Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza:- Mipaka ya Mradi wa Mafunzo ya Msitu wa Kijiji cha Igwata, Kata ya Nyabubinza, Wilaya ya Maswa imepanuliwa na kuchukua baadhi ya Mashamba ya Wanakijiji na hivyo kusababisha wananchi kukosa maeneo ya kulima:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalipa fidia wananchi hao ili waweze kununua maeneo mengine ya kufanya shughuli zao za kilimo?

Supplementary Question 1

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mimi ndiye mwakilishi wa wananchi wa Kijiji cha Igwata na Jimbo la Maswa Magharibi. Msitu huu ulipanuliwa na wakati wanapanua hawakushirikisha wananchi, ukamega mashamba ya watu. Sasa nataka niulize maswali ya nyongeza. Moja; kwa nini Serikali isirejeshe mashamba haya yaliyomegwa kwa wananchi ili waendelee kuyatumia kwa shughuli zao za kilimo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, sehemu ya mashamba au eneo lililomegwa kuna makazi ya watu, Serikali inasemaje juu ya watu hawa ambao wameweka makazi kwenye eneo ambalo limeongezwa? (Makofi)

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mashimba Ndaki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze sana Mheshimiwa kwa namna ambavyo amekuwa akifuatilia sana malalamiko ya wananchi wake ambayo yalitokana na uwekaji wa alama. Sisi kwenye Wizara yetu kimsingi hatukuchukua mashamba mapya ila tuliweka alama, lakini naomba nimpongeze sana kwa namna alivyofuatilia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zoezi ambalo tunaendelea nalo sasa katika Wizara yetu ni kupitia upya malalamiko yote yanayoletwa na Waheshimiwa Wabunge pamoja na viongozi wa Serikali katika maeneo husika. Kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Mbunge kama uchukuaji wa eneo hili una malalamiko, Wizara yetu inapokea malalamiko hayo na tunatekeleza agizo la Mheshimiwa Rais la kuhakikisha kwamba, tunarejesha maeneo ambayo yana malalamiko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali lake la pili, iwapo kuna wakazi ambao wakati wa uwekaji wa mipaka hii walikumbwa na zoezi hili nitamtuma Afisa wetu wa TFS kwenda kuangalia. Iwapo itathibika kwamba, maeneo hayo wananchi bado wanayahitaji tuta-review mipaka ili kuweza kuwaachia waweze kukaa.

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza:- Mipaka ya Mradi wa Mafunzo ya Msitu wa Kijiji cha Igwata, Kata ya Nyabubinza, Wilaya ya Maswa imepanuliwa na kuchukua baadhi ya Mashamba ya Wanakijiji na hivyo kusababisha wananchi kukosa maeneo ya kulima:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalipa fidia wananchi hao ili waweze kununua maeneo mengine ya kufanya shughuli zao za kilimo?

Supplementary Question 2

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza. Wananchi walioko Urambo katika Kata za Senda, Ukondamoyo na hasa Kijiji cha Yueta wana matatizo makubwa sana ya migogoro ya ardhi kutokana na kupakana na Pori la Akiba la Ugawa na kuwasababishia kukosa nafasi ya kulima na kufanya shughuli zao za mifugo. Je, Serikali itakuja lini Urambo kutatua tatizo hili ili wananchi hawa wanaopakana na Pori la Ugawa wafanye shughuli zao za kilimo na mifugo kwa raha? Ahsante.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Margaret Sitta, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Mashimba Ndaki, tumeelekezwa kupitia upya mipaka na malalamiko ya wananchi kwenye maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge anasema. Kwa hiyo, katika zoezi hili linaloendelea namwomba Mheshimiwa Margareth Sitta kwa sababu, wanaoleta malalamiko haya ni Halmashauri na Mkoa, atuletee malalmiko haya na tutayafanyia kazi.

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza:- Mipaka ya Mradi wa Mafunzo ya Msitu wa Kijiji cha Igwata, Kata ya Nyabubinza, Wilaya ya Maswa imepanuliwa na kuchukua baadhi ya Mashamba ya Wanakijiji na hivyo kusababisha wananchi kukosa maeneo ya kulima:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalipa fidia wananchi hao ili waweze kununua maeneo mengine ya kufanya shughuli zao za kilimo?

Supplementary Question 3

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona. Mheshimiwa Rais alipokuja Mkoani Morogoro kwa ziara aliagiza wananchi wa Mtaa wa CCT Mkundi ndani na Manispaa ya Morogoro wasibughudhiwe, lakini hivi sasa Maafisa wa Maliasili wameendelea kuwabughudhi wananchi wale. Je, ni kwa nini maafisa hawa wanapuuza agizo la Mheshimiwa Rais?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Minja, Mbunge wa Viti Maalum Morogoro, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Maafisa wetu wa Maliasili, kwa maana ya TFS, wamekuwa wakisimamia sheria hasa kuangalia mipaka ya kihalali ambayo ipo katika maeneo husika, lakini kama kuna maagizo ambayo yalitolewa na Mheshimiwa Rais kwamba, wananchi wasibughudhiwe, nitakwenda kufuatilia kuona ni kwa namna gani maafisa hao wanakiuka na tutatoa maelekezo.