplementary Question 2

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na jitihada za Serikali kuona inainua kilimo hiki au zao hili la muhogo ambalo ni tegemeo kubwa hususan kwa watu wa Mikoa ya Kanda ya Mashariki, lakini zao la muhogo linakabiliwa na magojwa ya Cassava Mill Bags. Je, nini kauli ya Serikali kukabiliana na wadudu hawa ambao wanaathiri sana zao la muhogo ambalo linawarudisha nyuma wakulima wanaolima zao hili?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Alichokisema ni kweli kabisa na haya masuala ya magonjwa ya mazao siyo kwamba yapo kwenye kilimo cha muhogo peke yake, bali mazao mengi yamekuwa yakiathiriwa sana na wadudu. Mheshimiwa Waziri wa Kilimo ameshatoa msisitizo na ametoa maagizo kwamba viuatilifu ambavyo ni feki visitumike kwenye mazao. Yeyote ambaye atakamatwa anauza au anampatia mkulima viuatilifu feki ambavyo havisaidii kupambana na magonjwa na wadudu atachukuliwa hatua kali na Serikali. Kwa hiyo, hiyo ni elimu mojawapo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imechukua hatua za makusudi kabisa na kupitia vituo vya utafiti kikiwemo Kituo cha Utafiti cha Naliendele na kituo cha utafiti ambacho kipo chini ya Wizara ya Kilimo cha pale Dar es Salaam wamefanya utafiti mzuri wa mbegu ambayo inahimili magonjwa kama hayo. Kwa hiyo, msisitizo ni kutumia mbegu ambazo zinahimili matatizo hayo.

Name

Justin Joseph Monko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. SONIA J. MAGOGO (K.n.y. MHE. MUSSA B. MBAROUK) aliuliza:- Wakazi wa Kata ya Kirare, Tongoni, Mzizima, Chongoleani, Mabokweni na Pongwe Wilayani Tanga Mjini ni wazalisaji wakubwa wa zao la muhogo lakini hawana soko la uhakika:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutafuta soko la uhakika wa zao la muhogo ndani na nje ya nchi? (b) Zipo mashine za kuchakata muhogo lakini bei zake ni kubwa na hivyo wakulima hawana uwezo wa kununua; je, Serikali haioni haja ya kuondoa kodi katika mashine hizo?

Supplementary Question 3

MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo walilonalo wananchi wa Tanga linafanana sana na tatizo walilonalo wananchi wa Mkoa wa Singida. Jimbo la Singida Kaskazini na Mkoa wa Singida kwa ujumla ni wakulima wakubwa sana wa vitunguu pamoja na alizeti. Hivi tunavyozungumza, soko la kitunguu gunia moja linauzwa kati ya shilingi 10,000/= mpaka shilingi 40,000/=, badala ya shilingi 80,000/= mpaka shilingi 120,000/= ilipokuwa katika msimu wa mwaka uliopita.

Je, Serikali iko tayari kuingilia kati suala hili na kuwanusuru wananchi ambao wanaendelea kupata hasara kutokana na kazi kubwa waliyofanya?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli alichokisema. Kwanza tunatoa tahadhari kwa Watanzania, wakulima pamoja na wafanyabiashara, lipo tatizo hapa nchini ambalo ni kubwa, watu wanakuja katika vijiji kununua, wengine wananunua kwenye mashamba bila kufuata utaratibu. Hilo tunashirikiana na Wizara ya Kilimo na tunashirikiana na Shirika la Vipimo kuhakikisha kwamba utaratibu wa kisheria unafuatwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, hao watu ambao wamekuwa wananunua halafu wanasafirisha nje ya nchi bila kuwa na vifungashio vinavyokubalika kisheria, hao wanakiuka sheria na kwa kweli itabidi tuchukue hatua kali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kuingilia kati suala la bei, namuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaingilia kati na tutatoa maagizo kwa maandishi kuanzia leo.