Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 10 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 112 2019-02-08

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza:-

Mipaka ya Mradi wa Mafunzo ya Msitu wa Kijiji cha Igwata, Kata ya Nyabubinza, Wilaya ya Maswa imepanuliwa na kuchukua baadhi ya Mashamba ya Wanakijiji na hivyo kusababisha wananchi kukosa maeneo ya kulima:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalipa fidia wananchi hao ili waweze kununua maeneo mengine ya kufanya shughuli zao za kilimo?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mashimba Mashauri Ndaki, Mbunge wa Maswa Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Msitu wa Hifadhi ya Igwata unahifadhiwa kisheria kwa Tangazo la Serikali Na. 324 la Mwaka 1953. Msitu huo una eneo la ukubwa wa hekta 132,851 ambapo hekta 85.19 ziko Wilaya ya Kwimba na hekta 47.678 ziko Wilaya ya Maswa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakala wa Huduma ya Misitu Tanzania ilianza kusimamia Msitu wa Igwata tangu mwaka 2010. Aidha, tangu kuanzishwa kwake mwaka 1953 msitu huu haujawahi kupanuliwa; katika mwaka 1915/1916 kazi zilizofanyika ilikuwa ni uimarishaji wa mpaka, uwekaji wa maboya ambao ulifanywa na TFS kwa kushirikiana na uongozi wa vijiji vyote vinavyozunguka msitu huo. Vilevile mwaka 2015/2016 kazi ya tathmini, Forest Inventory, ilifanyika kwa ajili ya kutayarisha mpango wa usimamizi wa msitu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara haijawahi kupokea malalamiko au madai yoyote ya wananchi kuchukuliwa mashamba yao kwa lengo la kuongeza ukubwa wa eneo la msitu. Aidha, hakuna mgogoro kati ya wananchi na taasisi zinazosimamia msitu huu, wananchi wanaendelea kutoa ushirikiano katika usimamizi na ulinzi wa msitu huo ambao ni hazina kubwa ya mbegu za miti asilia na urithi wa aina ya miti iliyopo katika hatari ya kutoweka ambayo inatumika katika tiba za jadi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.