Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakarabati mifereji ya maji ya mvua na kuta za mito inayoingiza maji ya bahari katika Mji wa Mikindani ili kuirejesha katika hali yake ya awali?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri; hata hivyo, nina maswali mawili ya nyongeza. Mji wa Mikindani ni miongoni mwa miji ambayo iko chini ya usawa wa bahari; kwa hiyo hii mifereji ninayoizungumzia ni ile ambayo maji ya bahari yakijaa inapitisha maji kuingia katikati ya mji na iko mingi na tangu zamani hii mifereji ilikuwa imejengewa lakini kutokana na uwezo mdogo wa halmashauri imeshindwa kuifanyia ukarabati mara kwa mara. Swali, je, Serikali iko tayari kuisaidia Manispaa ya Mtwara – Mikindani katika kukarabati mifereji hii ya Mji wa Mikindani kwa sababu kuiachia manispaa peke yake ni kuiongezea mzigo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, Mheshimiwa Naibu Waziri yupo tayari kwenda Mikindani kuona hicho ninachokizungumzia ili aweze kunielewa zaidi na hatua za haraka ziweze kuchukuliwa?

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika,
nichukue fursa hii kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Abdulrahman Ghasia, Mbunge wa Mtwara Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabla sijajibu swali na mimi nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa juhudi zake na ushirikiano mkubwa ambao anatupa sisi Wizara ya Mazingira katika kukabiliana na hali hii ya mazingira.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na swali lake la kwanza; kwanza nipo tayari na tupo tayari pia kusaidia maeneo yote kama ambavyo nimeeleza kwenye jibu langu la swali la msingi, kuhakikisha kwamba maeneo yote haya tunajitahidi ili tunakabiliana na mabadiliko ya tabia nchi kupitia mifuko ambayo tunapata fedha kutoka kwa wenzetu, kwa maana ya Global Climatic Change.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kuhusu kwenda Mtwara. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba ninayo ziara ya kuanzia tarehe 18 Iringa, lakini pia kwenda Mtwara, Njombe, Ruvuma, Lindi na baadaye nitakwenda Mtwara kwa ajili ya kuhakikisha kwamba najionea mazingira halisi ya hiyo mifereji ambayo ameitaja.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakarabati mifereji ya maji ya mvua na kuta za mito inayoingiza maji ya bahari katika Mji wa Mikindani ili kuirejesha katika hali yake ya awali?

Supplementary Question 2

MHE. YUSSUF S. HUSSEIN: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, naomba niulize swali dogo la nyongeza kwa Mheshimiwa Waziri. Hii mito ambayo inatoka baharini na kuingia nchi kavu inakuwa na kasi sana wakati yale maji yapoingia ama yanapotoka, kwa sababu tabia ya bahari, maji yanapojaa yanakuwa yana nguvu sana na yanapotoka vilevile yanakuwa na nguvu. Maana yake ni kwamba ongezeko la soil erosion linakuwa kubwa kuliko linavyotarajiwa. Ni upi sasa mkakati wa Kitaifa wa Serikali kwa sababu ardhi yetu inapungua kwa kasi? Msimbati itakuwa ni moja kati mfano mzuri wa kasi wa maji haya.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni upi mkakati hasa wa Kitaifa wa Serikali kudhibiti suala hili la erosion katika kingo za bahari zetu?

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa Serikali ulishaanza na nitoe mifano, ukiangalia kingo za bahari pale Ocean Road tumejenga. Pia ukienda Pangani tumejenga na maeneo mengine tutaendelea kadri ambavyo tutakapokuwa tunapata fedha za kuhakikisha tunakabiliana na haya mabadiliko ya tabia nchi. (Makofi)